Anwar Sadat na Mohamed Heykal

Anwar Sadat na Mohamed Heykal

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MONTAZA PALACE ALEXANDRIA 1988

Leo asubuhi nimeingia Maktaba na kukuta picha ya Montaza Palace.

Nilifika Montaza Palace kusali sala ya Ijumaa mwaka wa 1988 nilikuwa kwenye kozi mjini Akexandria na aliyenichukua alikuwa mmoja wa walimu zangu alipojua kuwa mimi ni Muislam.

Kozi ilikuwa na wanafunzi wengi kutoka Afrika lakini katika kundi zima lile Waislamu tulikuwa wawili tu.

Hii Montaza Palace lilikuwa jumba la Mfalme Farouk wa Misri la mapumziko yake wakati wa Kiangazi.

Montaza Palace baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1952 Gamal Abdel Nasser aligeuza kuwa Kasri la Wananchi na kwa ajili hii msikiti uliokuwa ndani ya viwanja vya jengo hili ukawa wazi kwa watu kuja wakati wowote kusali

Niliikumbuka Montaza Palace na kushukuru kufika hapo baada ya kukisoma kitabu cha Mohamed Heykal, "The Road to Ramadan," alipokuwa akieleza Vita vya Yom Kippur mwaka 1973 wakati Misri na Syria zilipopigana na Israel.

Vita vilikuwa vinawaendea vizuri Waarabu na Anwar Sadat akaamua kuja Alexandria wakati vita bado vinauma.

Majeshi ya Misri yalikuwa yamevuka Suez Canal na kuingia Sinai na kuvunja Bar Lev Line mlima wa mchanga uliojengwa na Wayahudi kuzuia mashambulizi kutoka Misri baada ya Six Day War 1967.

Huyu Heykal mtu mwenye akili sana na akiheshimiwa mno Misri kwa ajili ya bongo lake.

Basi akaenda Alexandria kupata taarifa za vita kutoka kwa Commander in Chief mwenyewe na hivi ndivyo alivyojikuta uso kwa uso na Anwar Sadat ndani ya Montaza Palace.

Heykal mtu wa tasnifa sana.
Ukimsoma sharti utacheka.

Heykal anaeleza katika kitabu hicho kuwa, "Kwa muda Sadat aliniangalia bila ya kunijibu swali langu mkononi kashika glasi ya kinywaji chake hadi alipomaliza kunywa.

Alipomaliza kunywa akaniambia, "Heykal acha kunishughulisha na maswali yako madogo madogo mimi ni Mkuu wa Majeshi nashughulishwa na mambo makubwa.

Hayo mambo yako majibu ungeweza kupata Cairo."

Sasa Heykal anaanza kumkanyaga Sadat.

Heykal anasema Sadat akishughulishwa sana na muonekano wake kiasi kuwa uniform zake za Commander in Chief aliziagiza kutoka Paris na zilitoka kwa designer mkubwa sana duniani - Yves Saint Laurent.

Heykal bado anashindilia anasema, "Sadat alipokuwa kijana alitaka kuwa muigizaji lakini alikuwa hana kipaji hicho sasa alipokuja kuwa Rais zile camera za tv kwake yeye aliziona kama camera za Hollywood."

Huyu ndiye Mohamed Hasnain Heykal.

Hii picha ya Montaza Palace katika Maktaba imenikumbusha mengi.

 
Shukran mzee wetu kwa kutupa japo kwa uchache historia ya MONTAZA PALACE la huko ALEXANDRIA.
Ukipata muda tunaomba utuchambulie japo kwa uchache sababu zilizopelekea waarabu kushindwa katika na Israel katika hio vita ya Six Day War, mimi nnamashaka sana na Saudi Arabia kuhusika katika kushindwa kwao.
Hivi kwa nini Msaudi hakushiriki kabisa na waarabu wenzake katika vita hio.
 
Mwalimu wako alikuchukua kukupeleka chakulani baada kugundua ww ni mwislam, Mohamed said kuwa makini sana na kuutumia uislam kama jukwaa lako, uislam hauna shida na yeyote lakini wewe ulishaanza kuwa na tatizo, nimefatilia kwa muda yaani unashidwa kuuwakilisha uislamu kwa njia sahihi
 
Mwalimu wako alikuchukua kukupeleka chakulani baada kugundua ww ni mwislam, Mohamed said kuwa makini sana na kuutumia uislam kama jukwaa lako, uislam hauna shida na yeyote lakini wewe ulishaanza kuwa na tatizo, nimefatilia kwa muda yaani unashidwa kuuwakilisha uislamu kwa njia sahihi
Emanuel...
Darasa zima tulikuwa Waislam wawili na aliponijua alichukua interest
ya kujua nchi ninayotoka na akauliza mbona mmkekuja hapa nyie
wachache kutoka nchini kwenu imekuwaje wenzenu ni wengi?

Maana kulikuwapo na washiriki kutoka Tanzania kundi kubwa.
Nilimjulisha kwa nini imekuwa hivyo.

Alinisikiliza kwa makini sana.
Aliniuliza kama namfahamu Um Kulthum nk. nk,

Alishangaa nilipomwambia kuwa mama zetu wakifurahi wanaimba
nyimbo za Um Kulthum.

Nikamweleza kuwa nawajua Mohamed Abdulwahab, Abdulhalim
Hafiz, Farid Atrash, Fairuz
nk.

Nikamfahamisha utamaduni wetu wa Kiislam uko sawa na wao na
mengi nikamueleza.

Hivi ndivyo alivyonichukua twende kusali pamoja sala ya Ijumaa pale
Montaza Palace.

Alishangaa zaidi aliponiuliza baada ya sala kama nimeelewa khutba.
Nikamjibu kuwa khatibu kasoma aya za Hijja.

''Umejuaje ilhali wewe hujui Kiarabu?'' aliniuliza.
Nikamwambia naijua Qur'an.

Furaha yake haikusemeka,

Unanitahadharisha niwe makini kutumia Uislam...

Mimi Mohamed Said Salum Abdallah, babu yangu Salum Abdallah
baba yake alimpeleka Unguja kusoma dini mwanzoni mwa 1900.

Mimi Mohamed jina hili ni la babu mzaa mama, Sheikh Mohamed
Mvamila
aliyehama Mkamba Uzaramo akiwa kijana hajapata hata mtoto
akahamia Musoma kwenda kusomesha Uislam na kazikwa huko.

Unanambia ati niwe makini na Uislam tena maneno haya unayasema
Tanzania kwenye nchi ambayo Waislam wako karne na karne.

Uislam mie naupenda sana na ndiyo maisha yangu sijapatapo kuona
aibu kujulikana mie ni Muislam hata siku moja.

Nimeandika hadi kitabu kuonyesha mchango wa Waislam katika TANU
kuundwa kwake na ushiriki wao kumuunga Mwalimu Nyerere mkono
na jinsi walivyopambana na ukoloni.

Ikiwa unataabika na Uislam wangu bora zikwepe post zangu usisome
ukajiudhi bure.
 
Shukran mzee wetu kwa kutupa japo kwa uchache historia ya MONTAZA PALACE la huko ALEXANDRIA.
Ukipata muda tunaomba utuchambulie japo kwa uchache sababu zilizopelekea waarabu kushindwa katika na Israel katika hio vita ya Six Day War, mimi nnamashaka sana na Saudi Arabia kuhusika katika kushindwa kwao.
Hivi kwa nini Msaudi hakushiriki kabisa na waarabu wenzake katika vita hio.
Mgugu,
Historia ya Six Day War hatuwezi tukaieleza hapa kwani ni ndefu lakini
vitabu vipo ambavyo utaweza kusoma na kuna maelezo mengi.

Lakini kitu kilichosababisha ushindi wa Israel ni kuwa walifanya pre-emptive
strike, yaani shambulizi la kushtukiza na karibu ndege za kivita 345 Misri
zilipigwa chini uwanjani.

Vita vikaanza Misri wakiwa hawana jeshi la anga.

Katika Siku Sita Nasser akasalimu amri na ndiyo ukawa mwisho wa vita na
Sinai, Golan Heights zikatekwa pamoja na Jerusalem.

Nitakuelezea kitu.

Waarabu wakajitayarisha na wakafanya vita vingine mwaka wa 1973 The Yom
Kippur War.

Vita hivi Misri na Syria walipigana kiasi ambacho dunia ilishangazwa sana.
Lakini katikati ya ushindi huu pakatokea ''matatizo,'' katika kuendesha hivyo
vita.

Saadat akasimamisha majeshi yake yasisonge mbele.

Hapo juu inaona nimeweka neno, ''matatizo,'' kwa hofu ya mimi kutumia neno
''usaliti.''

Lakini neno hili limetumika ndani ya jeshi la Misri na vijana ambao baadae kwa
huu usaliti waliamua kumpitishia adhabu ya kifo Saadat na ikatekelezwa.

Kuna barua ya mkono aliandika Hafiz Al Asaad wakati wa vita alipopata taarifa
kuwa Misri wamesimamisha vita majeshi yao hayasongi mbele na Syria sasa iko
peke yake kupambana na Israel.

Barua hii ipo katika kitabu cha Heykal, ''The Road to Ramadan.''

Hafiz Al Asaad alianza ile barua kwa maneno haya, ''Ndugu yangu Saadat hakuna
wakati ambao Waarabu wanaweza kurudisha heshima yao kama sasa...''

Hafiz Al Asaad alimsihi sana Saadat asirejeshi majeshi yake nyuma.
Yaliyotokea sasa ni historia kwani yote yanafahamika.

Saadat anadai kuwa walishinda Vita Vya Yom Kippur na nimefika sehemu moja
Cairo inaitwa Heliopolis, nilikuwa napita njia tu na nikakuta imejengwa kitu kama
mnara na kuna sanamu za madege na vifaru na pameandikwa aya ya Qur'an
isemayo, ''Msiseme kuwa wale waliokufa katika njia ya Allah wamekufa bali wahai...''

Hii imejenga kama alama ya kumbukumbu ya ushindi wa vita vile.

Lakini vita iliyokuja kuandika historia mpya kati ya Waarabu na Wayahudi ni vile
vya Hizbullah chini ya uongozi wa Hassan Nasralla walipopambana na Israel
mwaka wa 2006.

Vita vilipiganwa kwa siku 34 na baada ya UN kuleta sulhu kwa mara ya kwanza
majeshi ya Israel yalionyeshwa na vyombo vikubwa vya habari duniani kama
CNN, BBC wakirudi kwao wameinamisha vichwa vyao chini.

Nini yalikuwa maneno ya Hassan Nasralla?
 
Mgugu,
Historia ya Six Day War hatuwezi tukaieleza hapa kwani ni ndefu lakini
vitabu vipo ambavyo utaweza kusoma na kuna maelezo mengi.

Lakini kitu kilichosababisha ushindi wa Israel ni kuwa walifanya pre-emptive
strike, yaani shambulizi la kushtukiza na karibu ndege za kivita 345 Misri
zilipigwa chini uwanjani.

Vita vikaanza Misri wakiwa hawana jeshi la anga.

Katika Siku Sita Nasser akasalimu amri na ndiyo ukawa mwisho wa vita na
Sinai, Golan Heights zikatekwa pamoja na Jerusalem.

Nitakuelezea kitu.

Waarabu wakajitayarisha na wakafanya vita vingine mwaka wa 1973 The Yom
Kippur War.

Vita hivi Misri na Syria walipigana kiasi ambacho dunia ilishangazwa sana.
Lakini katikati ya ushindi huu pakatokea ''matatizo,'' katika kuendesha hivyo
vita.

Saadat akasimamisha majeshi yake yasisonge mbele.

Hapo juu inaona nimeweka neno, ''matatizo,'' kwa hofu ya mimi kutumia neno
''usaliti.''

Lakini neno hili limetumika ndani ya jeshi la Misri na vijana ambao baadae kwa
huu usaliti waliamua kumpitishia adhabu ya kifo Saadat na ikatekelezwa.

Kuna barua ya mkono aliandika Hafiz Al Asaad wakati wa vita alipopata taarifa
kuwa Misri wamesimamisha vita majeshi yao hayasongi mbele na Syria sasa iko
peke yake kupambana na Israel.

Barua hii ipo katika kitabu cha Heykal, ''The Road to Ramadan.''

Hafiz Al Asaad alianza ile barua kwa maneno haya, ''Ndugu yangu Saadat hakuna
wakati ambao Waarabu wanaweza kurudisha heshima yao kama sasa...''

Hafiz Al Asaad alimsihi sana Saadat asirejeshi majeshi yake nyuma.
Yaliyotokea sasa ni historia kwani yote yanafahamika.

Saadat anadai kuwa walishinda Vita Vya Yom Kippur na nimefika sehemu moja
Cairo inaitwa Heliopolis, nilikuwa napita njia tu na nikakuta imejengwa kitu kama
mnara na kuna sanamu za madege na vifaru na pameandikwa aya ya Qur'an
isemayo, ''Msiseme kuwa wale waliokufa katika njia ya Allah wamekufa bali wahai...''

Hii imejenga kama alama ya kumbukumbu ya ushindi wa vita vile.

Lakini vita iliyokuja kuandika historia mpya kati ya Waarabu na Wayahudi ni vile
vya Hizbullah chini ya uongozi wa Hassan Nasralla walipopambana na Israel
mwaka wa 2006.

Vita vilipiganwa kwa siku 34 na baada ya UN kuleta sulhu kwa mara ya kwanza
majeshi ya Israel yalionyeshwa na vyombo vikubwa vya habari duniani kama
CNN, BBC wakirudi kwao wameinamisha vichwa vyao chini.

Nini yalikuwa maneno ya Hassan Nasralla?
Enyi waarabu weusi na weupe hamjawahi kumshinda myahudi.
Mara zote mmekuwa mkichakazwa mkachakazika vyema.
Bila kuwatumia watoto na wanawake kama ngao yale makundi yenu ya kihalifu na kigaidi yangeshamalizwa muda mrefu.
Na ukibisha waambie wawaondoe wayahudi pale walipo.
Mtabaki kulia lia mpaka Bwana Yesu arudi aje alichukue Taifa lake na kuwaeleza ninyi njia ile pana mpite.
 
Ni maumivu yasiyoisha nikikumbuka ile vita jinsi tulivyochakazwa na myahudi
 
Kama sio UN Israel ungeangamiza waarabu wengi
Tuombe aman mashariki ya kati
Mgugu,
Historia ya Six Day War hatuwezi tukaieleza hapa kwani ni ndefu lakini
vitabu vipo ambavyo utaweza kusoma na kuna maelezo mengi.

Lakini kitu kilichosababisha ushindi wa Israel ni kuwa walifanya pre-emptive
strike, yaani shambulizi la kushtukiza na karibu ndege za kivita 345 Misri
zilipigwa chini uwanjani.

Vita vikaanza Misri wakiwa hawana jeshi la anga.

Katika Siku Sita Nasser akasalimu amri na ndiyo ukawa mwisho wa vita na
Sinai, Golan Heights zikatekwa pamoja na Jerusalem.

Nitakuelezea kitu.

Waarabu wakajitayarisha na wakafanya vita vingine mwaka wa 1973 The Yom
Kippur War.

Vita hivi Misri na Syria walipigana kiasi ambacho dunia ilishangazwa sana.
Lakini katikati ya ushindi huu pakatokea ''matatizo,'' katika kuendesha hivyo
vita.

Saadat akasimamisha majeshi yake yasisonge mbele.

Hapo juu inaona nimeweka neno, ''matatizo,'' kwa hofu ya mimi kutumia neno
''usaliti.''

Lakini neno hili limetumika ndani ya jeshi la Misri na vijana ambao baadae kwa
huu usaliti waliamua kumpitishia adhabu ya kifo Saadat na ikatekelezwa.

Kuna barua ya mkono aliandika Hafiz Al Asaad wakati wa vita alipopata taarifa
kuwa Misri wamesimamisha vita majeshi yao hayasongi mbele na Syria sasa iko
peke yake kupambana na Israel.

Barua hii ipo katika kitabu cha Heykal, ''The Road to Ramadan.''

Hafiz Al Asaad alianza ile barua kwa maneno haya, ''Ndugu yangu Saadat hakuna
wakati ambao Waarabu wanaweza kurudisha heshima yao kama sasa...''

Hafiz Al Asaad alimsihi sana Saadat asirejeshi majeshi yake nyuma.
Yaliyotokea sasa ni historia kwani yote yanafahamika.

Saadat anadai kuwa walishinda Vita Vya Yom Kippur na nimefika sehemu moja
Cairo inaitwa Heliopolis, nilikuwa napita njia tu na nikakuta imejengwa kitu kama
mnara na kuna sanamu za madege na vifaru na pameandikwa aya ya Qur'an
isemayo, ''Msiseme kuwa wale waliokufa katika njia ya Allah wamekufa bali wahai...''

Hii imejenga kama alama ya kumbukumbu ya ushindi wa vita vile.

Lakini vita iliyokuja kuandika historia mpya kati ya Waarabu na Wayahudi ni vile
vya Hizbullah chini ya uongozi wa Hassan Nasralla walipopambana na Israel
mwaka wa 2006.

Vita vilipiganwa kwa siku 34 na baada ya UN kuleta sulhu kwa mara ya kwanza
majeshi ya Israel yalionyeshwa na vyombo vikubwa vya habari duniani kama
CNN, BBC wakirudi kwao wameinamisha vichwa vyao chini.

Nini yalikuwa maneno ya Hassan Nasralla?
 
Enyi waarabu weusi na weupe hamjawahi kumshinda myahudi.
Mara zote mmekuwa mkichakazwa mkachakazika vyema.
Bila kuwatumia watoto na wanawake kama ngao yale makundi yenu ya kihalifu na kigaidi yangeshamalizwa muda mrefu.
Na ukibisha waambie wawaondoe wayahudi pale walipo.
Mtabaki kulia lia mpaka Bwana Yesu arudi aje alichukue Taifa lake na kuwaeleza ninyi njia ile pana mpite.
Kipuyo,
Nimeeleza vita baina ya Waarabu na Wayahudi Six Day War, Yom Kippur
na vita vya Hizbullah na Israel.

Ikiwa unataka kuelewa nini kilitokea katika vita vile unaweza kusoma mengi
katika mitandao:

''Hezbollah captured two Israeli soldiers at the border, which sparked a sustained aerial and ground war by Israeli forces — and tough resistance by Hezbollah. Both claimed victory, but neither won. In Israel, the 2006 Lebanon war is widely viewed by Israelis as a military failure.''
 
Ni maumivu yasiyoisha nikikumbuka ile vita jinsi tulivyochakazwa na myahudi
Yitzak,
Hutaki kujua maneno aliyosema Hassan Nasrallah?
Mbinu za vita zimebadilika sana kutoka Six Day War mwaka wa 1967.
 
tupe madini sheikh wangu wengine tulikuwa bado sana
Mamba1,
Hassan Nasralla wakati vita vikiendelea alikuwa akihutubu kwenye TV Station ya Hizbullah akisema, "Yako wapi majeshi ya Israel kwenye uwanja wa vita? Tunachoona ni ndege zao zikiruka angani na kudondosha mabomu kuvunja nyumba za raia."

Vita vilipoanza ulimwengu mzima uliamini baada ya siku chache Hizbullah watakuwa wamesalimu amri. Haikuwa hivyo. Siku zikawa majuma na kuendelea mbele hadi ikadhihiri kuwa vita hivi havishi karibuni.

Mwezi ukakatika na makombora ya Hizbullah yanazidi kutua Israel.

Wapatanishi wakaingia kati kumaliza vita.

Wajuzi wa siasa za Mashariki ya Kati wakawa wanaangalia vita za nyuma baina ya Hizbullah na Israel wakawa sasa wanasema kuwa Israel walipovamia Lebanon na kukalia sehemu yake Hizbullah waliwatangazia vita na vita viliuma hadi Israel ikaondoka.

Kwa nini Israel iliondoka kusini ya Lebanon?
Wayahudi wanaogopa sana kifo.

Hassan Nasralla akasema, "Sisi tunakwenda uwanja wa mapambano kwenda kufa. Wayahudi wanakuja wakitaka warejee majumbani kwao ndiyo utaona mbele wanatanguliza matenki na wao wanajificha nyuma na nyuma kabisa wanaweka ambulance."

Hassan Nasralla alipokuwa anasema maneno haya akawa anacheka.

Wayahudi wakawa wanasema ni vigumu kupigana na adui anaekuja vitani kufa.

Baada ya vita kwisha na kuanza kubadilishana mateka simanzi kubwa iligubika Israel pale walipokuwa wanapokea majeneza ya askari wao waliouliwa na wao wanawaachia askari walio hai wa Hizbullah.

Hassan Nasralla akahitimisha kwa kusema, "Sisi hatutaki vita na Israel lakini tuko tayari kupambananao wakati wowote."

Swali kubwa linaloshughulisha wataalamu wa mambo ya vita ni iweje jeshi lililokuwa na sifa kubwa kana IDF lishindwe na jeshi la mgambo?
 

Mamba1,
Hassan Nasralla wakati vita vikiendelea alikuwa akihutubu kwenye TV Station ya Hizbullah akisema, "Yako wapi majeshi ya Israel kwenye uwanja wa vita? Tunachoona ni ndege zao zikiruka angani na kudondosha mabomu kuvunja nyumba za raia."

Vita vilipoanza ulimwengu mzima uliamini baada ya siku chache Hizbullah watakuwa wamesalimu amri. Haikuwa hivyo. Siku zikawa majuma na kuendelea mbele hadi ikadhihiri kuwa vita hivi havishi karibuni.

Mwezi ukakatika na makombora ya Hizbullah yanazidi kutua Israel.

Wapatanishi wakaingia kati kumaliza vita.

Wajuzi wa siasa za Mashariki ya Kati wakawa wanaangalia vita za nyuma baina ya Hizbullah na Israel wakawa sasa wanasema kuwa Israel walipovamia Lebanon na kukalia sehemu yake Hizbullah waliwatangazia vita na vita viliuma hadi Israel ikaondoka.

Kwa nini Israel iliondoka kusini ya Lebanon?
Wayahudi wanaogopa sana kifo.

Hassan Nasralla akasema, "Sisi tunakwenda uwanja wa mapambano kwenda kufa. Wayahudi wanakuja wakitaka warejee majumbani kwao ndiyo utaona mbele wanatanguliza matenki na wao wanajificha nyuma na nyuma kabisa wanaweka ambulance."

Hassan Nasralla alipokuwa anasema maneno haya akawa anacheka.

Wayahudi wakawa wanasema ni vigumu kupigana na adui anaekuja vitani kufa.

Baada ya vita kwisha na kuanza kubadilishana mateka simanzi kubwa iligubika Israel pale walipokuwa wanapokea majeneza ya askari wao waliouliwa na wao wanawaachia askari walio hai wa Hizbullah.

Hassan Nasralla akahitimisha kwa kusema, "Sisi hatutaki vita na Israel lakini tuko tayari kupambananao wakati wowote."

Swali kubwa linaloshughulisha wataalamu wa mambo ya vita ni iweje jeshi lililokuwa na sifa kubwa kana IDF lishindwe na jeshi la mgambo?
Ahsantaaa sheikh
 
Back
Top Bottom