Anachofanya Fei Toto Sasa kwa Hersi ni kulijambia jiwe

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Mwl wangu wa shule ya msingi alinichapia hadithi ya fisi, mfupa na jiwe. Alisema, siku moja fisi mwenye njaa Kali alikiona kitu cheupe mbali kabisa akidhani kuwa ulikuwa ni mfupa unaofaa kula na kuponya njaa yake kali. Pamoja na njaa yake alikimbia umbali mrefu kuufuata "mfupa" aliouona kwa mbali. Baada ya kufika eneo la tukio aligundua kuwa haujuwa mfupa bali jiwe jeupe, hata hivyo hakuamini kama ule haujuwa mfupa, hivyo akaupiga jino ili kuhakikisha hadi akapoteza jino lake moja. Kwa hasira fisi aliligeukia na kulijambia na kusema na wewe harufu ya ushuzi wangu umeipata, kisha huyooo akaondoka na njaa yake kwa taabu sana.

Fei Toto sasa baada ya kushindwa kufanikisha dili lake ameamua kuzungumza na kutupa lawama kwa eng. Hersi kama mtu mbaya sana na aliyesababisha aondoke siku moja kabla Ya mechi ya Yanga vs Azam fc kama vile alikuwa na mpango wa kuisaidiia Azam ishinde mechi ile.

Kufanya hivi ni sawa na kulijambia jiwe ili linuke harufu ya ushuzi angalau, maana baada ya Fei Toto kuondoka Yanga imetwaa ubingwa, imeingia fainali ya kombe la Azam cup na kucheza finali za CAF na kuhama timu hahami hadi mkataba wake uishe.
 
afu alivyo chizi anatupima tumchague nani kati yake injinia CHIZI KWELI DOGO
 
Aise hhhhh
 
afu alivyo chizi anatupima tumchague nani kati yake injinia CHIZI KWELI DOGO
Uwezo wake kiakili sio mkubwa, anasema kati ya mambo yaliyomkimbiza Yanga ni manyanyaso, kuambiwa kauza mechi, mishahara alikuwa hapati kwa wakati na watu kumtukana bi mkubwa wake. Anasahau kuwa kabla ya yeye kuondoka Yanga siku moja kabla ya mechi na Azam hakuna mtu ambae alikuwa anafahamu Wala kumtaja bi mkubwa wake, bi mkubwa alifahamika baada ya kujitokeza mwenyewe kuwaudhi watu wenye hasira na mwanawe. Mechi ya kwanzA mwanawe Fei aliifunga Azam, kuondoka ghafla siku moja kabla ya mechi ya pili na Azam ilitafsiriwa kama hujuma ya Azam kwa Yanga kupitia Fei Toto, kifupi Fei Toto aliuza mechi.

Fei Toto aliona kitu cheupe kuleeee akatimua mbio kudhani ni mfupa aponye njaa yake kumbe haukuwa mfupa, ameona njia rahisi kwake ni kumjambia Eng. Hersi ushuzi. Hivi kweli jiwe linaathiriwa na ushuzi? Hata ukilinyea jiwe litasikitika? Hivi ni kweli wadau wa Yanga wanaweza kumchagua Fei Toto dhidi ya eng. Hersi? Hapo ndipo uwezo wake wa kiakili unapoweza kupimwa. Hata timu inayomtaka Faisal itashitushwa na aina hii ya kufikiria ya mchezaji wao tarajiwa.
 
Hahaaa, kwahiyo anataka Eng anuke.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…