Arsenal katika sakata la kumsajili Suarez

Arsenal katika sakata la kumsajili Suarez

Albinoomweusi

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2016
Posts
3,433
Reaction score
8,585
Suarez alikuwa hafurahii maisha ndani Anfield 2013 na alikuwa anataka kuondoka. Liverpool walimuambia hawana shida, wapo tayari kufanya mazungumzo na klabu yoyote aliyopo tayari kujiunga nayo.

Arsenal wakiwa wametangaza nia kweli ya kumsajili Suarez walituma ofa Liverpool ya kumsajili Suarez. Suarez alikuwa tayari kujiunga na Arsenal.

Arsenal waligundua kwenye mkataba wa Suarez kipo kipengele kinachoitaka klabu inayotaka kumsajili kulipa zaidi paundi 40 milioni. Wakatuma ofa ya paundi 40 milioni kwa Liverpool.

Liverpool wakawarudisha wakiwataka wafike kigezo cha mkataba ambacho kinawataka kulipa zaidi ya paundi 40 milioni.

Arsenal wakarudi, wakaa chini wakajadili halafu wakatuma ofa ya paundi milioni 40+1. Nielewe vizuri, hawakuongeza paundi milioni moja bali paundi moja. Yaani 2500 za kitanzania[emoji3].

Ndipo mmiliki wa Liverpool John Henry, alikasirika na kwenda Twitter kuwadhihaki Arsenal. Kupitia ukurasa wake wa Twitter aliweka picha ya Suarez na kuandika.

“What do you think they’re smoking over there at Emirates?”

Kwa kindereko kisicho rasmi ni kuwa "Unafikiri wanavuta nini huko Emirates?"

Lakini kweli Arsenal walikuwa wanavuta jani la wapi?? Yaani unaambiwa ukaongeze hela ya kumsajili Suarez halafu unaongeza shilingi elfu mbili kweli? Ila haishangazi hawa ni Arsenal[emoji1783].

Msimu mmoja mbele, Barcelona walilipa zaidi ya paundi 70 milioni kumsajili Suarez. Ni karibia mara mbili ya dau waliloliweka Arsenal mwaka mmoja nyuma.
[emoji871]@deo_mwanasoka


images%20(12).jpg
 
Prof. Arsené Wenger aliliweka wazi sababu kubwa ilikuwa NIDHAMU, Suarez alikuwa the best lakini nidhamu ilionekana tishio katika misingi ya soka la Arsenal.

Arsenal siku zote inazingatia nidhamu, hata leo utaona wachezaji wengi wametupwa, kuuzwa au kuwekwa chini sababu ya nidhamu.

Wachambuzi wa soka wengi Tanzania mnaongea na kuandika msioyafahamu bali kurithishana na kusikiliza yanayo trend!
 
Arsenali kama Taifa Stats tu! Sijui wana undugu hawa watu? Wote kuna kipindi wanafanya vizuri, hakafu kuna kipindi wanageuka na kuwa vichwa vya wendawazimu!
 
Ok halafu ameenda Atletico kwa shilingi ngapi?
 
Kwani walikosea kuengeza pound 1? Ambayo ni sawa na buku3 za kibongo, walichosema ndicho walichopewa
 
Back
Top Bottom