Arusha 1977 -1983

Kibunango

Platinum Member
Joined
Aug 29, 2006
Posts
8,468
Reaction score
2,349
Mara ya kwanza kuingia katika mji wa Arusha ilikuwa ni mwaka 1977, nikitokea mji wa Dodoma, kwa njia ya barabara. Safari hiyo ilichukua jumla ya masaa nane. Nilifika Arusha mjini usiku wa saa mbili. Tulipokfika Ngarenaro mji ulikuwa umajaa taa za mafuta, ukimulika giza la mji huu, kupita dirisha la gari niliokuwemo niliweza kuona mizunguko ya watu katika eneo hilo, wengi wao wakiwa ni wanaume. Niliweza kuona biashara kadhaa kando kando ya barabara kati ya hizo ikiwa ni mishikaki.

Hata tulipofika Uhuru road(Sokoine road), Nyumba za mbafu za mbwa zilifika kikomo, hapo niliweza kuona maduka makubwa kabisa, duka la kwanza kulitia machoni lilikuwa ni RTC, pembeni yake kulikuwa na kituo cha mafuta na nyuma yake kulikuwa na kituo cha treni.

Gari lilizidi kusonga mbele, huku nikishangaa mataa barabarani, Uhuru road ilikuwa tofauti sana na mtaa wowote niliowahi ku'uona Dodoma, hadi tulipofika mnara wa saa, nilitamani kurudi tena na kuangalia barabara ya uhuru! Dereva alizungusha gari na kuingia New Arusha Hotel.

New Arusha hotel ilikuwa ni tofauti sana na hoteli za Dodoma, kuanzia majengo yake hadi huduma zake. Hapa nina maana ya Dodoma Hotel, kwani ndio ilikuwa hotel kubwa kabisa wakati huo. Sijui sasa kuna hotel gani kubwa hapo Dodoma. Gari liliposimama wahudumu wawili walikuja kutulaki na kusaidia kubeba mizigo yetu. Kumbuka kuwa sikuwa peke yangu!

Baada ya kukamilisha taratibu za usajili, wahudumu wale walituzogeza kwenye korido, na kubonyeza kitufe kwenye ukuta, mara pakafunguka! wakaingia ndani huku wakituharishia tuwafuate, roho ilisita, macho yakanitoka! Hawa wahudumu wanataka kunipeleka wapi? Wezangu sijui kama walikuwa na mawazo kama yangu, kwani wailingia moja kwa moja kwenye kichumba hiko. Baada ya kufikili kwa sekunde kadhaa nami niliingia. Mlango ukajifunga na mhudumu kabonyeza namba tatu... Sikujua awali kuwa ile ilikuwa ni lift!

Tulikaa hotelini hapo kwa siku saba, nikawa mwenyeji na nikipanda lift zaidi ya mara kumi kwa siku, kiasi cha kuwakera baadhi ya wahudumu wa hoteli.

Makaazi mpya yalikuwa ni katika eneo E, ni eneo la viwanda. Ila eneo hilo lilikuwa linakaliwa na watu wengi ambao walikuwa wakifanya kazi katika jumuiya ya Afrika Mashariki. Sio mtaalamu sana wa mipango miji, ila ndio hivyo, nyumba ziikuwa zimepakana na kiwanda cha bia na kiwanda cha sabuni na peremende.

Hata baada ya siku kadhaa hapo mtaani, nilijua kumbe kuna viwanda vingi zaidi, kama kiwanda cha biskuti, kiwanda cha kiko na kiwanda cha nguo(Kilitex).

Ilikuwa ni shida kubwa kwenda dukani, maduka ya karibu yalikuwa yapo Sinoni, na ni baada ya kuvuka mto Themi(temi), Kuvuka mto huo inakubidi kutumia njia ya treni(reli). Kipindi hiki kilikuwa maarufu kwa mikate ilyojulikana kama kisu, ambayo uliweza kuinunua mzima ama nusu na hata robo yake. Maduka mengine yalikuwa ni Kijenge.

Shule za msingi nazo zilikuwa ni mbali, aidha hazikuwa nyingi hivyo, nakumbuka kuilkuwa na shule ya msingi Naura, Meru na Uhuru aidha na ile ya kiingereza Arusha School. Hizi ndizo zilikuwa za karibu. Kama mwanafunzi ama mwalimu mwendo ulikuwa ni wa miguu!

Zaidi huduma nyingi zilipatikana mjini, na hapakuwepo na daladala ama viford(nasikia siku vimejaa tele). Hivyo kwa mtu wa kawaida iimpasa kutembea kwa miguu kufika mjini. Hata hivyo kulikuwa na njia za mkato(shortcut) nyingi tu.

Burudani hazikuwa haba, Arusha ilikuwa na majumba mawili ya sinema, yakijulikana kama Metropol na Elite.. Metropol lilikuwa maarufu kwa aina ya simena walizokuwa wakionyesha nyingi zikitoka Ulaya na Marekani, aidha za Hong Kong na India, Jumba lao lilikuwa zuri na tofauti sana na lile ya Elite Cinema. Elite waliweza kuwakusanya wanafunzi wengi waliokuwa wakipenda kutoroka shule kwani katika siku za kazi waiweza kufungua jumba lao tokea saa nne asubuhi, huku Metropol wakianza saa kumi na mbili jioni.

Kulikuwa na sehemu za kuogelea kama pale New Arusha Hotel, Mount Meru Hotel na katika shule ya Arusha, aidha bembea za watoto zilikuwepo kuanzia Gymkhana hadi New Arusha Hotel. Viwanja vya gofu vikiwa Gymkhana na Mount Meru hotel.

Pale Sheikh Amir Abeid, tuliweza kushuhudia mashindano mbalimbali, kilichovutia miaka hiyo ni mashindano ya riadha... Yalivutia wengi na hasa vijana. nakumbuka ukiondoa mashindano ya Afrika Mashariki, wanafunzi wengi walikuwa wakicheza hapo na hasa siku za mwisho wa wiki huku washindi wakizawadiwa Zabibu za Dodoma.

Ukizungumzia michezo basi hutowacha kuangalia jinsi shule ya Arusha(Arusha school) na ile ya St Constantine walivyoweza kuwa na aina nyingi sana za michezo. Walikuwa na rugby, Kriket, michezo ya Farasi na hii mingine ya kawaida. Siku ukisikia kuwa katika shule hizo kuna open door kwa michezo, hakuna aliyependa kukosa.

Shule za msingi nazo zilikuwa na vituko kibao, kwa mfano shule ya Naura ilikuwa siku zote ikipigana na shule ya Meru, hata hivyo shule ya Uhuru ndio iliyokuwa na wababe kibao, kuanzia akina babu wa Kale na kundi lake... Hawa waliweza kutawala shule zote za mjini Arusha.

Nchi iliingia vitani, na baada ya vita vya Kagera, pale mtaani palibadilika sana. Watu walikuwa ni wengi mno karibu na milango ya viwanda. Awali nilizoea kuwanona vibarua, lakini sasa hawakuwa tena vibarua, bali ni wafanya magendo.

Huwezi kuamini kuwa bia ilikuwa inatowela kiwandani katika ndoo, na kukabidhiwa kwa wanamagendo. Upande wa kiwanda cha sabuni (EMCO) hizi zilikuwa zikivushwa kwa wingi kupitia kwenye fence ya kiwanda hicho. Lawalawa aka peremende hazikuwa na soko la kimagendo kwani tayali kulikuwa na ubani kwa jina la Big G toka Kenya.

Kwenye kiwanda cha biskuti, hali ilikuwa njema ukiondoa tatizo la watoto kujazana tele kwenye jaa la kiwanda hicho ili tu kupata kuokota biskuti zilizotupwa toka kiwandani hapo. Kwa kipindi hicho tabia hii ya watoto kujazana kwenye jaa la kiwanda na hasa siku za mwisho wa wiki halikuwa likitoa picha yoyote zaidi ya kwamba watoto wanavutiwa zaidi na harufu nzuri ya biskuti. Iwapo kiwanda hiki kama kipo hadi leo basi jaa lao litakuwa ni sehemu ya homeless na street children.

Magendo haya yalikuwa ni ya wazi, tokea viwandani hadi mipakani. Kuanzia mirungi hadi dawa za meno kutoka Kenya. Mji ulichangamka na wengi wakanawili. Arusha ikiwa ni Arusha kwelikweli, kila kitu kikipatikana...

Mwaka 1983 niliondoka katika mji huu, ambapo tayali vita dhidi ya uhujumu uchumi ikiwa imeanza...
 
1990-93
[TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Ulanguzi wa Bia Na Waarusha Kujirusha Na Wakenya[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Kushamiri kwa Machangudoa[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Kuibuka kwa Masugar Mammy[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Sina shaka kipindi hiki kilikuwa maarufu sana kwa bia za magendo toka Kenya. Biashara hii ilifanywa sana na akinadada toka Kenya huku wa Kiarusha wakijivuta kwa mbali, kwani wengi wao hawakuwa na mawazo ya kufanya biashara hiyo zaidi ya kufungua viduka vidogo vidogo.

Kumbuka kuwa katika kipindi hiki Viwanda vya Bia hapa Tz havikuweza kutosheleza mahitaji wa wanywaji, kiasi cha kuweka soko la bia wazi kwa bia za Kenya.

Kabla ya kwenda mbali Arusha zaidi ya kunywa bia, pia walikuwa ni maarufu sana kwa Mbege toka Moshi wacha Gongo toka kwanye Milima inayozunguka Mlima Meru..

Bia ya Kenya ilikuwa ni rahisi kulinganisha na bia toka Arusha(Arusha Breweries ama toka depot ya Moshi au kutoka Dar). Na uzuri wake ilipatikana mitaani, na sio katika sehemu maalumu kama kwenye bars na hotels.

Guest House za Mjini zilijaa wanawake wa Kenya na bia zao! Hapakuwa na haja ya kupoteza sh 250 kwa bia ya Tz wakati ya Kenya unaweza kupata kwa sh 150 hadi chini ya hapo kutegemea mdomo wako, tena kwenye street ama Guest house. Nakumbuka siku moja wakati Watz walipoandaa Challenge Cup, walikuwa na timu mbili, moja Taifa Stars iliyocheza Dar na Kilimanjaro iliyocheza Arusha.

Sheikh Amir Abeid iligeuka kuwa mini bar, kwani wadada wa Kenya waliweza kuingia na makreti ya bia uwanjani na kuuza bia kama njugu. Hii ilikuwa Arusha!

Napata wakati mgumu kuangalia ni kwa namna gani uchangudao ulivyoweza kuibuka kwa kasi kubwa mjini Arusha, tofauti sana na Dar es Salaam ama Zanzibar. Ukiangalia Arusha ni mji wa kitalii, hivyo nilitegemea kuwa machangu watakuwa wakivutiwa sana na watalii zaidi ya watu wa kawaida, kama ilivyo kwa machangu wa kawaida wa DSM.

Hebu angalia Zanzibar ya miaka hiyo, Uchangu ulikuwa ni kuwinda watalii, raia wa kawaida hakuwa na nafasi yoyote mbele ya Machungudoa na hasa waliotoka Bara. Hii ilikuwa ni tofauti sana kwa kinadada hawa ambao hawakuweza kuweka vigezo vyovyote kwa wateja wao. Pengine ni kutokana na madini yanayopatika Arusha, ama tabia tu ya watu wa Arusha.

Machangudoa waliweza kupatikana kuanzia saa kumi jioni, hii ni tofauti sana na miji mikubwa mingi ya Tanzania, hadi kufikia saa nne usiku mitaa ya Goliodoi(kama nakumbuka vizuri) illikuwa imejaa Machangu wa aina zote. Kulikuwa na bendi ya muziki wa dansi pale Ikweta Hoteli, ambayo ilitokea DSM, wao walikuwa wanapiga muziki wao kuanzia saa tisa alasiri hadi saa nne usiku. Kwa wale wakware hii ilikuwa ni eneo lao kuu!

Ukishindwa kupatana na Changu kwenye mitaa hiyo, haina maana kuwa siku imeisha, kwani kuanzia saa tano usiku wengi wao walikuwa wakijibana pale Arusha By Night. Hawa kidogo walikuwa ni mwenye gharama nyingi, kuanzia kununua bia na mazagazaga mengine.

Au ilikuwa unaweza kwenda Cave Disco, hapa machangu wake walikuwa ni makini na wa mataifa mengi kama vile waliohusu Somalia na hawa Wakimbizi wa Burundi na waliotokea kwenye makambi ya Tabora... Tabia yao moja kubwa ni ujeuri... Aidha katika disco hili kulikuwepo na uwezekanao wa kupata kitu cha kiaarusha chenye elements za kichangu wengi wao wakiwa chini ya miaka 20

Arusha imejaliwa, kuna mabenk na makampuni kadha wa kadha. Kuna maajenti wa mashirika ya ndege na wengi wao wakiwa ni kinamama.. Hawa waliweza kujipenyeza vizuri kwa wasomi, wa Arusha Tech na wale wa Ilboru High school. Wakiwa wakitafuta vijana wadogo wenye nguvu zao sina la ziada zaidi ya kuwaita masugar mami. Mitindo yao ilikuwa tofauti, walipendelea sana kuanza kujikusanya kwenye vigrocery vilivyopo karibu na target zao. Kama kawaida wanafunzi wengi hawana uwezo kwa kutoka out every weekends, hivyo waliweza kuwapata vijana wengi kupitia vipato vyao. Klabu kubwa ya kukutana na aina hii ya kina mama ilikuwa pale opposite na Library ya Arusha, nyama choma kwa wingi na muziki mkubwa wa dansi. Maisha yakiwa matamu na hii ndio ilikuwa Arusha!
 
Mkuu safi kwa kutupa habari tusiojua na kuwakubusha wengine..., nimependa hii historia unayoitoa kwa angle ya wewe ulivyouona mji..., endelea mkuu wasomaji tupo kwahio it means ulikuwepo tuko 77 - 83 na kurudi 90 - 93 nadhani wengine wanaweza kujazia wewe ulipoachia tupate picha kamili..

Ila nimependa hio ya kina dada wajasiriamali kutoa full huduma inclusive ulanguzi wa bia na mambo mengine
 
Naam Arusaa ya 90s! nilipita hapo June 1990 kuelekea bara(loliondo bus service), nikarudi Arusa 94 kutokea Dodoma via kondoa (Sahib Bus Service) nilikaa Ngarenero, vijiwe cha kona ya NBI, naziona nyumba za mbavi za mbwa majengo na ukanda kuelekea mashamba ya kahawa sombetini, dei waka za Burka estate , nyam choma ya moshi hoteli, fresh mbege ya kwa mrefuu, inashukaa toka jikoni moshi! Ubaridi wa asbh costa za moshi -arusaa na ( video coach) muziki ya Aurus Mabele, Pepekale, Victoria group,mikate ya Arusaa! jamani Arusa ninakuja tena, napata mzuka km ule wa Lerionka (Is it Possible?H .R.Ole Kulet)
 
Mkuu kipindi hicho kukaa New Arusha Hotel ilikuwa kiasi gani
 
Mkuu kipindi hicho kukaa New Arusha Hotel ilikuwa kiasi gani
Sikumbuki vizuri, kwani ilikuwa ni issue ya kifamilia! Hata hivyo kuna uwezekana wa kuwa ni chini ya sh 100 kwa siku.

Niliwahi kusafiri kwenda dar miaka hiyo hiyo kwa nauli ya sh 70 na baadae kwa nauli ya sh 125 luxury bus( KAMATA)

Wakati mwaka 91 nilipanda Tawafiq kwenda dar kwa sh 3500(bei ya ulanguzi)
 
Naam Arusaa ya 90s! nilipita hapo June 1990 kuelekea bara(loliondo bus service), nikarudi Arusa 94 kutokea Dodoma via kondoa (Sahib Bus Service) nilikaa Ngarenero,)
Hakuna mtaa uliowahi kutisha katika historia ya Arusha kama Ngarenaro... Kila aina ya maisha ilipatikana hapo, kwa mfano unaweza kuibiwa mitaa ya Haile Selasi na watu wakuambia nenda kujadili issue yako Ngeranaro. Na ukiwa makini unapata ulichoibiwa... Hii ilikuwa kwenye miaka hiyo ya 80, sijui sasa kuko vipi...


Kambi ya Fisi ulifika?
 
Yap, Kamanda nilikuwepo miaka hiyo katika mji huo na baadae kidogo mwaka 94 kwa miezi kadhaa... Ama hakika bado naupenda sana!
 
Mwaka 1977 kulikuwa na lift Atown? Nilikuwa Arusha 1983 makazi yetu yalikuwa yamepakana na hifadhi ya wanyama sikumbuki ni wapi ila kuna siku walipita pundamilia mother akutuchukua fasta na kutufungia ndani tukawa tunawaangalia kwa nje kupitia uwazi wa mlango.
 
Mwaka 1977 kulikuwa na lift Atown? .
Yap, ilikuwepo na inawezkana kuwa ilikuwepo kabla ya mwaka huo... mbali na New Arusha Hotel, kulikuwa na Safari Hotel ambayo kipindi hiko ilikuwa na maarufu maradufu ya New Arusha Hotel, kwani ilipata kuonekana kwenye silver screen ya hollywood
 
Yap, ilikuwepo na inawezkana kuwa ilikuwepo kabla ya mwaka huo... mbali na New Arusha Hotel, kulikuwa na Safari Hotel ambayo kipindi hiko ilikuwa na maarufu maradufu ya New Arusha Hotel, kwani ilipata kuonekana kwenye silver screen ya hollywood
Naam. Mwaka 1962 mwigizaji maarufu wa Hollywood John Wayne ali shoot sinema maarufu ya HATARI mjini Arusha na scenes zili cover New Safari Hotel, Clock Tower, Mt Meru hospital na baadae nje ya Arusha maeneo ya Ngarenanyuki, Momella, Ngurdoto na kisha Lake Manyara.
 
Longido Primary School - 1981-83

[TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Shule ya Bweni[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Shule maalumu kwa vipofu wa Arusha[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD]*[/TD]
[TD]Shule MchanganyikoWanaume na Wanawake)[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


Baada ya kusoma Naura Primary school kwa miaka kadhaa, nilihamishiwa shule ya Longido ambayo miaka hiyo ilikuwa katika Wilaya ya Monduli na Mbunge wetu akiwa ni Marehemu Sokoine. Hii iikuwa ni shule ya bweni tokea darasa la kwanza hadi la saba, ikiwa ni ya mchanganyiko kati ya wavulana na wasichana pamoja na idadi kubwa ya vipofu ambao walitoka kona mbalimbali za Arusha.

Ukiondoa vipofu, shule hii ilikuwa na idadi kubwa ya Wamasai, kiasi cha kujenga matabaka matatu makubwa shuleni hapo, yakiwa ni Wamasai, Waswahili(Wanafunzi wote wasiohusu Umasai na Walemavu wa macho). Ilikuwepo shule pacha na hii sehemu nyingine wilayani Monduli ila nimesahau jina lake, aidha Longido ilikuwa maarufu zaidi kwani kulikuwa na wanafunzi toka hadi Zambia, wa wale wa Dar es Salaam.

Shule ilikuwa na mabweni zaidi ya saba, matatu yakiwa ya wasichana na manne ya wanaume, wote tulichanganyikana humu pasipo kujali upo darasa la ngapi ama umri wako. Waalimu wote walikuwa na nyumba zao zilizozunguka upande mkubwa wa shue hii. Longido pamoja na kuwa ni kituo cha pili toka mpakani Namanga(Kenya na Tanzania)haikuwa na umeme kipindi hicho. Kijiji cha Londigo kilikuwa na kituo kikubwa cha Polisi na Dispensari kubwa, kwani kwa wakati huo ilikuwa katika hadhi ya Tarafa, hivyo Kata kadhaa zikileta wagonjwa wake Tarafani.

Palikuwepo na Kanisa la Kirutheli, na msikiti mdogo, aidha wenye maduka kipindi hicho walikuwa ni Waabeshi toka Ethiopia na Wasomali wachache sana. Matajiri waliokuwa na sauti huku maduka yao yakiwa yamenona ni hao Waabeshi. Palikuwepo na mnada mkubwa ng'ombe kila Jumamosi. Na ni wakati huu pekee ambao unaweza kufaidi jeuri za Mamorani wa Kimasai.

Ukiondoa Migahawa mitatu, palikuwepo na maduka kadhaa na moja la ushirika wa kijiji, aidha migahawa mingi ilitumika kuuza pombe za kienyeji vilevile. Tarafa hii pia ilikuwa na uwanja wa mpira wa miguu na netibali.

Shule ya Londigo wengi walipenda kuuita kama ni shule ya watukutu, ila mpaka leo napingana na dhana hii, kwani uwezi kusema kuwa walemavu wa macho ni watukutu! ama Wamasai ambao walitoka mbali kuja kupata elimu hapo.

Shule ilikuwa ni ya serikali, hivyo ilikuwa ni bure, ukiacha ule mchango wa sh. 20 ya UPE. Siku ya kwanza ukifika shuleni hapo, unapewa kitanda chako, shuka na blangeti na uniform pair mbili. Hata hivyo mpango wa uniform za bure ulikoma mwaka huo huo nilipojiunga... kiasi nijione nina nuksi.

Mwalimu Mkuu akijulikana kama Mrs Tarimo, ingawa sikuwahi kumwona Mr Tarimo hadi siku nilipoondoka kwenye shule hiyo. Zaidi ya kukupokea yeye ndie aliyekuwa akishika pocket money ya wanafunzi wa shule hii. Na utaratibu wake ulikuwa kama hivi, pocket money money yako unaweza kuitumia siku ya Jumamosi tu! Hivyo kila Jumamosi kulikuwa na kundi kubwa la wanafunzi nyumbani kwake. Kima cha chini kutoa kilikuwa ni sh 5. ana cha juu ni sh,10. Jii iliweza kukusaidia kubadilisha aina ya chakula na kununua pipi na big g. Chakula kikubwa nje ya shule ni chapaiti na supu ya ng'ombe.

Kwenye mabweni ilikuwa ni maisha mengine tofauti sana, kulikuwepo na kila aina ya inywanyasaji. Kwa mfano mwanafunzi wa kiume wa kimasai ambaye bado kuwa morani, aliweza kutembea na vijana wadogo kwake zaidi ya wawili... baadae sana ndipo nilipojua kuwa huu ulikuwa ni tabia ya kishoga. Waathirika wa kadhia hii ni wengi sana!

Maisha ya kila siku shuleni hapo yalikuwa ni magumu sana! Kwa mfano mara tatu kwa wiki lazima kwenda maporini kutafuta kuni, hii ilikuwa ni lazima. Viranja walikuwa na uwezo wa kuchapa viboko wanafunzi wengine. Kuamka ni asubuhi ya saa kumi na moja. Ni vipofu tu ambao hawakupata uzumbufu huu.

Maisha ya kwenda kua chapati na supu yalibadilika baada kuwepo kwa wanafunzi wengi toka nje ya umasai na baada ya Mrs Tarimo kupoteza umaarufu wake wa kutunza pesa ama kuja kwa waalimu toka UPE. Hapa milango ya kufanya biashara na Kenya ilifunguka.

Badala ya kupoteza sh.10 kila Jumamosi, kwa chapati, wanafunzi wengi waliamua kwenda Namanga na kunua vitu adimu kwa upande wa Tanzania. Ulikuwa ni wakati pekee kufanya magendo pasipo bughuza za polisi.
 
Dah ....First and Last pale karibia na stendi kuu ya mabasi palikuwa centre ya kinywaji kwa wazee wa zamani....nilikula chips mayai kwa mara ya kwanza pale nikitoka kucheki mechi ya Ndovu FC na Pamba ya Mwanza nikiwa na marehemu Mzee wangu....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…