Anza biashara bila mtaji wa pesa

Anza biashara bila mtaji wa pesa

wa zion

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2013
Posts
223
Reaction score
481
Katika maisha kila mtu anapenda afanikiwe na kuweza kukidhi mahitaji yetu ya kila siku. Leo naongea na wewe ambae unawaza siwezi kufanya biashara sababu sina mtaji kwa kutoa uzoefu wangu mdogo kwenye biashara niliyoanza kiutani utani na nashukuru Mungu mambo sasa yanaenda vizuri kabisa.

Miezi michache iliyopita nilianza kuuza dagaa wa mwanza wa kukaanga na wakavu bila ya kutumia pesa yangu yoyote(NB: pesa nilikuwa nayo nilitaka kujaribu hili wazo langu) nilianzaje? kwa upande wangu ninaishi mwanza kwa sasa nikiwa sina ujuzi wowote wa biashara hii niliwatafuta wamama wanaouza dagaa wakavu nikawauliza bei ya dagaa wanayouzia nikakutanana na elfu 5 kwa sado nikamuita mama mmoja pembeni nikamwambia mimi nitakua nanunua kwako tu nataka bei ya jumla akaniambia dagaa wakavu jumla nitakuuzia 3500 kwa sado moja tukakubaliana nikapiga picha dagaa zake.

Nikachunguza bei ya dagaa wakavu Dar wanaoanikwa kwenye mawe, nikakutana na bei ya elfu nane kwa kilo moja dagaa wa kawaida tu nikaona itanilipa, kifupi niliingia facebook kule kuna makundi mengi ya wanawake wanasogoa tu nikatangaza biashara yangu kwa kuwambia kwamba ninakufikishia hadi mlangoni (nani asiependa hii raha ) nikawauzia 6500, unalipia kwanza kabla ya kupata mzigo wako (njia niliyotumia nyingine ni kuwafundisha wapi wanaweza kuuza dagaa watakao nunua kwangu mfano mama ntilie, masokoni)

Nikatafuta oda za dagaa wa kukaanga nikapata hii ilikua kwenye benki moja hapo mjini sikuwa na connection yoyote nilipost kwenye magroup ya whatsapp nikapata oda moja tu na huyo huyo mteja akaanza kunimiminia wateja wa kutosha, kukuza soko kwenye corporate industry nikampa ndugu yangu mmoja sample ya dagaa wa kukaanga(daraja la kwanza) nikamwambia sasa ingia kwenye maofisi ukifika wape waonje na tangaza soko lako na sasa si haba biashara inaenda vizuri.

vijana msio na ajira na mnaotoka vyuoni, tumieni vizuri mitandao ya kijamii na tafuta biashara kutokana na sehemu ulipo, si lazima uanze na pesa kubwa kuna biashara kauli unazotoa tu ndio biashara yenyewe
 
Katika maisha kila mtu anapenda afanikiwe na kuweza kukidhi mahitaji yetu ya kila siku. Leo naongea na wewe ambae unawaza siwezi kufanya biashara sababu sina mtaji kwa kutoa uzoefu wangu mdogo kwenye biashara niliyoanza kiutani utani na nashukuru Mungu mambo sasa yanaenda vizuri kabisa.

Miezi michache iliyopita nilianza kuuza dagaa wa mwanza wa kukaanga na wakavu bila ya kutumia pesa yangu yoyote(NB: pesa nilikuwa nayo nilitaka kujaribu hili wazo langu) nilianzaje? kwa upande wangu ninaishi mwanza kwa sasa nikiwa sina ujuzi wowote wa biashara hii niliwatafuta wamama wanaouza dagaa wakavu nikawauliza bei ya dagaa wanayouzia nikakutanana na elfu 5 kwa sado nikamuita mama mmoja pembeni nikamwambia mimi nitakua nanunua kwako tu nataka bei ya jumla akaniambia dagaa wakavu jumla nitakuuzia 3500 kwa sado moja tukakubaliana nikapiga picha dagaa zake.

Nikachunguza bei ya dagaa wakavu Dar wanaoanikwa kwenye mawe, nikakutana na bei ya elfu nane kwa kilo moja dagaa wa kawaida tu nikaona itanilipa, kifupi niliingia facebook kule kuna makundi mengi ya wanawake wanasogoa tu nikatangaza biashara yangu kwa kuwambia kwamba ninakufikishia hadi mlangoni (nani asiependa hii raha ) nikawauzia 6500, unalipia kwanza kabla ya kupata mzigo wako (njia niliyotumia nyingine ni kuwafundisha wapi wanaweza kuuza dagaa watakao nunua kwangu mfano mama ntilie, masokoni)

Nikatafuta oda za dagaa wa kukaanga nikapata hii ilikua kwenye benki moja hapo mjini sikuwa na connection yoyote nilipost kwenye magroup ya whatsapp nikapata oda moja tu na huyo huyo mteja akaanza kunimiminia wateja wa kutosha, kukuza soko kwenye corporate industry nikampa ndugu yangu mmoja sample ya dagaa wa kukaanga(daraja la kwanza) nikamwambia sasa ingia kwenye maofisi ukifika wape waonje na tangaza soko lako na sasa si haba biashara inaenda vizuri.

vijana msio na ajira na mnaotoka vyuoni, tumieni vizuri mitandao ya kijamii na tafuta biashara kutokana na sehemu ulipo, si lazima uanze na pesa kubwa kuna biashara kauli unazotoa tu ndio biashara yenyewe
Nashukur sana ndugu....
Tutalifanyia kazi asa fursa kama izi ..nimejifunza kuwa ba kauli nzuri kwa mteja
Mi nna 500000 sina business idea yyte ..je waweza nisaidia mi nipo dar ifm
 
Nashukur sana ndugu....
Tutalifanyia kazi asa fursa kama izi ..nimejifunza kuwa ba kauli nzuri kwa mteja
Mi nna 500000 sina business idea yyte ..je waweza nisaidia mi nipo dar ifm
kuna thread humu inaongelea biashara ya kufanya ukiwa chuoni ipitie itakusaidia, kwa Ifm ningekwambia uza urembo wa wanawake, nguo za ndani, kama una mtu fungua sehemu ya matunda au kama unaweza jifunze kubandika kucha na kupaka rangi muda wako wa ziada utumie kupaka rangi wasichana kwenye hostel zao.
 
kuna thread humu inaongelea biashara ya kufanya ukiwa chuoni ipitie itakusaidia, kwa Ifm ningekwambia uza urembo wa wanawake, nguo za ndani, kama una mtu fungua sehemu ya matunda au kama unaweza jifunze kubandika kucha na kupaka rangi muda wako wa ziada utumie kupaka rangi wasichana kwenye hostel zao.
Ntajitahidi kk ila ya matunda imekaa poa zaid
 
Safi sanaNa kweli biashara ni ujanja tu unaangalia gape liko wp unaingia front!
Huwa inaanza kwa wazo..ukitia nia na wazo lako automatic hela utapata tu!
 
Safi sanaNa kweli biashara ni ujanja tu unaangalia gape liko wp unaingia front!
Huwa inaanza kwa wazo..ukitia nia na wazo lako automatic hela utapata tu!
Ni kweli ukisema usubiri upate hela ya mtaji haitakuja na wala haitatosha,kujiongeza tu kunatakiwa.
 
Ni kweli ukisema usubiri upate hela ya mtaji haitakuja na wala haitatosha,kujiongeza tu kunatakiwa.
Na ukianza biashara haichujkuagi muda milango ya fursa inafunguka zaidi...yaan sijui inakuaga km fursa umezifungia hv ukianza tu deal kibao za kukuingiza zaidi mapato!
Kwahyo hizo dagaa za kikaangwa unauzia mwanza tu!?watamu jaman wale dagaa..sema wameanza chakachuaa
 
Back
Top Bottom