Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Baraza la seneti la Argentina, limepitisha mswada wa sheria wa kihistoria unaohalalisha uavyaji mimba katika taifa ambalo Kanisa Katoliki limekuwa na ushawishi mkubwa kwa muda mrefu.
Argentina imekuwa miongoni mwa kundi dogo la nchi za Amerika Kusini kuchukua hatua hiyo.
Muswada huo ulipendekezwa na Rais Alberto Fernandez na ulipitishwa katika mabaraza ya chini Desemba 11, licha ya upinzani mkali kutoka katika Kanisa Katoliki na makanisa ya Kievanjelisti.
Serikali ya Argentina inasema kati ya visa 370,000 na 520,000 vya uavyaji mimba kinyume na sheria hurekodiwa nchini humo kila mwaka, katika taifa hilo lenye watu milioni 44.
Miaka miwili iliyopita, muswada kama huo ulipitishwa katika mabunge ya chini, lakini ukaangushwa baadaye katika baraza la seneti.
Muswada huo unawaruhusu wanawake kuavya mimba, hadi muda usiopita wiki 14 tangu kupata ujauzito.
Argentina imekuwa miongoni mwa kundi dogo la nchi za Amerika Kusini kuchukua hatua hiyo.
Muswada huo ulipendekezwa na Rais Alberto Fernandez na ulipitishwa katika mabaraza ya chini Desemba 11, licha ya upinzani mkali kutoka katika Kanisa Katoliki na makanisa ya Kievanjelisti.
Serikali ya Argentina inasema kati ya visa 370,000 na 520,000 vya uavyaji mimba kinyume na sheria hurekodiwa nchini humo kila mwaka, katika taifa hilo lenye watu milioni 44.
Miaka miwili iliyopita, muswada kama huo ulipitishwa katika mabunge ya chini, lakini ukaangushwa baadaye katika baraza la seneti.
Muswada huo unawaruhusu wanawake kuavya mimba, hadi muda usiopita wiki 14 tangu kupata ujauzito.