ANUNNAKI: Nadharia za Mungu, miungu, fumbo la sciencenscience na Teknolojia kubwa katika Dunia ya kale, kuanguka Kwa civilization na kuinuka Tena

Hii sio poa kabisa, ruhusu kila mtu amwage madini bhana....acha jukwaa libaki huru.
nimetoa msisitizo hapo chini kama jambo hawalijui wasilete ujuaji wakae watulie wachambuzi walete ushahidi sio mihemko,.
Hilo onyo linahusu kundi Fulani kama Kuna mjadala huru hua wanakuja hisia zaidi kuliko fact hivyo nilitoa tahadhari!
Nisinukuliwe vibaya!
 
ubinafsishaji Kivipi wakati Kila Religion believer wanajua Jina la Miungu Yao?
Ndiyo, kila religion wanampa jina Mungu na kumfanya kama wa kwao ndiyo huyo mkuu kuliko wote. Lakini Mungu ni mmoja na religion zote wanamtumikia huyo. Utaona kuwa tukimuacha tu katika cheo chake kuwa ni mungu hatutapingana sana ila tukimpa majina binafsi ndo tabu inaanza. Inafikia wakati kabila au nchi tu inajiamulia kwamba Mungu ni wa kwao, ni wa babu zao jambo ambalo sio jema. Yaani awaumbe wote halafu nyie tu mmmiliki binafsi.?
 
unaweza ukanipa uthibitisho Juu ya Uwepo wa huyo Mungu unayedai yupo,ila Hana jina?
 
Hii kitu haijawahi ingia akili mwangu! Ni somo ambalo halieleweki tofauti na Mungu wa kwenye Biblia, huyu Annunaki haeleweki! Mara mnasema anakuja kufanya utafuti najiuliza utafiti gani??? Mungu ndiye muumba wa vyote na anajua yote bila shaka anapaswa kujua ilipo shehena ya dhahabu lakini huyu hajui lolote kutwa kucha kiguuguu na njia anafanya utafiti toka sayari moja kwenda nyingine eti anasaka shehena ya dhahabu, kweli?

Haya, yataletwa na maelezo lukuki mwisho wa siku mnasema mtangulizi wa Annunaki alikuwa alalu halafu nashtuka he... Kumbe Annunaki siyo mwanzilishi? Kumbe kuna watangulizi tena? Mmmh inafikirisha sana! Hapana, nadhani shetani anataka kutupiga na kitu kizito usoni! Shitukeni, hawa siyo Mungu! Tuungane, tumkatae🤣🤣🤣 atatuchonganisha na Mungu wetu! Maelezo yake ni lugha gongana sijapata kuona aiseee!
 
Nadhani watu wengi sana mnachanganya mambo kutokana na uelewa finyu,Hivi kati ya Mungu wa kwenye BIBLIA na Annunak wa kwenye maandishi ya Sumeria nani mkongwe?

Sumeria Deities yaani Enki na Enlil ni wakongwe kuliko huyo Mungu wa Abrahamic Religion na usichokijua hata mwanzilishi wa hiyo Imani aliwaabudu hao hao ANUNAK Hivi Kwa ufahamu wako unadhani Biblia inamtaja Mungu Gani kama Sio Elohim/YWH mmoja wa miungu Annunaki Katika Mesopotamia aliyeabudiwa na Abraham aliyetokea Uru ya Ukaldayo Mesopotamia ambako ndio nadharia ya Miungu ilianza!

Halafu kingine rejea maana ya neno 'Mungu' nimelifafanua kule Juu maana yake likiwa kama cheo sio jina la kiumbe yeyote unayemfikiria kwenye kichwa chako maana huyo Mungu hayupo na Hakuna uthibitisho juu ya uwepo wake!
 
Dumas the terrible:kwa hiyo wewe binafsi unajua au unaamini nini na baada ya Kifo chako nini kitafuata?

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
unaweza ukanipa uthibitisho Juu ya Uwepo wa huyo Mungu unayedai yupo,ila Hana jina
Sidhani kama ni jambo sahihi kuutafuta uthibitisho kwa maana ya kithibiti. Ila kulikaribia hilo lengo labda kuna uthibitisho wa uhalali wa wazo la Mungu. Ulifanyika kwa analojia ya kibailojia;

Kidole kadogo akitaka kumthibitishia kidole gumba kwamba 'mtu' wanayemtumikia yupo atatumia kithibitisho gani? nikwambie tu kwamba hata akiweza kumuonesha ubongo atakuwa bado hajathibitisha kuwa huyo 'mtu' yupo. Sababu hapo inakuwa mtu yupo katika mfumo wa 'wazo' wakati vidole ni mifupa na nyama. Mifupa na nyama inaweza kuinteract na majimaji, gesi mpaka miale labda lakini haiwezi kuifikia levo ya wazo. Ni mpaka ama wazo lichukue umbo la mifupa na nyama au au mifupa na nyama vikubali kulitambua wazo kama lilivyo.

Vidole vya mwili wako vinatumikiana vyenyewe na kuvitumikia viungo vingine vyoote pia na kwa kufanya hivyo vinamtumikia mtu pia. Kumbuka viungo vingine pia vinatumikiana na viungo vyote vingine ikiwamo vyenyewe! Kuhusu vinamtambua au havimtambui huyo MTU mimi sijui. Lakini ninachojua ni kwamba mtu anao upendo kwa viungo vyote vya mwili wake regardless yeye yupo juu ya vyote na ndani ya vyote. Hashikiki na hathibitishiki kimashikomashiko
 
Ilipanza vizuri sasa unaanza kuunyea Uzi wako.... Ukishaleta mambo ya Mungu Mungu na ukahusanisha na Imani za watu ...ushalinyera.... Ungebaki kwenye historia yako tu.
ukiwa ni mwenye akili timamu huwezi watenganisha accient Sumerian na dhana za Mungu na miungu hebu Soma kichwa Cha mada acha kukurupuka,
Mesopotamia ndipo ilipoanzia dhana ya Mungu na hekalu la kwanza la Mungu ANU Katika Uruk ndipo ilipoanzia.

Kitu kingine angalia tafsiri ya neno Mungu/Miungu ndipo uje uniqote Tena,
Karibu!
 
Mbona unaamin anunak
Daaaa aisee kazi ipo Annunaki sio Imani ni jamii ya viumbe kutoka Sayari ya Nibiru au Nephilims 12th Planet walioitembelea Dunia miaka zaidi ya 350,000 BCE Kwa ajili ya kuutafuta dhahabu na ndio walianzisha ustaarabu wa Mwanzo kama kujenga Pyramids,kuchimba Dhahabu na madini mbali mbali,pia walifanya mambo mengi Sana Katika accient world
ANUNNAK mwonekano wao ni kama Binadamu tulivyo ila ni wa refu futi Mpaka 12 wakiwa na mbawa mbili,
Ukiangalia michoro ya kale ya Wasumeria utawaona pia Kwa jamii za Israelites waliwaita Nephilims/Watchers/Angels

Watu wa kale waliwaabudu kama miungu sababu ndio waliofanya human cloning na human manipulation akapatikana
Homo sapiens,hivyo ilikua simple watu kuwaabudu kama miungu
Hujiulizi Kwa Nini Vitabu vya dini vimewaandika kwamba zamani Malaika walikuja duniani kutoka mbinguni na kuishi na watu lakini Leo kwanini hawaji?
Utapata jibu ya kwamba wale viumbe waliondoka na kurudi huko kwao na hawajawahi rejea ila nadharia zao kupitia dini zote duniani Bado zipo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…