Angalizo: Sio Watanzania tu, hata Waingereza wameikataa DP World

Misozwe

Member
Joined
Dec 23, 2022
Posts
21
Reaction score
26
  • Ilifukuza kazi wafanyakazi 800 bandarini Uingereza kwa mkupuo bila kufuata taratibu
  • Iliajiri vibarua toka nje ya Uingereza na kuwalipa ujira mdogo kinyume na sheria
  • Manamba na vibarua wa Tanzania wajiandae kulipwa kiduchu
  • Hisia: Waingereza wanasema rushwa imeibeba DP World


Uamuzi wa kuruhusu mmiliki wa P&O Ferries kushiriki katika mradi mkubwa mpya wa miundombinu umesababisha hasira, baada ya kampuni hiyo kuwatimua kazi wafanyakazi 800 bila taarifa mwaka jana.

DP World imeidhinishwa kusimamia pamoja na bandari huru ya Thames huko Essex, kama sehemu ya mpango wa bandari huru wa Rishi Sunak.

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi lilisema ilikuwa ni "uamuzi mbaya", ambao unawezesha waajiri wengine "kutenda bila kujali". P&O Ferries iliwaachisha kazi mamia ya wafanyakazi wa baharini mwezi Machi 2022 na kuwabadilisha na vibarua wa kigeni waliolipwa chini ya mshahara wa chini kinyume cha sheia. Hatua hiyo ilisababisha hasira na kusababisha miito ya kujiuzulu kwa mkurugenzi mtendaji wa P&O, Peter Hebblethwaite.

Wiki moja baadaye, Bwana Hebblethwaite alikiri mbele ya wabunge kuwa uamuzi huo ulikiuka sheria za ajira. Wakati huo, serikali iliita matendo yaliyowakumba wafanyakazi kuwa "hayakubaliki kabisa". Grant Shapps, ambaye wakati huo alikuwa waziri wa usafiri, alisema sheria itabadilishwa ili kuzuia kampuni kuwaachisha kazi wafanyakazi kwa papo hapo.

Ni angalizo tu.
 
Hii Habari sio sahihi
Vibarua ni kutoka kwa agencies za kuajiri wafanyakazi ambao ni wa hapa hapa uk na sio kutoka nje
Hapo umepotosha

P&O waliuziwa na wakaamua kuwafukuza wafanyakazi hao kwa kuanza na watu wengine

Hayo ni makubaliano kuwa nimenunua kampuni nataka wafanyakazi wapya niwalipe kwa uwezo wangu

Kumbuka kuna upinzani na P&O ilikuwa ina miaka 180 ilipouzwa
 
Wamekataliwa ?au wamelalamikiwa?
Kukataliwa ni kufukuzwa na kunyimwa kufanya kazi husika ...
Sasa kama serikali imewapa vibali husika ... malalamiko ya wafanyakazi ndo unaita "kukataliwa"???

Huku wanaendelea na kazi kama kawaida??.....

Rekebisha kichwa chako cha habari ..
Outrage sio na kuwa terminated au revoked....
Outrage za wafanyakazi ni malalamiko
 
Wanaokoteza anything na kukiremba Kwa uongo
 
Kama wamefanya hayo United Kingdom itakuwaje hapa Buguruni Mapipa?!
 
Yaani km mwarabu anafanya huu ugaidi kwa wazungu itakuwaje kwa TANGANYIKA yetu

Watanganyika wakataeni Hawa watu wataisambaratisha TANGANYIKA
 
Yani mnatak kuungana na miingereza mnaona wenzenu hao? Hata wao ni waamba ngoma pia sio wa kuchekea.

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
 

Wameikataa wapi? Unajua lugha ya kizungu vizuri wewe?

Kulalamikiwa na kukataliwa ni sawa? Au hujui hata kiswahili pia
 
mkuu wewe ni mzanzibar?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…