Anataka Kutoa Mimba -Nimemkatalia

Anataka Kutoa Mimba -Nimemkatalia

Status
Not open for further replies.

Regia Mtema

R I P
Joined
Nov 21, 2009
Posts
2,970
Reaction score
866
Nikiwa nimekaa nyumbani kwangu jana usiku nikifuatilia tamthlia ya Ruby mara nikapata mgeni.Mgeni huyu ni jirani yangu.Akaniomba nitoke nje ili tukaongelee huko.Akanileleza habari yake kwa kirefu.Kifupi ni kwamba yeye ni binti wa miaka 33 ana mtoto aliyemaliza darasa la saba mwaka jana na mtoto huyo amechaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza hapa jijini Dar es salaam.Anasema kwamba mtoto huyu baba yake alimkataa tangu akiwa mimba hovyo kwa kipindi cha miaka yote hii amekuwa akimtunza yeye mwenyewe.Yeye anafanya kazi za kubahatisha.Baada ya mtoto wake huyu kufaulu anahitaji mahitaji mbalimbali ya kumfanya aweze kwenda shule na yeye uwezo hana.Baada ya kutafakari kwa kina akaona bora amtafute mwanaume fulani aliyekuwa akimtongoza siku za nyuma kwa lengo la kuomba msaada wa fedha ili mwanae aende shule.Jamaa akampa masharti huyu dada kwamba kama anataka kumsadia ni lazima akubali afanye naye mapenzi.Mdada hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali..Anasema baada ya kufanya mapenzi na bwana huyu,bwana huyu akaingia mitini bila kumpa dada huyu ujira wake..Hivi sasa dada huyu ni mjamzito na jamaa hapokei kabisa simu za huyu dada..Dada huyu kanifuata jana na kutaka nimpe hela ili aende akatoe mimba kwani anadai hawezi kuzaa mtoto mwingine asiye na baba.Imani yangu ya dini hairuhusu kutoa mimba wala mimi mwenyewe kama mwanaharakati siungi mkono suala la kutoa mimba..Nimemkatalia kabisa,najua ujirani wetu uko mashakani..Niko njia panda.
 
Good manners are of more importance than Laws

GS ni hivyo tu kwa sasa
 
kwakweli upo sahihi na simamia msimamo wako na jaribu kumshauri vizuri na kumpa madhara ya kutoa mimba kwani ukimpa msaada ni kwamba na ww umeshiriki dhambi ya kuua asilimia mia
 
Kama utapata nafasi tena ya kuweza kuzungumza naye fanya hivyo. Mweleze nini hasara ya kutoa mimba si kwamba ni kinyume tu na mapenzi ya mungu bali pia kwa afya yake na umuhimu wa uhai kwa kiumbe alichobeba. Awe mvumilivu ataweza kama ameweza kwa huyo aliye naye sasa na huyu naye mungu atamjalia ataweza. Azikatae nguvu za shetani na mambo yake katika hili. Mungu ni mwema kwetu sote ndio maana alituumba kwa mfano wake.
 
Nikiwa nimekaa nyumbani kwangu jana usiku nikifuatilia tamthlia ya Ruby mara nikapata mgeni.Mgeni huyu ni jirani yangu.Akaniomba nitoke nje ili tukaongelee huko.Akanileleza habari yake kwa kirefu.Kifupi ni kwamba yeye ni binti wa miaka 33 ana mtoto aliyemaliza darasa la saba mwaka jana na mtoto huyo amechaguliwa kuendelea na kidato cha kwanza hapa jijini Dar es salaam.Anasema kwamba mtoto huyu baba yake alimkataa tangu akiwa mimba hovyo kwa kipindi cha miaka yote hii amekuwa akimtunza yeye mwenyewe.Yeye anafanya kazi za kubahatisha.Baada ya mtoto wake huyu kufaulu anahitaji mahitaji mbalimbali ya kumfanya aweze kwenda shule na yeye uwezo hana.Baada ya kutafakari kwa kina akaona bora amtafute mwanaume fulani aliyekuwa akimtongoza siku za nyuma kwa lengo la kuomba msaada wa fedha ili mwanae aende shule.Jamaa akampa masharti huyu dada kwamba kama anataka kumsadia ni lazima akubali afanye naye mapenzi.Mdada hakuwa na jinsi zaidi ya kukubali..Anasema baada ya kufanya mapenzi na bwana huyu,bwana huyu akaingia mitini bila kumpa dada huyu ujira wake..Hivi sasa dada huyu ni mjamzito na jamaa hapokei kabisa simu za huyu dada..Dada huyu kanifuata jana na kutaka nimpe hela ili aende akatoe mimba kwani anadai hawezi kuzaa mtoto mwingine asiye na baba.Imani yangu ya dini hairuhusu kutoa mimba wala mimi mwenyewe kama mwanaharakati siungi mkono suala la kutoa mimba..Nimemkatalia kabisa,najua ujirani wetu uko mashakani..Niko njia panda.

according to your story wewe ni mchango mkubwa wa hiyo zahma na nasikitika kwamba wewe kama mgombea ubunge bado uko kimnya wakati kuna vyombo husika vya sheria vinaweza kufanya hii kazi
 
Umefanya vizuri sana mama endelea kushauri asitoe kabisa!
 
Kama una uwezo jitolee kumsaidia huyo mtoto wake aliye shuleni ili kumuondolea frustration huyu dada na Mungu kwa njia zake za ajabu atakurudishia na kukuongezea pale utakapopungukiwa
 
usimpe chochote

usije ukatenda dhambi kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutimiza wajibu wa kumpa huyu mama pesa.

kuna zaid ya hilo, wakati hajampata huyo jamaa maisha yake alikuwa anayaendesha vip?
 
mwambie azae kisha na amgawe mtoto....................nafikiri kuna watu kadhaa wa kadhaa waliokuwa wanatafuta watoto hawana.
 
hii habari imekosa nguvu ya ushawishi. tena sioni kama mleta habari alihitaji kuileta jamnvini. nadhani huyo dada kama kweli alitaka kutoa mimba asingekwenda kuomba pesa ya kutolea mimba- angeweza hata kudanganya shida nyingine kwa mtoa maada, apate pesa, ili mimba itoke. pili huyu dada wakati anatafuta ada ya mtoto hakuwai kumfuata mtoa maada na kuomba pesa ya ada? au kama si ada basi hata kutaka ushauri wa nani wa kumkopa???. miaka 33, unamfuata mwanaume ambaye unasemaanakutongoza humtaki- kwanini umfuate ukiwa na shida?? ktk mazingira haya, kipi raisi kuomba ada kwa mtoa maada au kuombapesa ya kutoa mimba???.tena dada ana shughuli zake ndogondogo ktk hizo shughuli hakuna watu wengine anawajua isipokuwa huyo mwanamme?? nadhani kwanza kabisa dada asingekwenda kukopa kwa mtu ambae walitofautiana ki-msimamo. kama ni kweli basi kuna cha kujifunza kuoka kwa huyo mama.
 
Aroo GS, swala sio tu kutoa mimba ni hatari kwa afya yake, bali ni uvunjifu wa sheria ya Tanzania.
Mwambie hata asipojali afya yake kwa kuitoa hiyo mimba lakini mkono wa sheria upo pale pale, atawajibishwa.
Nipe details zake ili nihakikishe sheria ya nchi inafuatwa.
 
Usiue - Amri kuu ya mungu
Mwambie huyu mpendwa kuua ni dhambi na pia ni hatari kwa maisha ya huyo Binti.sio kwanba ndio mwisho wa maisha ya binti anaweza kujifungua na kuendelea na masomo yake
All the best
 
mwambie azae kisha na amgawe mtoto....................nafikiri kuna watu kadhaa wa kadhaa waliokuwa wanatafuta watoto hawana.

Kweli Gaijin
hata mie naweza kupewa huyo mtoto nikamtunza kama mwanangu ..GS mwambie huyo binti ajifungue anigawie mtoto..ruksa kuja kumsalimia
 
hivi watu wanafanyaje mapenzi jamani bila kufikiria mara mbili mbili? li mtu umekutana nalo tu hata kinga hamtumii?jamani matatizo mengine ni ya kujitakia kabisaaaa.
 
hii habari imekosa nguvu ya ushawishi. tena sioni kama mleta habari alihitaji kuileta jamnvini. nadhani huyo dada kama kweli alitaka kutoa mimba asingekwenda kuomba pesa ya kutolea mimba- angeweza hata kudanganya shida nyingine kwa mtoa maada, apate pesa, ili mimba itoke. pili huyu dada wakati anatafuta ada ya mtoto hakuwai kumfuata mtoa maada na kuomba pesa ya ada? au kama si ada basi hata kutaka ushauri wa nani wa kumkopa???. miaka 33, unamfuata mwanaume ambaye unasemaanakutongoza humtaki- kwanini umfuate ukiwa na shida?? ktk mazingira haya, kipi raisi kuomba ada kwa mtoa maada au kuombapesa ya kutoa mimba???.tena dada ana shughuli zake ndogondogo ktk hizo shughuli hakuna watu wengine anawajua isipokuwa huyo mwanamme?? nadhani kwanza kabisa dada asingekwenda kukopa kwa mtu ambae walitofautiana ki-msimamo. kama ni kweli basi kuna cha kujifunza kuoka kwa huyo mama.


huyu dada hakwenda kumkopa mkaka, bali alienda kufanya na wamalizane kifedha lakini mkaka akamwacha solemba, ndivyo nilivyoelewa.
 
Msaidie tu huyo dada kwa kumsomeshea mtoto wake na mshauri madhara ya kutoa mimba pia
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom