Uchaguzi 2020 Anayewatukana mabeberu 'wazungu' ajitafakari upya

Uchaguzi 2020 Anayewatukana mabeberu 'wazungu' ajitafakari upya

Trust None

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2018
Posts
1,260
Reaction score
4,419
Sijui ni upofu au ni chuki binafsi na wapinzani. CCM wanatukana 'mabeberu' bila kukumbuka kuwa bila hawa 'mabeberu' hata huo uchumi wa kati tusingefika.

Ni kweli 'mabeberu' wana mabaya mengi walitufanyia na sasa yapo kupitia 'ukoloni mamboleo' lakini CCM hawahawa wamekuwa wakishirikiana na hawa 'mabeberu' katika nyanja nyingi.

Mabeberu hawa hawa ndio hufadhili ARVs, kondomu, dawa za malaria na dawa zingine za magonjwa hatari. Bila wao sijui wangapi wenye watatizo hayo wangekuwa hai.

-'Mabeberu' ndio wanaotoa misaada na mikopo kwa serikali ya CCM

- Mabeberu ndio huleta pesa za kigeni kupitia utalii.

- Mabeberu hawa ndio huchangia bajeti kuu ya serikali.

- Mabeberu hawa ndio wanamiliki na kuendesha migodi Tanzania.

- Mabeberu hawa ndio hufadhili elimu na ikitokea ZITTO akahoji mambo fulanifulani, CCM hawahawa wanawaka.

NB. Yapo mengi yanayofanywa na 'mabeberu' kwa manufaa ya Tanzania, hivyo CCM mje na hoja nyingine.

Kiufupi Tanzania bila 'mabeberu' ingekuwa nyuma sana kimaendeleo kwahiyo wapinzani kuwakumbatia 'mabeberu' wanaendeleza kile kinachofanywa na CCM
 
Inategemea anongea na akina nani. Mwongeaji akijua kwamba anaongea na wenye akili basi anatumia jina "wafadhili" au "wahisani".

Ila akiona anaongea na riff raff, basi anatumia neno "mabeberu". Mfano wote wale wa buku saba ni riff raff
 
Chini ya CCM hii na wafia chama wake neno beberu limepoteza maana. Kuna jamaa waliitwa mabeberu walipo tinga bongo mazungumzo yalipokwisha hao hao wakaitwa WANAUME.
 
Sijui ni upofu au ni chuki binafsi na wapinzani... CCM wanatukana 'mabeberu' bila kukumbuka kuwa bila hawa 'mabeberu' hata huo uchumi wa kati tusingefika...
Shida huelewi maana ya neno ubeberu unafikiri ni tusi. Ubeberu ni ubepari uliyovuka mipaka ya nchi yake. Pale unapokua na nchi kama uingereza au marekani na ufaransa ambayo uchumi wake unaendeshwa kwa mfumo ya makampuni makubwa hadi yamewekeza kote duniani.

Serikali za nchi hizo zinasaidia kulinda maslahi ya makampuni hayo kote yalipowekeza. Wakati mwingi serikali za nchi hizo hutumia njia za mabavu nguvu na hila za kila aina ili kuendeleza maslahi ya wawekezaji wao. Hapo ndio unakuta nchi hizo ndio haohao waliyokua wakoloni ndio haohao wahisani ndio hao hao wawekezaji ndio haohao mabeberu.
 
Shida huelewi maana ya neno ubeberu unafikiri ni tusi. Ubeberu ni ubepari uliyovuka mipaka ya nchi yake. Pale unapokua na nchi kama uingereza au marekani na ufaransa ambayo uchumi wake unaendeshwa kwa mfumo ya makampuni makubwa hadi yamewekeza kote duniani. Serikali za nchi hizo zinasaidia kulinda maslahi ya makampuni hayo kote yalipowekeza. Wakati mwingi serikali za nchi hizo hutumia njia za mabavu nguvu na hila za kila aina ili kuendeleza maslahi ya wawekezaji wao. Hapo ndio unakuta nchi hizo ndio haohao waliyokua wakoloni ndio haohao wahisani ndio hao hao wawekezaji ndio haohao mabeberu.
Sasa tuchague nini kwa maelezo yako haya.Mabeberu ni watu wazuri hapo hapo wabaya.Je,tujitenge nao ama tuishi nao??
 
Shida huelewi maana ya neno ubeberu unafikiri ni tusi. Ubeberu ni ubepari uliyovuka mipaka ya nchi yake. Pale unapokua na nchi kama uingereza au marekani na ufaransa ambayo uchumi wake unaendeshwa kwa mfumo ya makampuni makubwa hadi yamewekeza kote duniani. Serikali za nchi hizo zinasaidia kulinda maslahi ya makampuni hayo kote yalipowekeza. Wakati mwingi serikali za nchi hizo hutumia njia za mabavu nguvu na hila za kila aina ili kuendeleza maslahi ya wawekezaji wao. Hapo ndio unakuta nchi hizo ndio haohao waliyokua wakoloni ndio haohao wahisani ndio hao hao wawekezaji ndio haohao mabeberu.
Hayo watu walijua wakati tunafundishwa siasa shuleni. Kujaribu kufundisha tafsiri hizo kwa hiki kizazi cha wavaa katakei unatwanga maji tu.
 
Hayo watu walijua wakati tunafundishwa siasa shuleni. Kujaribu kufundisha tafsiri hizo kwa hiki kizazi cha wavaa katakei unatwanga maji tu.
😂😂Tujitahidi tusikate tamaa..
 
Ni ajabu sana unatukana beberu wakati hapo uliposimamia wakati unatukana upo kwenye kiganja cha beberu je beberu likiamua kukifumba kiganja chake wewe mtukanaji siutafinyangwa mpaka na kinyesi juu
 
Ni ajabu sana unatukana beberu wakati hapo uliposimamia wakati unatukana upo kwenye kiganja cha beberu je beberu likiamua kukifumba kiganja chake wewe mtukanaji siutafinyangwa mpaka na kinyesi juu
Beberu sio tusi beberu ni sifa
 
Watu hawana shida na tafsiri ya neno mabeberu watu wanahoji wahusika wanaoitwa mabeberu kwanamna yakukebehi uwepo wao ili hali bado tunashirikiana nao kwa mambo kadha wa kadha.
Shida huelewi maana ya neno ubeberu unafikiri ni tusi. Ubeberu ni ubepari uliyovuka mipaka ya nchi yake. Pale unapokua na nchi kama uingereza au marekani na ufaransa ambayo uchumi wake unaendeshwa kwa mfumo ya makampuni makubwa hadi yamewekeza kote duniani. Serikali za nchi hizo zinasaidia kulinda maslahi ya makampuni hayo kote yalipowekeza. Wakati mwingi serikali za nchi hizo hutumia njia za mabavu nguvu na hila za kila aina ili kuendeleza maslahi ya wawekezaji wao. Hapo ndio unakuta nchi hizo ndio haohao waliyokua wakoloni ndio haohao wahisani ndio hao hao wawekezaji ndio haohao mabeberu.
 
Shida huelewi maana ya neno ubeberu unafikiri ni tusi. Ubeberu ni ubepari uliyovuka mipaka ya nchi yake. Pale unapokua na nchi kama uingereza au marekani na ufaransa ambayo uchumi wake unaendeshwa kwa mfumo ya makampuni makubwa hadi yamewekeza kote duniani...
Sisi si kisiwa Ni kuwatumia positive kaa na waridi unukie uwaridi. Hakuna nchi iliyowahi shirikiana na mabeberu ikawa fukara.
 
Watu hawana shida na tafsiri ya neno mabeberu watu wanahoji wahusika wanaoitwa mabeberu kwanamna yakukebehi uwepo wao ili hali bado tunashirikiana nao kwa mambo kadha wa kadha.
Ni chuki za waliosoma mitaala ya zamani mashuleni zilifundisha jinsi ya kuwachukia wakoloni weupe ili kuwapumbaza watu wasahau kuhusu ukoloni weusi
 
CCM wakiwa na njaa wanawaita wazungu wafadhili. CCM wakishashiba na wakajikuta wako kwenye "heat" wazungu wanabadilishiwa jina na kuitwa mabeberu!
 
Back
Top Bottom