Antonio Nugaz hafai hata kuwa msemaji wa timu ya rede

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Your browser is not able to display this video.


Ni sahihi kwamba msemaji wa club ya Yanga bwana Antonio Nugaz hana hadhi ya kujadiliwa humu JF. Ila pale inapobidi ni lazima kufanya hivyo.

Binafsi nimekuwa nikimpuuza na kauli zake za hovyo na kudhalilisha club yake. Lakini hii ya kuita Mapinduzi Cup kwamba ni mashindano madogomadogo,siwezi kulipuuza.

Kauli hii imedhalilisha na kutusi mapinduzi tukufu ya Zanzibar na kutusi wazanzibar kwa ujumla.

Yanga wametoa tamko kujibaraguza kuonyesha kuheshimu Mapinduzi Cup,lakini wamefanya hivyo kwa kuchelewa. Kwani tayari msemaji wao ameshalikorogo.

Naamini waandaaji wa mapinduzi Cup watamtolea tamko huyu msemaji maandazi na timu yake,na kumtaka kufuta kauli hiyo.
 
Walioandaa wanajisikiaje?
Ila hiyo haiondoi ukweli kuwa hayo ni mashindano madogo.
 
Kwenye mchezo wa mpira usipende kuchukulia maneno seriously mzee hasa ya hawa wasemaji... Ile sio officially statement ni maneno yake binafsi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hugo mpuuzi...sio msemaji wa Yanga....sema hajui majukumu yake ya uhamasishaji anatakiwa afanye nini na aache nini!?!?

Hapa Yanga inabidi walitue hilo zigo...linafikiria kuropoka tu kama msemaji wa Simba

Uhamasishaji na usemaji wa Timu ni vitu viwili tofauti...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mashindano ya Mapinduzi Cup ni madogo sana, Yanga wasingeshiriki kabisa, mshindi zawadi milioni 15, hata usafiri tu wa kuwafikisha zanzibar ni mara mbili ya zawadi, ilifaa timu ndogo ndogo za zanzibar ndio zishiriki
 

Ukweli ni kuwa hayo ni mashindano madogo kabisa, hili halina ubishi...ila pengine kwa kuduimisha Muungano mambo mengine ni kunyamaza tu...Aidha ni afadhali huyo Nugaz mara mia kuliko yule msemaji wa timu au klabu fulani ambaye ana kauli za kuudhi na udhalilishaji wa kiwango ccha juu na ambaye baadala ya kuzungumzia masuala ya klabu yake yeye siku zote ni kuzisema timu nyingine na kujitapa kuwa yeye ni maarufu ..hovyo kabisa yule jamaa.
 
Lakini ukiwaza upande wa pili kuna ukweli miaka ya nyuma tulisema ahhaa hewala mpira ni burudani tu bwana lakini sasa dunia imebadilika mpira ni biashara swali kwa wadau wa kabumbu haya mashindano lengo lake ni lipi?Huku bara kuna ligi ya vodacom imesimamishwa kupisha hayo mashindano ,je kulikuwa na umuhimu wa kusimamisha ligi huku baadhi ya vilabu vikienda Zanzibar wengine wakisubiri?Pia naomba mwenye kanuni za uendeshaji wa ligi hasa zile za FIFA maana naona huku Tanzania akifa karumanzila ligi inasimama sasa nilitaka upana wa haya masuala ya ligi,Asanteni
 

Attachments

  • IMG_20191212_210658.jpg
    76.3 KB · Views: 1
Kiongozi, tuwe wakweli. Mapinduzi Cup ni bonanza.
Ukweli Yanga na Simba hawataki kushiriki lakini inabidi kwa sababu za kisiasa.
Afadhali zamani yalikuwa na mpangilio mzuri zaidi.
Ratiba ni suala kubwa. Michuano inazalisha viporo au kuwachosa wachezaji bila sababu za msingi.
Angalia hakuna tena timu za nje ya Tanzania.
Wanakazimisha timu zipeleke first eleven. Wangukubali viende vikosi B
 
Mashindano madogo kweli kwani bingwa anajulikana na CAF
 
Huyo ndio Juma Khatib alias Anthony Nugaz alias tena mzee clean sheet.

Yupo pale sio kwa ajili ya yanga bali GSM maana inasemakana hata hicho cheo cha awali( Uhamasishaji) hakipo kwa mujibu wa katiba wa YANGA.

Ndio maana akajiongeza kimjini kimjini na kujiongeza cheo cha msemaji wa yanga kwa maana iyo anaingilia majukumu ya Hassan Bambuli,mjini njaa kali sana mwacheni tu.
 
Msumali huu
 
KWELI NI MASHINDANO MADOGO, LAKINI KWANI HAO YANGA WANA KOMBE GANI WALILO NALO MKONONI KWA SASA WATALIITA NI KUBWA KULIKO MAPINDUZI CUP? NATAKA SITAKI.
 
Yaani kila manara atachosema mbumbumbu una C& P bila hata kujifikirisha km uhalisia ukoje.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba ina msemaji gani kama si mropokaji tu sema yeye kapata kiboko yake Antonio
 
Vichwa vya habari vya magazeti ya leo
1.Bila hirizi Simba haitambi
2.Mbeleko yagoma Leo
3.Simba wapo porini hawa waliopo Mjini ni mapaka ya bar
4.Pingili ya muwa yazama mkiani kwa simba
5.Rununu zinasumbua Hata ukiandika neno Simba inakuja Simbilis
6."Bora refa angekuwa mmama tena " asema Manara
7.Simba Kama housegirl yaani kimoja tu MIMBA
8.Simba ni zaidi ya maharage ya Mbeya hata ukilibana kwenye kwapa linaiva
9."Bora pesa yangu Hata ningewekeza kwenye Upatu" bilionea asema hayo
10.Bosi wa simba abwaga manyanga ni baada ya Timu yake kulewa muwa.
11. Mapinduzi aendelea kuipindua simba kama balama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…