Arobaini za ATCL zatimia kwa Waziri Kawambwa

Arobaini za ATCL zatimia kwa Waziri Kawambwa

Pdidy

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2007
Posts
57,951
Reaction score
32,619
Orobaini za ATCL zatimia kwa Waziri
Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,January 29, 2009 @21:15



Kamati ya wataalamu iliyopewa kazi ya kuchunguza chanzo cha matatizo ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), imewasilisha ripoti yake serikalini na kutoa mwanya kwa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu kutoa uamuzi kulingana na mapendekezo yaliyomo.

Ingawa haikufahamika mara moja mapendekezo yaliyomo katika ripoti hiyo iliyokabidhiwa jana Dar es Salaam, lakini Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa alisema serikali ilikuwa ikiisubiri kwa hamu ripoti hiyo kwa ajili ya kuyatumia yaliyomo kutolea uamuzi unaolenga kuboresha kampuni hiyo.

“Tulisuburi kwa hamu. Baada ya upembuzi wa kina, kazi yetu ya kuboresha ATCL itakuwa rahisi,” alisema Dk. Kawambwa na kusisitiza kuwa baada ya uchambuzi, watatafakari na kuchukua uamuzi uliopendekezwa ndani ya muda mfupi.

Chini ya uenyekiti wa Profesa Idrissa Mshoro, kamati hiyo ilikuwa ikichunguza kwa kina, kubaini kwa ufasaha matatizo yanayoikabili ATCL na kutoa mapendekezo ya kutatua matatizo hayo. Waziri alisema ana imani mapendekezo yaliyotolewa hayajafungwa na kitu chochote kwa kuwa kamati hiyo siyo ya kichama na wala kiserikali, bali ni ya wataalamu na iliyokuwa huru katika uchunguzi wake.

Alisema kamati hiyo ilipewa muda mfupi wa siku 21 kufanya kazi hiyo kutokana na dharura ya suala lenyewe la kutaka mapendekezo ya kitaalamu ili kuboresha huduma za kampuni hiyo. Timu ilitumia siku 28 badala ya ilizopewa kutokana na kile alichosema Waziri kwamba ni ugumu wa kazi yenyewe.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Mshoro alisema watu 56 kutoka maeneo tofauti walihojiwa. Vile vile wamepitia nyaraka mbalimbali na kuzichambua. Wajumbe wa kamati hiyo ni Dk. Marcellina Chijoriga, Profesa Ibrahim Juma, Mtesigwa Maugo, Dk. Mussa Assad na Dk. Hamisi Kibola. Katika ripoti hiyo iliyokabidhiwa, Profesa Mshoro alikabidhi vitabu viwili; kimoja kikiwa cha ripoti husika na kingine kikihusisha nyaraka mbalimbali walizoona ni muhimu ziendane na ripoti hiyo
 
jamani hii ni habari njema nyingine wenye uwezo wa kupata data zilizopo humo ndani tujulisheni jamani tjaribu kuchangia hoja za ma proffesa wetu
 
Orobaini za ATCL zatimia kwa Waziri
Stella Nyemenohi
Daily News; Thursday,January 29, 2009 @21:15



Kamati ya wataalamu iliyopewa kazi ya kuchunguza chanzo cha matatizo ya Kampuni ya Ndege Tanzania (ATCL), imewasilisha ripoti yake serikalini na kutoa mwanya kwa Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu kutoa uamuzi kulingana na mapendekezo yaliyomo.

Ingawa haikufahamika mara moja mapendekezo yaliyomo katika ripoti hiyo iliyokabidhiwa jana Dar es Salaam, lakini Waziri wa wizara hiyo, Dk. Shukuru Kawambwa alisema serikali ilikuwa ikiisubiri kwa hamu ripoti hiyo kwa ajili ya kuyatumia yaliyomo kutolea uamuzi unaolenga kuboresha kampuni hiyo.

“Tulisuburi kwa hamu. Baada ya upembuzi wa kina, kazi yetu ya kuboresha ATCL itakuwa rahisi,” alisema Dk. Kawambwa na kusisitiza kuwa baada ya uchambuzi, watatafakari na kuchukua uamuzi uliopendekezwa ndani ya muda mfupi.

Chini ya uenyekiti wa Profesa Idrissa Mshoro, kamati hiyo ilikuwa ikichunguza kwa kina, kubaini kwa ufasaha matatizo yanayoikabili ATCL na kutoa mapendekezo ya kutatua matatizo hayo. Waziri alisema ana imani mapendekezo yaliyotolewa hayajafungwa na kitu chochote kwa kuwa kamati hiyo siyo ya kichama na wala kiserikali, bali ni ya wataalamu na iliyokuwa huru katika uchunguzi wake.

Alisema kamati hiyo ilipewa muda mfupi wa siku 21 kufanya kazi hiyo kutokana na dharura ya suala lenyewe la kutaka mapendekezo ya kitaalamu ili kuboresha huduma za kampuni hiyo. Timu ilitumia siku 28 badala ya ilizopewa kutokana na kile alichosema Waziri kwamba ni ugumu wa kazi yenyewe.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Mshoro alisema watu 56 kutoka maeneo tofauti walihojiwa. Vile vile wamepitia nyaraka mbalimbali na kuzichambua. Wajumbe wa kamati hiyo ni Dk. Marcellina Chijoriga, Profesa Ibrahim Juma, Mtesigwa Maugo, Dk. Mussa Assad na Dk. Hamisi Kibola. Katika ripoti hiyo iliyokabidhiwa, Profesa Mshoro alikabidhi vitabu viwili; kimoja kikiwa cha ripoti husika na kingine kikihusisha nyaraka mbalimbali walizoona ni muhimu ziendane na ripoti hiyo

Nimefurahi sana kupata habari hizi njema kuwa ile timu ya wataalam imemaliza kazi na kuikabidhi kwa Mh Waziri. Ni matumaini yangu kuwa ripoti hiyo kama alivyosema Mh Waziri si ya kichama wala serikali basi ataonesha ujasiri wa kuiweka wazi ili wadau wote tuisome na kupata mwelekeo wa pamoja.
 
Kamati ya wataalamu wa Dr. shukuru Kawambwa iliyoongozwa na Prof. Mshoro haitakuja na jingine jipya juu ya masahibu ya kampuni ya ATCL. The injection of adequate working capital is a necessary condition for the rejuvenation of tha ailing Airline but the sufficiency condition is that ATCL should be manned by competent and professional personnel!! Once the necessary and sufficient conditions are met, ATCL will be up and running!! We all know this, we do not have to wait for a task force to tell us about this after spending our millions of hard earned tax payers money. I guess the minister wanted some justification to fire the management and their AMBASSADOR!!
 
Huko zamani niliwahi kusikia kisa cha timu ya wataalamu waliokusanywa na kampuni moja kutafuta jinsi ya kupunguza matumizi ya chumvi ya mezani. Baada ya utafiti wao uliochukua miezi kadhaa na kutumia karibu dola milioni moja timu hiyo ilitoa taarifa yao yenye juzuu tatu.

Pendekezo lao la kwanza na kubwa lilikuwa: KUPUNGUZA MATUNDU YA KWENYE SALT SHAKERS!


well..naweza kusema kilichopendekezwa kwa uhakika wa asilimia 99.9 na sihitaji kufanya utafiti!...... PUNGUZENI MATUNDU YA ATCL SHAKERS!
 
Huko zamani niliwahi kusikia kisa cha timu ya wataalamu waliokusanywa na kampuni moja kutafuta jinsi ya kupunguza matumizi ya chumvi ya mezani. Baada ya utafiti wao uliochukua miezi kadhaa na kutumia karibu dola milioni moja timu hiyo ilitoa taarifa yao yenye juzuu tatu.

Pendekezo lao la kwanza na kubwa lilikuwa: KUPUNGUZA MATUNDU YA KWENYE SALT SHAKERS!


well..naweza kusema kilichopendekezwa kwa uhakika wa asilimia 99.9 na sihitaji kufanya utafiti!...... PUNGUZENI MATUNDU YA ATCL SHAKERS!

Teeh eteh hiii aaahha aaahh mmmh. Wee Mwanakijiji ni balaa sana. Jiandae kwa RB kutoka kituo cha Polisi Magomeni kwa kusababisha mtu kuvunjika mbavu kwa kucheka kutokana na huu ushauri wako. Only watu walio na Ph.F (Si Ph.D) katika masuala ya uchumi wanaweza kukuelewa kaka.
You're really awesome.
 
Back
Top Bottom