Asante serikali kwa ajira, ila wanajua kutunyoosha!

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Kama mtu huna ajira ni afadhali utafute tu namna ya kujiajiri.

Ajira za serikali zina changamoto zake nyingi!

Fikiria mtu anaajiriwa kwa mshahara wa laki 4 kwa mwezi.

Kama haitoshi mtu huyu ananyimwa nyongeza ya mshahara kwa kigezo cha ajira mpya ilihali gharama za maisha ziko juu kwa wote.
 
Hujasoma sheria inasemaje?
 
Acha kazi,Mimi nimeanza ajira napokea 460,000 basic,take home 380,000, milisavavu hadi muda huu niko kwa 790,000 basic,take home 500,000+,can you imagine!?,bado mikopo,ukiweka na mikopo nabaki na 263,000 ila maisha yanasonga,maana nakula na nimejenga nyumba,

Siwezi kulalamika maana sijafungwa namba ninao uwezo wa kuacha kazi Mara moja nikitaka
 
Ajira mpya utapewaje nyongeza, subiri mwakani au hujui maana ya "annual increment"?
 
KATAA AJIRA, AJIRA NI UTAPELI
 
Hiyo sio Nyongeza ya Mshahara ni anual increment sasa wewe upewe anual increament wakat upo kwenye probation hebu subiri kwanza usote upate comfirmation letter angalau utambulike kama mtumishi wa umma sasa hivi bado upo kwenye vetting
 
Umesema ajira mpya.?.. Tena shukuru Samia kaongeza hao wa laki nne mwaka juzi walikuwa na laki tatu....
 
Duh ni Ticha wa Primary?
 
Safi sana ndugu ..pambana ununue na kausafiri kadogo
 
Daaa laki tano, unaona kubwa, hiyo ni hela ya posho kwa watu fulani
 
Elimu Yako ndogo sana ungekuwa engineer kwa sasa ungekuwa unalipwa 1,500,000/-
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…