Mzee Rufiji
JF-Expert Member
- Aug 24, 2024
- 261
- 395
ASANTE SANA KARIAKOO!
NINGEKUWA kwenye jengo lililoporomoka. Sina matumaini ya kuokolewa. Nini ningefanya? Simu yangu ingekuwa na charge, network ipo sawa, ningeandika ujumbe gani kwa familia? Ningepost nini mtandaoni jamii isome?
Moyo mzito kuwafikiria waliowapoteza ndugu zao waliowapenda. Waliagana asubuhi kwa bashasha na matumaini ya msako wa riziki na manunuzi. Kumbe ni ile siku isiyobashiriwa.
Namfikiria mwenye jengo. Namfikiria Shetani. Bila tetemeko la ardhi wala kimbunga. Jengo limemwagika. Ujenzi chini ya kiwango? Ghorofa kwa bei chee? Walisema wahenga, tamaa mbele, mauti nyuma.
Nasoma ujumbe na kusikiliza sauti za waathirika waliokwama handakini. Najaribu kumwelewa Mungu. Shetani ametoa adhabu. Mungu anatoa fundisho.
Nawatazama vijana shupavu waliojitoa kuokoa wenzao waliokwama. Nauona Utanzania. Saa 40 na mshale unaendelea, haijawezekana kuwafikia waliokwama handakini. Unadhihirika udhaifu wetu.
Utajiri wa mbwembwe. Ufahari na maonesha kusaka mitaji ya kisiasa. Mipango ya bajeti ya kila mwaka. Kariakoo imethibitisha kama nchi hatujawahi kuwa tayari kukabiliana na ajali.
Soma Pia: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa
Nazungumza na nafsi yangu. Mimi kama baba, naweza kusafiri nikaacha wanangu wanaangamia ajalini? Niseme safari ilishapangwa, kwa hiyo siwezi kuahirisha. Nitoe maagizo kwa wadogo zangu: “Walioumia watibiwe, waliopoteza maisha wazikwe.”
Ni baba gani mimi? Nisafiri kutafuta fedha kwa ajili ya watoto ninaowaacha wanakufa? Ni swali kwangu, ningekuwa Rais wa Tanzania, ningeridhika kwenda Brazil kwenye mkutano wa G20, nikiwaacha Watanzania wakipoteza maisha Kariakoo?
Lengo namba moja la urais wangu ni nini? Bila shaka maisha ya Watanzania ndiyo kipaumbele. Kama ndivyo, nawezaje kukwea ndege nikiacha Watanzania wameangukiwa na ghorofa Kariakoo, makumi kwa makumi wakiwa hawajui hatima yao?
Rais kama mfariji mkuu wa nchi. Tangazo likitoka kuwa nimeahirisha ziara nje ya nchi kwa sababu ya ghorofa kuanguka Kariakoo, ili nibaki nikihakikisha nahimiza uokoaji na kupokea ripoti za mara kwa mara, tena hatua kwa hatua, ni kiasi gani nyoyo za wananchi zitafarijika?
Tuwatakie safari jema ndugu waliokatishwa uhai wao. Tuwaombee afua waliojeruhiwa. Tuwaweke kwenye maombi waliopoteza mali. Kariakoo kitovu cha uchumi, ndiyo kitovu cha ujenzi holela. Mamlaka husubiri maafa kuchukua hatua. Asante sana Kariakoo.
©Luqman MALOTO
NINGEKUWA kwenye jengo lililoporomoka. Sina matumaini ya kuokolewa. Nini ningefanya? Simu yangu ingekuwa na charge, network ipo sawa, ningeandika ujumbe gani kwa familia? Ningepost nini mtandaoni jamii isome?
Moyo mzito kuwafikiria waliowapoteza ndugu zao waliowapenda. Waliagana asubuhi kwa bashasha na matumaini ya msako wa riziki na manunuzi. Kumbe ni ile siku isiyobashiriwa.
Namfikiria mwenye jengo. Namfikiria Shetani. Bila tetemeko la ardhi wala kimbunga. Jengo limemwagika. Ujenzi chini ya kiwango? Ghorofa kwa bei chee? Walisema wahenga, tamaa mbele, mauti nyuma.
Nasoma ujumbe na kusikiliza sauti za waathirika waliokwama handakini. Najaribu kumwelewa Mungu. Shetani ametoa adhabu. Mungu anatoa fundisho.
Nawatazama vijana shupavu waliojitoa kuokoa wenzao waliokwama. Nauona Utanzania. Saa 40 na mshale unaendelea, haijawezekana kuwafikia waliokwama handakini. Unadhihirika udhaifu wetu.
Utajiri wa mbwembwe. Ufahari na maonesha kusaka mitaji ya kisiasa. Mipango ya bajeti ya kila mwaka. Kariakoo imethibitisha kama nchi hatujawahi kuwa tayari kukabiliana na ajali.
Soma Pia: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa
Nazungumza na nafsi yangu. Mimi kama baba, naweza kusafiri nikaacha wanangu wanaangamia ajalini? Niseme safari ilishapangwa, kwa hiyo siwezi kuahirisha. Nitoe maagizo kwa wadogo zangu: “Walioumia watibiwe, waliopoteza maisha wazikwe.”
Ni baba gani mimi? Nisafiri kutafuta fedha kwa ajili ya watoto ninaowaacha wanakufa? Ni swali kwangu, ningekuwa Rais wa Tanzania, ningeridhika kwenda Brazil kwenye mkutano wa G20, nikiwaacha Watanzania wakipoteza maisha Kariakoo?
Lengo namba moja la urais wangu ni nini? Bila shaka maisha ya Watanzania ndiyo kipaumbele. Kama ndivyo, nawezaje kukwea ndege nikiacha Watanzania wameangukiwa na ghorofa Kariakoo, makumi kwa makumi wakiwa hawajui hatima yao?
Rais kama mfariji mkuu wa nchi. Tangazo likitoka kuwa nimeahirisha ziara nje ya nchi kwa sababu ya ghorofa kuanguka Kariakoo, ili nibaki nikihakikisha nahimiza uokoaji na kupokea ripoti za mara kwa mara, tena hatua kwa hatua, ni kiasi gani nyoyo za wananchi zitafarijika?
Tuwatakie safari jema ndugu waliokatishwa uhai wao. Tuwaombee afua waliojeruhiwa. Tuwaweke kwenye maombi waliopoteza mali. Kariakoo kitovu cha uchumi, ndiyo kitovu cha ujenzi holela. Mamlaka husubiri maafa kuchukua hatua. Asante sana Kariakoo.
©Luqman MALOTO