Arudisheje hisia kwa mumewe? ...Msaada tafadhali

MwanajamiiOne
I think the best thing for her is to pick a side an stick with it. Since at this point she lost feelings kwa mume and obviously prefers mshefa, akae na mshefa na amuulize how he feels about her leaving the husband for him? Maana hawa side dishes nao wengine wanakupendaga wakati uko kwa mume na si limzigo lao. If he is ok with it, then she can just move on, personally sioni faida and/or point ya kung'ang'ania ndoa while one partner is lusting for someone else!!!
 
ni vyema mwanamke kujua mapungufu ya mumewe ili aweze kumrekebisha na waishi kwa amani vingnevyo kweli huyo bidada atajutia hyo ndoa na mwisho wa ck huyo anaemuita mshefa atasepa!
 
Mara nyingi watu waliopo katika situation kama hizo hua tayari wanajua deep down ni nini anataka.... kuomba ushauri inakua kama tu a way ya kuoanisha ushauri anaopewa na kile anachokitaka... IMO kama huyo dada atathubutu kumuacha mumewe awe na huyo the so called mshefa akiamini ndio atakua na amani as a result of the love in between atachemka...

MJ1 mwambie akumbuke kua huyo mshefa anaonekana ni fun sababu ni stolen kisses and Sex (hio hujenga saana exitement mpaka ile euphoria you feel usipoangalia waweza changanya na mapenzi ya dhati...) Ni mara chache mno mwanaume ambae anatembea na mke wa mtu kutaka kumuoa huyo mwanamke akiachika - for the simple reason kua; anatahisi akiwa nae ka vile atatoka na other guys.... mkuki kwa nguruwe.... Na ukizingatia the hubby has changed for the better... Yaani kweli tell her to choose wisely, na ajiulize kama huyo mshefa mume wa mtu katoka nje, kitu gani kitamzuia kutoka akiwa nae - na ikiwa hivo, why not just stick to the hubby??
 
Kwa kweli ngumu sana, maana nachojua wanawake wengi tunacheat sababu ya kuadhibiwa na mateso ya upweke na waume zetu, ila rohoni huwa mapenzi mazito tunakuwa nayo kwa waume kuliko kule tunapoenda kupata pumziko la muda mfupi, sasa huyu mwenzetu imekuwa tofauti, na moyo ukihama hauwezi urudisha kirahisi,

Ndio pale inabidi atumie nguvu ya ziada, yaani aache kabisa kuonana na huyo jamaa, aanze kutafuta mazuri ya mumewe na kuya enzi, wapange mfumo wa maisha ambao utawafanya wanakuwa pamoja muda mwingi,amwambie mshefa mumewe kamjua na anamfatilia sana, hata ikiwezekana amdanganye amekuta picha zake ii amwogopeshe yule, ndio, si anataka nyumba yake irudi?mie naona hivi sijui wenzangu
 
Mwanajamii one,
mi nafikiri mtu akishatambua tatizo inakuwa rahisi zaidi kukabiliana nalo. kama kweli yuko serious, hamna namna ni kuachana na huyo 'mshefa'. ila pia sio guarantee kwamba mume ndo ametulia jumla...akikumbuka siku moja moja lazima atarudia alikozoea, human nature! well, si nzuri mara nyingine kuomba ushauri wakati mtu unajua unalofanya.
 
uuuuhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh

Kaka Shemeji........this is all that you can say to this thread?? please hebu okoa jahazi................mdada amekiri kuwa kakosea sasa anatamani kurekebisha mambo ila ndo hivyo tena mambo ya hisia /feelings yanagoma ikichangany'wa na manipulation za huyo Mshefa ndo kabisaaaa anabakia kuishi na mume kisanamu!! Hebu toa nasaha zako bwana
 

......Jestina mydia mimi ninaamini kama amefikia hatua ya kutoa hii siri na kuonyeshab dhamira yake ya kuacha ni wazi ameshaona haina tija............. anavyodai ni kuwa huyu ni mumewe na alishawahi kumpenda na wamejenga familia pamoja na ni mumewe wa halali (ndoa). Mshefa ni mume wa mtu na sawa yaliyotokea kati yao yalitokea but anataka sasa ayahitimishe ili arudishe moyo, akili na mapenzi kwa mumewe wa ndoa but ndo hajui afanyeje.......kwa wenzetu wataiita amekuwa addicted sijui but anasema anashindwa hajui aanzie wapi!

duu ndefu hiyooo

Ndetichia we acha tu mie mwenyewe nimebakia mdomo wazi..........sikujua kama mtu ukicheat (hasa kwa wanawake) inakuwa ngumu kucheat kwa akili na si kwa hisia lol.........................

The Boss leo unaguna sana.......vipi umefakamia mihogo bila kunywa maji?lol
Jestina mwache tu kaka shemeji wangu agune maji marefu haya ni haki yake hahahah

Kumbe wanawake nao huwaga wanacheat? Maajabu ya mwaka hayo!

......................Shemeji!! Kuwa hukuwa unajua hilo?? mbona ni kawaida sana?? ulimwengu huu wa usawa umetuletea both pros and cons.
 
Huyo mdada aache ulimbukeni. Mume ni first huyo mshega hana lolote na hatakaa afikie renk ya mume. Ni vizuri amrudie Mungu wake akifanya intensive maombi ya kuachana na huyo laghai asiyekuwa na mshipa wa aibu wala akili.

Wanawake angalie sana, kuna vitu tunafanya end of the day ni majuto. Mwanaume au mwanamke harekebishwi kwa Reveange, ni maombi tu.Poleni wale mnaofikiri kwamba kuna vidumu au ndoo zitazidi waume au wake zenu. Piga ua mtazunguka sana na kuhangaika ila suluhu ya matatizo iko mikononi mwa walengwa yaani MKE au MME.
 

Mwanajamiione, rafiki kama huyu ni kumfukuza kwa herufi kubwa, hata kama angekuwa ni mdogo wako wa damu ana tabia za kijinga kamahizi FUKUZIA MBALI akawatumikie washefa na mashetani wenzie.
 
huyo dada wala asijigangaishe kulazimishia tamanio la penzi kwa mumewe, litakuja tu au jamaa atalipotezea kabisa

Amini nakuambia, mwanaume akishajua umemzunguka, hata kama atakusamehe ujue akili yake imeshapanda treni

she better prepare for both
 

Nakubaliana na wewe 100%. Huyo mwanamke anatakiwa achague moja kati ya mume ama mshefa. Kuendelea kuwa mguu mmoja ndani mmoja nje ni kujidanganya na reality. I'm afraid kama alivyosema AshaDii, huyo mshefa anampenda huyo mwanamke sababu ana mume, believe it or not....the moment akimtamkia mshefa kuwa amemwacha mume wake...guest what?.....mshefa atafreeze na hatomtaka tena. Wanaume ndivyo tulivyo ktk issue kama hizo, tunakuwa na wewe sababu you are a wife of someone else, tunaona raha ya kumwibia mwengine, lakini tukisikia eti umemwacha mumeo ile uwe pamoja na mimi, mapenzi hapo hapo yanayeyuka na ule mvuto unaisha.
Mwambie rafikiyo aachane na mshefa amrudie mumewe then amove on. Ndio maana HIV inatumaliza kwa drama kama hizi!!
 
Mshauri aendelee na Mshefa - Ndoa za siku hizi "nyumba ndogo" na "vidumu" ni muhimu sana!
B_E bwana habari yako bana za miaka? hapana bana huyu bidada ameshaona kuwa hahitaji tension za kutumikia mabwana wawili (afu anadai huyo Mshefa anademand kuliko hata mwenye mali) sasa anataka kuwa 'mtoto' mzuri hebu tumsaidie bana!


VoR huyu mdada kwa mujibu wa maelezo yake ni kuwa ameshafanya analysis na anaelewa kabisa kuwa ni mumewe ambaye anampenda (???- hapa hata mie nilishindwa kumwelewa) ila sasa hisia zake bado ziko kwa Mshefa (Hivi muda wa Infatuation mwisho ni wakati gani??) maana mwanzo nilihisi pengine ana prolonged-infatuation!!
 
neno mshefa naona ni zuri zaidi kuliko buzi lol

Lol la zamani lakini hilo Kaka Shemeji.........Mshefa

Ebana kweli asee....lina sound kihelahela! Buzi linasound kaa jinga flani hivi. What do you think?

Lol Shemeji kuwa unapendekeza uitwe Mshefa eh?? Makubwa

mimi naona bora niitwe mshefa kuliko buzi lol
Mna vituko nyie viumbe wawili....................Haya rudini kwenye mada husika tafadhalini.
 

AD you've hit the nail in the head!
Huyo mshefa anampenda huyo rafikiye Mwanajamii1 sababu ni mke wa mtu. The moment akimwacha mumewe mshefa ataingia mitini.
Huyo mdada anatakiwa aachane na mshefa ASAP na a-stick na mumewe then she has to move on. The problem is the fact that she's in denial. Mwenye kuiba vya watu hatokupenda kwa dhati daima, anakupenda sababu una mwenyewe!
 
story hii imenikumbusha story moja ya majirani zangu wawili. jamaa kaanza kula mke wa jamaa. mume kagundua na kaona ili kupunguza machungu kafanya juu chini akaanza kula mke wa mgoni wake. mgoni alipogundua ikawa haitoshi. lol... mkuki kwa nguruwe!!
 
ndoa hizi dah heri nitafute kiserengeti changu nijisevie wallah

For how long will you stay like this sweetheart??

aliponifufurahisha mj1 ni hapo aliposema hakuamini kuwa mwenzie ana cheat...lol mbavu zangu mimi lol

na hapo aliposema alikiri na kuapa lol duh.....jaribuni stand up comedy jamani lol

Whatever you mean Kaka kusema ukweli kwa umri na status alonayo dada yule sikuwahi kuimagine kama angelipiza kisasi kwa staili hii.

Na hiyo stand up comedy......Do you think I have any reason do cook up things?? what for?!


Lizzy ni habari ya kusikitisha kusema ukweli.......kutokana na kupishana kwetu umri sidhani kama huyu dada anaelewa impact aliyoitengeneza kwenye maisha yangu.............yaani naona hata aibu kumtizama usoni Mr kwani najiona msaliti kwa niaba LOL
 

si kweli,she can keep both of them.............mbona ndoa za mitala wanaume wanaweza kuwa na wake wawili ? wanawezaje?........huyu mshefa yeye hayuko full time kwa sababu ana mke,mie sioni litakalomshinda huyu dada kuwa nao wote wawili mpaka hapo moyo wake utakapochagua kuwa na mmoja.LOL
 
wanawake ni mashetani ninyi... afu mwaji eksipozi wenyewe.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…