Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Nimesikitishwa sana na zaidi ya watu 2000 kupoteza ajira katika mgodi wa Bulyahkulu.

Je kuna mtu mwenye mapenzi mema na hii nchi anaweza kulishangilia hili?

Je serikali hii ni ya wanyonge kama inavyosemekana, huku ikishuhudia maelfu ya watu wanapoteza ajira bila kuchukua hatua zozote huku ikishangilia mwekezaji akifunga biashara ya matrilioni?

Kwa wanaofaham na waliobahatika kufika Bulyahkulu hasa hasa mwenye uchimbaji chini ya ardhi atakubaliana na mimi kuwa kule ni chuoni, kwani watanzania wengi waliobahatika kufanya kazi pale wamepata ujuzi na kuweza kupata kazi nje ya nchi ....

Je familia na biashara zilizokuwa zinategemea hawa wafanyakazi , ni watu watakuwa wamekosa matibabu, elimu, chakula, kipato n.k ?

Haya yote na madhara mengine ni matokeo ya ripoti ya Pro. Mruma ambayo ina takwimu ambazo watu wanaojua mining sector zinatia shaka.

Tunatakiwa kuwa makini na hizi ripoti na kujiridhisha kabla ya kuchukua maamuzi, kwa watakaothirika ni watanzania wanyonge na sio mwingine.
 
Umeambiwa upambane na hali yako na yeye amesema anachotaka kusikia ni kwamba wameondoka na sio watu kupoteza ajira.
 
Naomba ni declare interest Iam teacher by professional.Ninaposema simuelewi naaamanisha hivi.
Wakati wa Jk dagaaa za Mwanza nilinunua 1kg@kwa Tsh 3000 Sasa hv ni Tsh 12000 kwa kg.
Mafuta ya kula nilinunua Tsh 15000 kwa lita 5 sasa hv 22500.
Sukari 1kg Tsh 1800 sasa Tsh 3500.
Kodi ya nyumba kwa mwezi 15000 sasa Tsh 30000. Na mshahara ni ule ule wa Jk.Sasa nakuomba mhe Rais sikuwahi na sitawahi kuwa mpiga madili kwani shule ya msingi kuna madili mpaka niwe mpiga madili .Ninapolalamika ugumu wa maisha ugumu wa maisha upo, Ujue upo .Nasimimi tuuu jua watanzania wote wanalamika ugumu wa maisha hebu fanya reseach bila kuwatumia hao viongozi wako wanaokupa data utaona uchumi unavyoendrlea kudidimia.Naomba msiniteke na kuniua pia naomba nisiitwe mchochezi, Sina sehemu nyingine ya kulalamikia isipokuwa kwennye forum kama hz. Nawashawashwa
 
Alishasema yale maneno matamu aliyozungumza yalikuwa ya kufanyia kampeni na wakati wa kampeni umepita...usiite maisha ni magumu endelea tu kufanya kazi kama maisha yakiwa magumu sana achana nayo ufanye mambo mengine!
 
Kuna msemo anasema hajapunguza wala kuongeza mshahara, anae lalamika ni mpiga dili ..

Mkataba wa board ulikuw 8% Leo hii ni 15% makato ...

Sielewi inaposemwa mshahara haujapunguzwa
 
Mkuu nyie si ndo huwa mkipewa kofia na vitenge kwenye kampeni, afu mnasimamia 'uchafuzi' wenyewe, mnatwambia tutaisoma ya kirumi, leo mnalalamika tena. Au umekua mstaafu
 
Hakuna wa kukuteka hapo umeongea kiuungwana sana Mfumo wa uchumi wake ni wa kukomoana ameweka pia mifumo mizuri ya kukusanya kodi ila Hailpi Madeni ya ndani hiyo Mifumo Hailipi kodi Anaye lipa kodi ni mimi na wewe ''No welfare for his people'
 
Napenda naposikia walimu muna hali mbaya , mana nyinyi huwa wepesi wa kusahau ,shida zote mnazopitia ikifika kipindi cha uchaguzi mnakuwa vipofu .
Na bado
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…