ARSENAL BADO WANAKOMAA NA MUDRYK
RASMI: Klabu ya Arsenal imetuma ofa ya pili ya kumsajili nyota wa Shakhtar Mykhaylo Mudryk baada ya ile ya kwanza ya €40m na nyongeza ya €20m kukataliwa.
Kwa mujibu ripoti, Arsenal wametuma ofa ambayo wanaamini itamaliza dili hilo.
Ikumbukwe Shakhtar wanataka kiasi kisichopungua €55m bila kipengele cha nyongeza ya kulipa baadae kama atakuwa kwenye kiwango kikubwa akiwa na Arsenal.
Mazungumzo yanaendelea kati ya klabu zote mbili.