(M)ungu na sio (m)ungu"mungu mdogo" - hahitaji sheria,katiba,bunge bajeti wala ushauri wa shetani au malaika kufanya atakalo ,kwani jeshi na polisi si wanafuta amri yake?
Kwamba unataka Tanzania iwe Rwanda? Mambo ya Rwanda yanaingia hapa kweli? Hakuna shaka yoyote wewe ndiye uko brain washed! Soma historia ya Rwanda na umsome Kagame mwenyewe, kisha uje kwenye historia yetu na umsome JPM...Sema sielewi, usiseme huoni hoja. Nitajie nchi hata moja iliyoendelea kwa kukumbatia hicho unachoita demokrasia mwanzoni mwa mchakato wa maendeleo yake. Nchi zote duniani zimekuja kukumbatia demokrasia baada ya kupata maendeleo. Huwezi kuendelea huku umewaachia watu wafanye kila wanalotaka. Paul Kagame wa Rwanda alikuwa anapigiwa kelele hivyo hivyo. Leo wanamwelewa alichokuwa anafanya. Hii tendency ya kuwa brain washed kuwa vyama vinakandamizwa ni upuuzi wa Hali ya juu. Sasa wewe subiri utamwelewa rais baadae.
We malaya tunaongelea serikali !Ofisi ipi hiyo ya umma unayoisema ?by the way
Ofisi za Chadema mikoani zina karatasi?
[emoji23] [emoji23] [emoji23] Kahabaaa!!!Magufuli atafanya yaliyoko kwenye ilani na atapimwa kwa ilani ya CCM iliyopendwa na wapiga kura wengi....waliokosa muelekeo ni wale walioahidi kwenda kuchunga ng'ombe mara wakaahidi kwenda ICC na mara waahidi kuzunguka nchi na blah blah kibao.
Wakati wa Uchaguzi tuliwaonya sana muache kuwa Nyumbu na wazungusha mikono na badala yake msikilize sera na kupima kama zinatekelezeka....
Kama mngesikiliza Ilani ya CCM kama ilivyonadiwa na Magufuli usingekuja kuuliza pumba hizi unazouliza leo hii...
Magufuli aliahidi kupambana na Rushwa(Ni mgombea pekee aliyeongelea rushwa kwa hisia na kweli)....Mwezi wa Saba Mahakama ya Mafisadi inaanza kazi
Magufuli aliahidi kushughulikia Tatizo la mikopo elimu ya juu....Wanafunzi wamepata mikopo,bodi imefumuliwa na mikopo imeanza kurejeshwa.
Magufuli aliahidi elimu bure...Imeshaanza pamoja na changamoto zake.
Magufuli aliahidi kukusanya kodi na kuondoa viushuru vya ajabu ajabu...Salamu za bandari za nchi kavu umezisikia na kama unafuatilia kuna viushuru vya kwenye kahawa vimeanza kuondolewa.
Magufuli aliahidi kupunguza msongamano Dar....Mabasi ya mwendo kasi yameanza ns hapa majuzi kitwanga anaongelea kuhusu flyover kuanza kujengwa...
Magufuli aliahidi kurejesha nidhamu kwa watumishi wasio waadilifu....unataka niongee??
Magufuli aliahidi kuwanyang'anya mashamba wale wasioendeleza ....unataka kuniambia hujamsikia lukuvi??
Hivi hujasikia kiwanda cha tiles kilichoanza kujengwa Mkuranga ?hivi hujamsikia rais akiwaasa NSSF PPF kujenga viwanda badala ya maghorofa yasio na tija??
Pale Muhimbili CT SCAN ilikuwa ni kipimo adimu sana kukipata nadhani unaweza kuona nini kinaendelea Baada ya Rais kuzuru Muhimbili consistently (Changamoto ya dawa na vifaa tiba kuwepo kwenye vituo pamoja na ujenzi wa zahanati)....universal coverage ya bima ya afya ni sheria inayonukia mwezi septemba.
kuhusu maslahi ya wafanyakazi PAYE imeanza kufikia single digit as per july this year.
Kuhusu kuulinda muungano...Rais ametuvusha salama salmini bila tone la damu kumwagika kule Zanzibar pamoja na hila zenu zilizokosa uzalendo na za kuwategemea mabwana wa kizungu.
Ndio maana narudia tena kuwaita Nyumbu au pengine ni fisi mnaofuata mzoga ulipo maana hamjielewi mshike kipi.....
Matatizo yenu ya kupokea makapi na mizoga muyamalize huko huko msituletee shombo sisi wastaarabu!!!
MAGUFULI AMEFANYA ZAIDI KABLA YA MUDA WAKE KUANZA!!
Hivii makusanyo ya kodi TRA MWEZI ULEEE.. ULIOPITA... NA HUU SASA TUMEKUSANYA NGAPI VILEEE?[emoji84]Akupeleke kwani wewe umekuwa zombie? Raisi Magufuli hayuko hapa kukupeleka wewe popote pale, bali wewe ndiyo unatakiwa ujipeleke mahali kwingine, wewe ndiyo unatakiwa ujitoe hapo ulipo na kwenda sehemu nyingine, wewe ndiyo unatakiwa ujifungue minyonyoro uliyofungwa na fisadi Lowasa, Mbowe & Co. na kuwa mtu huru Raisi Magufuli hawezi kulifanya hilo na wala siyo kazi yake!
Unabii huu hatari,Mungu ni Mwema tutajua......anguko la karneNi vizuri tukajifunza katika Biblia jinsi tawala mbalimbali zenye nguvu zilivyaanguka kama nyumba ya mabua.
Tukisoma katika kitabu cha Danieli 5:1-10 Mfalme Belshaza wa Babylon alikuwa na nguvu na kiburi kingi sana katika utawala wake, wala hakutaka kushauriwa wala kukosolewa. Alijihisi yeye ndio anayejua kuliko watu wake wote, na mwenye akili nyingi kuliko raia wote. Hakutaka kushauriwa na yeyote hata wakuu wengine katika utawala wake waliiga matendo yake. Ila siku moja aliandaa karamu kuwafurahisha watumishi ndani ya utawala wake, ndipo Mungu alionyesha maajabu yake kiganja cha mkono kuandika juu ya ukuta Menemene=ufalme wako umepimwa=Peresi=umepungua au unamapungufu=Tekeli= umegawanywa nao umepewa wengine.
Utawala huu umefanania sana ufalme wa Babeli ambao Mfalme Belshaza alifikiri kuwa yeye anajua kuliko watu wote.
Utawala huu unahisi kwamba watu wengine hawafai kabisa kutoa mawazo yao maana ni ya kipuuzi.
Utawala huu unaongozwa na hisia na visasi, kuliko uhalisia. Utawala huu unafikiri kwamba watafanikiwa kuwafumba kinywa wote wanao wakosoa na kujaribu kuwashauri.
Utawala huu unapenda sifa na kujiinua. ni utawala unaotaka kuchukuwa utukufu hata wa Mungu.
Utawala huu umejaa watu wanafiki wasiokuwa na uhuru wa fikra bali wana nidhamu za woga.
kwa hali hii utaporomoka maana Mungu hawezi kuruhu watu kunyimwa uhuru wa kutoa hisia zao.
Unabii huu hatari,Mungu ni Mwema tutajua......anguko la karne