Siku zote Watanzania tukishaona tumefikia steji fulani basi hutaki kukubali ukweli, hata leo JF app imeridhika.
Tuje kwenye app ya Simba, mara ya kwanza kuzinduliwa hii app niliona itakuja kuwa mchango mzuri kwa wapenzi wa burudani kuhusu Simba na habari zake, ila likaja na swala la kulipa ada ili kupata habari. Lakini malipo ukilipa hakuna chochote ni kama imezubaa tu na mwisho wa siku wanajisifu kukusanya pesa nyingi.
Pitapita yangu nikakuta kwenye app store ya mwana Msimbazi, aisee hii app hata hakuna malipo na habari zinakuja kwa wakati.