Elections 2010 Anayotaka Dr Slaa haya hapa!

MAISHA BAADA YA UCHAGUZI........
Kama wote twalijua hili kwa nini sisiem wanalazimisha matokeo? we don't need rocket science kujua ccm wameiba kura, everyone knows, sisi tunajua na wao wanajua
 
I'm sick and tired of the name Kikwete, especially when he is tampering with grand gift God have given us, namely peace!
 
Jamani Jamani......Nadhani Watu wa usalama wa taifa wameingia kwenye JF. Baadhi ya page hazifunguki kwa sasa na nyingi zimekuwa private...Inauma...sambaza ujumbe
 

Hata kama mechi hairudiwi lakini walau isemwe kuwa goli lilifungwa kwa mkono na siyo kwa mguu wakati kila mtu na linesmen waliona goli lifingwa kwa mkono. Tukiambiwa hilo tuhoji je sheria za mpira zinasema nini kuhusu ufungaji wa goli. Binafsi uchakachuaji huu unatunyemelea kuanzia kwenye mitihani ya shule, vyeti, kwenye huduma zingine na sasa kwenye kura na baada ya hapo utahamia sehemu nyingine. Njia nzuri ya kupambana nao siyo kuufumbia macho bali kuupiga vita kwani utaweza kutufarakanisha.

Ni kama mtu uchumbie fiancee A na siku ya harusi ukute fiancee B halafu uambiwe 'kubali yaishe' hilo ndilo lilikuwa chaguo lako. Inaingia akilini? Kwa namna nyingine ni kwamba: suppose umeoa na ikatokea mke wako ni mjamzito na taarifa za clinic zioneshe kajifungua mtoto wa kiume hospitali na ndugu au jirani waone kweli ni mtoto wa kiume. Halafu baadaye nesi alete mtoto mwingine, ambaye ni wa kike kutoka sehemu watoto wadogo wanapohifadhiwa. Je, yupi ni mtoto wako halali: yule aliyezaliwa na kuonekana ni wa kiume au huyu wa pili wa kike? Hivyo nidvyo ilivyotokea kwenye uchakachuaji.
 
Kwa mimi naona jambo la msingi ni sisi wananchi na wabunge tupiganie katiba iliyopo ibadilishwe kwani hadi sasa inaegememea chama kimoja.tukiamua inawezekana na tume ya uchaguzi itakuwa ya huru na haki kwan iliyopo imeteuliwa na mafisadi kwa maslahi yao haina nia ya kumkomboa mlalahoi kama mimi.
 

Hata kule Bukombe nasikia wakati akiwa kwenye kampeni, watu walionekana kutomuunga mkono na kumwonyesha dhahiri kuwa walikuwa upande wa Dr. Slaa ndipo akawaambaia maneno "mpigieni kura mnayemtaka lakini CCM itashinda kwa kishindo". Maneno haya yana maana kuwa lazima washinde na namna ya kushinda alikuwa anaifahamu.
 

Ndugu yangu unayoongea yamenitia uchungu sana. Ni mawazo mazuri sana. Unajua watanzania tuna ushabiki wa kijinga sana na tunapenda kuchukulia mambo juu juu tu bila kuyatafakari kwa kina kinacholalamikiwa na watu walioonewa. Kwa utamaduni huu, ccm itaendelea kuitawala nchi hii kwa ubavu bila kujali kama wananchi wanaipenda au la. Nchi hii ina watu wengi walioelimika lakini ni waoga wa kudai haki na mabadiliko ili kuondoa uwizi na ukilitimba unaofanywa na ccm. Mimi binafsi ninampongeza sana Dr. Slaa na kwa kweli Mungu ambariki sana. Ushauri wangu kwa Dr. Slaa ni kwamba pamoja na hatua anayochukua ya kudai haki, asikate tamaa kueneza elimu ya uraia kwa wananchi. Wabunge wa chadema walioongezeka si haba na kwa kweli ni mafanikio makubwa sana yaliyotokana na juhudi kubwa iliyofanywa na chama cha chadema. Mimi nina hakika tena sana kwamba kasi hii ya kuongeza wabunge ndiyo itakayotuwezesha kuibadili tume ya uchaguzi kuwa huru na hivyo kuondoa uwezekano wa ccm kuiba kura.

Ninawatakia afya njema viongozi wote wa chadema na mwenyezi Mungu aendelee kuwawezesha ili hatimaye nchi hii ifikie ukombozi kamili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…