Tengeneza Njia
Senior Member
- Jul 29, 2022
- 121
- 205
Wadau,
Katika kipindi chote cha kuona serikali tofauti tofauti hapa Tanzania kero ambazo zimekuwa zikijirudia rudia sana ni hii ya upatikanaji wa maji na umeme.
Watanzania wameshazoea kuiomba serikali kupewa huduma hizi kitu ambacho ni haki yao tena ya msingi kama walipa kodi.
Ifike mahali tutumie historia kama best practice kuona namna ambavyo tunaweza kujikwamua katika changamoto ambazo imekuwa kama trend kuendelea kutokea na changamoto hizi kutumika na wanasiasa kujinadi wanapotaka kupewa kura vipindi vya uchaguzi kuwa "mkinichagua nitawaletea maji, umeme etc."
Tulitokaje kwenye mfumo wa kuwa na kampuni moja tu ya mawasiliano (ya kiserikali TTCL) mpaka sasa ambapo yapo makampuni mengi na wananchi wanapata nafasi ya kuchagua huduma ya simu wanaotaka.
Ifike sasa sekta binafsi iruhusiwe kuanzisha mifumo mingine itakayokuwa inatoa huduma za maji na umeme kubwa zaidi tofauti na kutegemea hizi za serikali tu, kama tulivyokuwa na mashirika ya bima tofautitofauti.
Katika kipindi chote cha kuona serikali tofauti tofauti hapa Tanzania kero ambazo zimekuwa zikijirudia rudia sana ni hii ya upatikanaji wa maji na umeme.
Watanzania wameshazoea kuiomba serikali kupewa huduma hizi kitu ambacho ni haki yao tena ya msingi kama walipa kodi.
Ifike mahali tutumie historia kama best practice kuona namna ambavyo tunaweza kujikwamua katika changamoto ambazo imekuwa kama trend kuendelea kutokea na changamoto hizi kutumika na wanasiasa kujinadi wanapotaka kupewa kura vipindi vya uchaguzi kuwa "mkinichagua nitawaletea maji, umeme etc."
Tulitokaje kwenye mfumo wa kuwa na kampuni moja tu ya mawasiliano (ya kiserikali TTCL) mpaka sasa ambapo yapo makampuni mengi na wananchi wanapata nafasi ya kuchagua huduma ya simu wanaotaka.
Ifike sasa sekta binafsi iruhusiwe kuanzisha mifumo mingine itakayokuwa inatoa huduma za maji na umeme kubwa zaidi tofauti na kutegemea hizi za serikali tu, kama tulivyokuwa na mashirika ya bima tofautitofauti.