Anahitajika mtaalamu (mganga) wa kumgandisha mwizi na mali aliyoiba sehemu alipoibia

Anahitajika mtaalamu (mganga) wa kumgandisha mwizi na mali aliyoiba sehemu alipoibia

makaveli10

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2013
Posts
31,583
Reaction score
92,670
Ndugu zangu nimekwama, tena nimekwama haswa. Nimegadhibika pasina mfano 😠😡, mimi si mtu wa kwenda vilingeni ila kwa hili Mola wangu anisamehe sana.

Shambani nina minazi takribani 100 ila siambulii kitu,
Hawa waduwanzi naona sasa wanaleta mazoea yasiyovumilika. Zamani kila baada ya miezi mitatu nilikuwa navuna nazi najaza canter ya tani 4 vizuri tu. Taaratiiibu mambo yakawa yanabadilika, nazi 2000+ zikaja kuwa navuna nazi 800+, ikashuka ikawa naambulia nazi 300+, ikaja nazi 100 na hapo ni za kutafuta haswa, naangua mpaka ambazo si kavu.

Hawajatosheka sasa wanaangua mpaka madafu, nafika nakuta minazi hakuna kitu, nimevumilia nimechoka.
Hii ni tabia ambayo kijiji kile imeota pembe. Sasa basi nahitaji mtaalam ambae anaweza kumgandisha mtu shambani na zigo lake aliloiba, sitaki kuua wala kutiana uchizi, nataka nimkute mtu yupo shambani mwangu na zigo lake la nazi.

Malipo ni baada ya kazi kufanyika na matokeo chanya kupatikana.

Ninajaribu kuwatag kina mshanajr, mzizimkavu, likud na wengineo inagoma.
 
Tupac amekuweje siku hz🤔
Si bora hivi, ningekuwa na chamoto nishampiga mtu cha matako, kuna vitu vinakera saana mzee, mwanzo walikuwa wanaiba naambulia nazi 2000 sio kesi kabisa yaani, napata naridhika, sio siku hizi siambulii kitu kabisa. 😠😡
 
😂 😂 😂 Sitamani iwe hivyo, nataka nikamate mwenyewe, iwe fundisho kwa wengine..
Ila aibu sana na kujiendekeza wizi.Kwa mfano,unanikuta pale nakuibia nazi halafu nina "kishkwambi" changu kina app ya JF!Kesho yake tangazo kubwa:
BABA BHOKE MWIZI WA NAZI NA MADAFU.
😂😂😂😂😂😂
 
Si bora hivi, ningekuwa na chamoto nishampiga mtu cha matako, kuna vitu vinakera saana mzee, mwanzo walikuwa wanaiba naambulia nazi 2000 sio kesi kabisa yaani, napata naridhika, sio siku hizi siambulii kitu kabisa. 😠😡
🤣 Chonga mifagio mkuu Nazi zishapata wenye nazo au kuti hazianguki ??
 
Bwana Tupac, tuanze kwanza hilo eneo minazi ilipo, je ni lindi au ni upande gani?
 
Ila aibu sana na kujiendekeza wizi.Kwa mfano,unanikuta pale nakuibia nazi halafu nina "kishkwambi" changu kina app ya JF!Kesho yake tangazo kubwa:
BABA BHOKE MWIZI WA NAZI NA MADAFU.
😂😂😂😂😂😂
Bora hata wangekuwa wanaiba kiasi, wasenge wannapuruwa kila kitu na inasemekana kuangua angua madafu kuna changia kua kabisa mnazi. 😠😡
 
Jenga kibanda kisha uweke mlinzi.
Mzee kuna nyumba kabisa, kuna mtu yupo, nami huwa nalala huko wakati mwingine, lengo haswa nihamie huko moja kwa moja nikimaliza michakato fulani town, ila bado haijawa solution.
Wanaibiwa wenyeji wa huko, unalala ndani mtu anaiba nje.
Waduwanzi wanakuja usiku wanapanda na viroba huko au kamba wanakata kole zima wanashusha kwa kamba, husikii chochote.
 
Back
Top Bottom