JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Goli lililofungwa na Martin Ødegaard dakika ya 2 lilikuwa na baraka ya kuifanya Arsenal kushusha mvua ya Magoli 5-1 dhidi ya Manchester City katika Ligi Kuu ya England "Premier League" kwenye Uwanja wa Emirates
Magoli mengine yamewekwa wavuni na Thomas Partey, Lewis Skelly, Kai Havertz na Ethan Nwari, huku City ikipata goli lake kupitia kwa Erling Haaland. Ikumbukwe mchezo uliopita baina ya timu hizo ulimalizika kwa sare ya 2-2
Arsenal imefikisha pointi 50, nyuma ya Liverpool inayoongoza Ligi, ikiwa na alama 56 huku City imebaki nafasi ya 4 ikiwa na pointi 41.
Magoli mengine yamewekwa wavuni na Thomas Partey, Lewis Skelly, Kai Havertz na Ethan Nwari, huku City ikipata goli lake kupitia kwa Erling Haaland. Ikumbukwe mchezo uliopita baina ya timu hizo ulimalizika kwa sare ya 2-2
Arsenal imefikisha pointi 50, nyuma ya Liverpool inayoongoza Ligi, ikiwa na alama 56 huku City imebaki nafasi ya 4 ikiwa na pointi 41.