"Anayekula nyama ya mtu haachi " Hapa Mwl Nyerere alimaanisha nini ?

"Anayekula nyama ya mtu haachi " Hapa Mwl Nyerere alimaanisha nini ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Hili bila shaka lilikuwa fumbo kubwa sana , maana katika hali ya kawaida hakuna binadamu anayekula nyama za watu , na kwamba akinogewa ataendelea kuwatafuna tu binadamu wenzake hili si la kulichukulia poa , sasa katika hili Baba wa Taifa alilenga kutuma ujumbe gani kwa jamii ?
 
Mkuu hili ni fumbo pana sana na linachukua nyanja zote kwa muqtada huo, na ukizingatia mambo yanavyoenda kwa sasa basi ujumbe huo uko mahala pake!
 
Hili bila shaka lilikuwa fumbo kubwa sana , maana katika hali ya kawaida hakuna binadamu anayekula nyama za watu , na kwamba akinogewa ataendelea kuwatafuna tu binadamu wenzake hili si la kulichukulia poa , sasa katika hili Baba wa Taifa alilenga kutuma ujumbe gani kwa jamii ?


Yeye alijuaje kama mtu akila nyama ya mtu hawezi kuacha kula??!!, inatupasa tuanze kumuhoji yeye kwanza kabla ya kuingia kujadili alikuwa na maana gani!!.🤣
 
Yeye alijuaje kama mtu akila nyama ya mtu hawezi kuacha kula??!!, inatupasa tuanze kumuhoji yeye kwanza kabla ya kuingia kujadili alikuwa na maana gani!!.🤣
unayo hoja mkuu
 
Hili bila shaka lilikuwa fumbo kubwa sana , maana katika hali ya kawaida hakuna binadamu anayekula nyama za watu , na kwamba akinogewa ataendelea kuwatafuna tu binadamu wenzake hili si la kulichukulia poa , sasa katika hili Baba wa Taifa alilenga kutuma ujumbe gani kwa jamii ?
Maanake ni kwa zimwi likujualo halikuli likakumaliza mzee baba, kifupi mwalimu alijaribu kupotrait picha ya kwamba ukimuona mtu fulani anamuonea mwingine nawe usimkemee na kusema hayo hayakuhusu basi siku uyo muoneaji akikosa wa kumuonea atakuijia wewe maana ndo utakayekuwa umebaki ivyo kwa umoja wetu tunatakiwa kuupinga uonevu wa aina yoyote na kwa nguvu zote!
 
Back
Top Bottom