Ansbert Ngurumo: Swala na Tembo waanze kushituka na kukimbia

Kwa system iliyopo Tanzania ni ngumu Chama cha Upinzani kupewa Nchi, kuna muunganiko wa moja kwa moja kati ya CCM na Serikali.
Hakuna kisicho na mwisho..

Kama Roman Empire na utawala wa Farao wa Misri ya kale vilianguka na kutoweka, CCM ni kitu gani bwana?

Yaani Mimi nacheka tu Kwa sababu ni wazi kuwa mwisho wao umefika..!!

Very soon, CCM na serikali yake unazosema zimeungana, hakika zitaanguka kwa kishindo kikuu na watu wengi hawataamini macho na masikio yao!!

Hii desperation ya CCM na serikali itoshe kumpa kila mtu kuona kuwa hii ndio ishara ya anguko lao..
Kuna utatu mkubwa kati ya Chama na Serikali kuanzia DED, DSO, DC, Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri, Polisi n.k, Hawa kwa sehemu kubwa ndiyo wapanga mipango ya nani awe Diwani, Mbunge ama Rais wa Nchi.
Utawala huu wa uovu hautaondoka Kwa mfumo wa uchaguzi. Haya ya utatu yasikusumbue ndugu Grahams.

Kwa hatua hii ya CCM kutumia damu za watu kuua, kutesa na kubambikia kesi ili wa - withhold power na madaraka yao, basi sasa kuondoka kwao si kwa sanduku la kura tena because, that can't work..

Hawa wataondoka tu kwa intervention toka kwa mamlaka iliyo kuu kuzidi mamlaka yao inayowapa nguvu ya kutawala. Mamlaka hii kuu ni ile itokayo juu mbinguni, yaani Mungu Baba ktk Kristo Yesu pekee..

Ndugu Grahams, intervention hii tayari iko kazini. Kwa watawala wetu hawa, watu wa Mungu kama Mch Mbarikiwa Mwakipesile wa Mbeya anapofanya maombi ili CCM na utawala wake vitoweke kwao wanamuona kama ni mtu fulani mjinga na mpumbavu fulani hivi aliyechanganyikiwa..

Lakini, believe me, that is the most powerful and efficient means to overthrow any powerfu evil regime..

Utawala wa Farao wa Misri haukuangushwa na watu wenye physical weapons bali na wale waliokuwa na silaha zisizoonekana kwa macho zinaitwa spiritual weapons..
 
Mkuu ni ombi la kila mtu ila kwa jinsi utatu huo unavyofanya kazi sioni kama jambo hilo litatokea leo ama kesho, labda kama itapitishwa Katiba Mpya ambayo kimsingi Viongozi waliopo hawaitaki.

We hujiulizi kwanini kwenye Taaluma nyingine kupanda vyeo, inategemea Elimu, Umri wako kazini n,k lakini kwakutumia madaraka yake Mhe. Rais ndiyo anateua Wakuu wote wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama?

Njoo kwa Wasimamizi wa Uchaguzi, wote ni Wateule wa Rais

Kiongozi hili jambo ni gumu sana kama ngamia kupenya kwenye tundu la Sindano
 
Mkuu ni ombi la kila mtu ila kwa jinsi utatu huo unavyofanya kazi sioni kama jambo hilo litatokea leo ama kesho,
Ni kawaida ya binadamu wasio na imani inayoona kutoamini mpaka waone. Nawe u mmoja wao bila shaka.

Nakuhakikishia kuwa utaona hili likitokea si muda mrefu. Mr Grahams, Mungu anataka kujitukuza ktk Tanzania. Ni wakati wake sasa kumwonesha kila Mtanzania kuwa yeye ndiye mwenye Tanzania na watu wake..
labda kama itapitishwa Katiba Mpya ambayo kimsingi Viongozi waliopo hawaitaki.
Mungu hatumii silaha hii. Njia zake kamwe sio kama zetu wanadamu. Je, kuna jambo ngumu lolote la kumshinda bwana Mungu muumba wa mbingu na nchi??
We hujiulizi kwanini kwenye Taaluma nyingine kupanda vyeo, inategemea Elimu, Umri wako kazini n,k lakini kwakutumia madaraka yake Mhe. Rais ndiyo anateua Wakuu wote wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama?
Wewe ndiye unayefikiri kwa masafa haya. Mimi siko huko. Mimi naamini hili. Njia za Mungu ni zaidi ya njia zetu. Aweza kutenda mambo makuu ambayo jicho halijawahi kuyaona wala sikio halijawahi kuyasikia. USIOGOPE ndugu Grahams
Kiongozi hili jambo ni gumu sana kama ngamia kupenya kwenye tundu la Sindano
Wewe ndivyo unavyoona na kuamini, siyo? Nikutoe hofu tena kwa kukuambia, USIOGOPE, Mungu anadhibiti kila kitu Kwa sasa..!

Kwa Mungu hakuna jambo gumu la kumshinda. Ni kuamini na kuchukua hatua tu zilizo ndani ya uwezo wetu. Yaliyo nje ya uwezo wetu, Mungu anasema mimi (yaani yeye) atafanya!!
 
Kuna waandishi wa habari hata kama hukubaliani nao, ila unawaheshimu na kuwasikiliza!
 
Sawa
Sawa mkufunzi
 
Ntarudi soon pakinoga
 
Mkuu sikupingi ila na tofautia nawe kuhusu uwezo wa Mungu kwa Watanzania, seems haoni anatutesa kutuletea Viongozi wasiojalia maslahi ya Raia wake isipokuwa yao binafsi.

Na huwa nakeleka kuambiwa eti tuwaombee, like seriously 🙌
 
Sawa keyboard worries,
 
Machafuko ama mapinduzi ya kijeshi ndio yatavunja huu mfumo CCM.
 
Ndivyo ilivyo🪑
 
Bro msiogope, wawashike wapinzani wote ndio mambo yanoge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…