Da Vinci XV
JF-Expert Member
- Dec 7, 2019
- 3,862
- 6,438
Ukizungumzia hii siku basi unazungumzia, siku ya kuwafanyia vibweka watu na vituko mbalimbali.
Huadhimishwa tarehe moja April , kwa kufanya mzaha au kituko chochote mbele ya mtu au kumlaghai juu ya jambo fulani.
Na mtu yoyote atakejisahau hii siku akaingia mkenge basi hugeuzwa kenge wa hii siku na kuingia kundi lile la kuitwa Wajinga.
Pengine nmekuzindua mapema hapa leo ili kesho usije kutana na dhahma bin shari.
Nakumbuka miaka ya utoto nilimshamlizaga Anko wangu 50, kwa masihara ya kumdanganya ngombe wa jirani Anauzwa. Kuna kastori katikati hadi akaingia kwenye nyuzi 360 na kuchomolewa 50k baada ya kugundulika kilichonipata ni Malaika wa Mungu tu Gabriel na wenzie ndiyo walikuwa watetezi wangu
😅😅
Kesho tunaweza kushuhudia mengi
Unaweza kutumegea kisa hapa kama uliwahi kuingizwa mkenge kwenye siku hii na ilikuwa kwa namna ipi?
LAKINI, JE?
What if April fools day was really on April 2nd au siku nyingine yoyote and not April 1st
😅😅
And they've been fooling us the whole time, na hatuelewi kinacholea
INAKUAJE?
Its called April fools Day for Reason!