BornTown
JF-Expert Member
- May 7, 2008
- 1,716
- 482
Nimeombwa ushauri na rafiki yangu mmoja nimekosa jibu la kumpa issue yenye iko hivi:
Ni mkaka wa miaka 40 alikuwa na mahusiano na mdada mmoja wakaja wakaachana kutokana na huyo mkaka kupata mwanamke mwingine ka kipindi cha miezi 3 cha urafiki mpya na huyo mwanamke mwingine wakafunga ndoa kanisa katoliki waliishi mwakamiaka 2 na nusu wakakorofishana.
Hapo walijaliwa kupata mtoto wa kike na wakiume baada ya kukorofishana mwanamama akakimbilia kwako anadai chanzo ni wivu wa mke kupitiliza mke hataki baba aongee na mwanamke yeyote yule hata kazini kwa baba asizungumze na mwanamke hata kama wanafanya wote kazi.
Ukija mtaani mama hataki mahusiano na wenzie akiona mama wa jirani akimsalimia mumewe ni ugomvi sasa alicho kifanya akavuruga pale mtaani kwake hivi anamfuata mke wa jirani anamwambia mumeo kanitongoza halafu anaenda kwa mume anamwambia mkeo anatembea na mume wangu.
Ikumbukwe anafanya hivyo kwa kila familia pale mtaani kwao alifanya hivyo kwa majirani zake karibu 10 ss ukawa ugomvi mke anamtuhumu mume na mume anamtuhumu mke.
Mwisho wasiku wanaume wakaitana wakaa wakaamua kumwita huyu kaka wampe kubwa walipanga kumfanyia kitu mbaya sana huyo kaka wakiamini kuwa ni kweli anatembea na wake zao.
Sasa basi wakati wanayapanga hayo yule kaka tokea kwenye ile bar waliokaa akawasalimia hakuna aliye mjibu akawashangaa jirani zake wamekuwaje akamfuata mmoja ambaye ni mkubwa kuliko wote ni mtu mzima akamwambia mzee nina shida nataka kukueleza jambo.
Basi yule baba akamsililiza yule kaka akamwambia mkewe anamtuhumu mambo ambayo hayawahi kuyafanya na wala hategemei kuyafanya pale mtaani wanaume wakakaa wakayaongea wakakubalia jmosi inayofuata jumuiya inafanyika kwa huyo mkaka basi watakaa wayaongee.
Wakarudi majumbani mwao kila mtu akamweleza mkewe kuwa jmosi tutayamaliza maneno yote tukitoka jumuiya. Mmoja wa hao kinamama akamfuata mke wa huku kaka akamweleza kuwa jmosi tunakuja kukata mzizi wa fitina.
Mke kuambiwa hivyo akatahamaki akasubiri mgeni ametoka akapiga simu kwao akaita kenta akasomba kila kitu akakimbilia kwao mume kurudi jioni nyumba nyeupe kama wanataka kuhamia akipiga simu ya mkewe haipokelewi akawauliza majirani wamakwambia mkeo ndie alihamisha vitu.
Basi kaka wa watu akaenda nyumbani kwa wakwe zake kumfuata mke kujua tatizo akafika na kupokelewa na matusi mama na baba mkwe wanamtukana kuwa amepanga yeye na jirani zake kwenda kumuua binti yao.
Uzuri yule kaka alitoka na yule mzee mtaani kwake ili amsindikize yule baba alishangaa kusikia yale maneno toka kwa wale wazee. Akajaribu kuwaeleza wale wazee walichofanya ni kuwafungulia mbwa na kuwaitia makelele ya wezi wakakimbia kunusuru maisha yao.
Hadi sasa ni mwaka wa 4 unaenda yule dada hajarudi kwa mume na hataki mume awaone watoto. Sasa ushauri anaomba ni
Je akienda mahakamani huyu kaka kudai talaka na apate haki ya kukaa wa watoto wake
Pili ili aoe tena na je kanisa katoliki litamruhusu kufunga tena ndoa kanisani?
Sheria inachukua muda gani kutoa talaka maana ngazi zote ameshapitia ustawi wa jamii imeshindikana mabaraza ya wazee nao imeshindikana aombeni ushauri nimsaidieje.
Ni mkaka wa miaka 40 alikuwa na mahusiano na mdada mmoja wakaja wakaachana kutokana na huyo mkaka kupata mwanamke mwingine ka kipindi cha miezi 3 cha urafiki mpya na huyo mwanamke mwingine wakafunga ndoa kanisa katoliki waliishi mwakamiaka 2 na nusu wakakorofishana.
Hapo walijaliwa kupata mtoto wa kike na wakiume baada ya kukorofishana mwanamama akakimbilia kwako anadai chanzo ni wivu wa mke kupitiliza mke hataki baba aongee na mwanamke yeyote yule hata kazini kwa baba asizungumze na mwanamke hata kama wanafanya wote kazi.
Ukija mtaani mama hataki mahusiano na wenzie akiona mama wa jirani akimsalimia mumewe ni ugomvi sasa alicho kifanya akavuruga pale mtaani kwake hivi anamfuata mke wa jirani anamwambia mumeo kanitongoza halafu anaenda kwa mume anamwambia mkeo anatembea na mume wangu.
Ikumbukwe anafanya hivyo kwa kila familia pale mtaani kwao alifanya hivyo kwa majirani zake karibu 10 ss ukawa ugomvi mke anamtuhumu mume na mume anamtuhumu mke.
Mwisho wasiku wanaume wakaitana wakaa wakaamua kumwita huyu kaka wampe kubwa walipanga kumfanyia kitu mbaya sana huyo kaka wakiamini kuwa ni kweli anatembea na wake zao.
Sasa basi wakati wanayapanga hayo yule kaka tokea kwenye ile bar waliokaa akawasalimia hakuna aliye mjibu akawashangaa jirani zake wamekuwaje akamfuata mmoja ambaye ni mkubwa kuliko wote ni mtu mzima akamwambia mzee nina shida nataka kukueleza jambo.
Basi yule baba akamsililiza yule kaka akamwambia mkewe anamtuhumu mambo ambayo hayawahi kuyafanya na wala hategemei kuyafanya pale mtaani wanaume wakakaa wakayaongea wakakubalia jmosi inayofuata jumuiya inafanyika kwa huyo mkaka basi watakaa wayaongee.
Wakarudi majumbani mwao kila mtu akamweleza mkewe kuwa jmosi tutayamaliza maneno yote tukitoka jumuiya. Mmoja wa hao kinamama akamfuata mke wa huku kaka akamweleza kuwa jmosi tunakuja kukata mzizi wa fitina.
Mke kuambiwa hivyo akatahamaki akasubiri mgeni ametoka akapiga simu kwao akaita kenta akasomba kila kitu akakimbilia kwao mume kurudi jioni nyumba nyeupe kama wanataka kuhamia akipiga simu ya mkewe haipokelewi akawauliza majirani wamakwambia mkeo ndie alihamisha vitu.
Basi kaka wa watu akaenda nyumbani kwa wakwe zake kumfuata mke kujua tatizo akafika na kupokelewa na matusi mama na baba mkwe wanamtukana kuwa amepanga yeye na jirani zake kwenda kumuua binti yao.
Uzuri yule kaka alitoka na yule mzee mtaani kwake ili amsindikize yule baba alishangaa kusikia yale maneno toka kwa wale wazee. Akajaribu kuwaeleza wale wazee walichofanya ni kuwafungulia mbwa na kuwaitia makelele ya wezi wakakimbia kunusuru maisha yao.
Hadi sasa ni mwaka wa 4 unaenda yule dada hajarudi kwa mume na hataki mume awaone watoto. Sasa ushauri anaomba ni
Je akienda mahakamani huyu kaka kudai talaka na apate haki ya kukaa wa watoto wake
Pili ili aoe tena na je kanisa katoliki litamruhusu kufunga tena ndoa kanisani?
Sheria inachukua muda gani kutoa talaka maana ngazi zote ameshapitia ustawi wa jamii imeshindikana mabaraza ya wazee nao imeshindikana aombeni ushauri nimsaidieje.