Angelina Jolie aanza kusumbuliwa na Mama wa mtoto aliyemuasili

Mkuu kwa wabongo tunafanya au tuliwahi fanya hiyo mambo lakini kwakweli wabongo ni tatizo.
Mimi niliwahi kuasili watoto 3 wawili walikuwa ndugu na mmoja ni wa familia nyingine
Tatizo lilikuja pale wale wawili walipo fika chuo kikuu wana boom akijitokeza mtu kuwa ni mzazi wao na mambo kibaaao!
Nilipata usumbufu wa kila aina ikabidi niache watoto waamue kwasababu tayari ni wakubwa.

Akabaki 1 ambae sasa yupo kidato 4 huyu nae mlezi wake akaanza longolongo kwakuwa sipendi vyesi nikamburuza Ustawi wa jamii kwasababu sikumchukua mtoto kienyeji. Akasalim amri amuache mtoto asome Mtoto ataamua pa kwenda akifikisha miaka 18.

Kuasili watoto wa watu wasiojielewa ni mtihani.
Ukitaka kuasili nenda kaasili kutoka vituo vya watoto yatima tofauti na hapo fanya shughuli nyingine za kusaidia wasiojiweza. Lakini usiali mtoto mwenye wazazi hatakama hajiwezi kupindukia.
 

Upo sahihi hapo pa "usiasili mtoto mwenye wazazi" kama maisha yao ni magumu sana msaidie akiwa hapo hapo kwa wazazi wake,

Pia huko kwenye vituo wengi wanalalamika masharti yao ni magumu sana inafanya watu wanashindwa kuasili watoto.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]Nimechekaa sana Cuzo, hii Dunia au tuimarinate na tangawizi Nini mbona ngumu hivi???
Sasa baba kama yule kuendekeza njaa Hadi kujitoa akili maana yake Nini?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sielewi tunakoelekea Cuzo.....Siyo salama kabisa.
 
Hii pic ya kwanza ka Zahara ndio kana miezi 7, na sasa ana miaka 18,

Hongera kwa Angelina amemlea vizuri sana huyu mtoto, ana adabu, upendo na utu,

Anaingia rasmi kwenye kiwanda cha fashion.
Kumlea vizuri au kumlisha vizuri
Usije kushangaa ukisikia ana mpenzi ambaye ni mwanamke mwenzie
Wazungu ni wa ovyo sometimes.
 
Hiyo haipo.........aende kule alikokimbilia si ndio alipaona bora
 
Wanamchanganya mtoto tu, na Angelina naye hawajamfanyia haki.

This is very selfish.

Ukishakubali kumtupa mtoto wako, umeshakubali, usitake tamaa za kuona mtoto kakua ukataka kuongea naye.

Very selfish mother.
Huyo mwanamke mpuuzi sana. Kama kweli angekua anampenda mtoto wake kama anavyosema si angekaa kimya kuliko kumsumbua kiakili na kumchanganya kwa sasa.
 
Maza ni mpuuzi sana, alimtelekeza dogo afe njaa.
 
Dah!... umasikini ulaaniwe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…