Angalia jela hiyo ughaibuni

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Inaitwa Justice Center Leoben, iko Austria ni jengo ambalo lina mahakama pamoja na jela. Aliyeli -design architect anaitwa Josef Hohenssin likakamilika 2005.

Lina uwezo wa kuweka wafungwa 205 na limejaa wafungwa 205 lengo la kujengwa gereza zuri hivyo ni kusimamia Kwa vitendo na kuonyesha kwamba kila binadamu ana Haki Sawa, amezaliwa huru na anapaswa atendewe Kwa heshima.

 
Ha ha.

Jela ni Jela tu.

Fuvu likipigwa Jela ni Jela.

Ukifungwa Ulaya au Ukifungwa Afrika, ni Jela.

Kiufupi Ukiwa mhalifu wewe ni Mhalifu, haijalishi ukiwa ni Mzungu au Mwafrika.

Itoshe unapofungwa jela, ni kwamba haki zako zingine za msingi, zinagota hapo Jela.
 
Huku kwetu watu wanaachiwa wanaenda kubaka au kuiba tena ili warudi kula ugali wa bure ukizijenga hizo gereza si itakuwa balaa.
Miaka ya nyuma kidogo niliishi kwa shem yangu. Yani alikuwa akiweka soda chupa chache kwenye Friji tunazifakamia zote halafu anatumaind balaa lakini dada yetu alikuwa anatukingia kifua. Dada akaamua kusolve hili tatizo akaamua kila siku kununua kreti tano za soda nakuziweka kwenye Friji nakutuachia tunywe tunavyopenda. Baada ya siku moja tukakinai soda wala hatukutaka kuziona zilikuwa zinabakia kwenye Friji hadi zinaexpire.
 
Hii scenario kwa nchi yetu haiwezekani. Kwamba serikali ifanye raia wazoee maisha mazuri kwa kiwango cha kuona kulala gereza lenye tv, choo cha kuflash na AC ni kawaida?
 
Ma rais wa nchi za Afrika wanatakiwa kuwekwa hapo.
 
Hii itapromote uhalifu
 
Hiyo Net ni Anti Drone kwasababu Drones zilikuwa zikitumika sana kuingiza Drugs kwenye Jela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…