Asha Mkwizu Hauli-Na kesi ya kumuua hawara wa mumewe

Huyu hawala nadhani alikuwa pumbuani. Wewe unamshitaki mtu anatishia maisha yako, na pia unamchukulia mme, alafu unafuatana naye nyumbani kwake kupata vinywaji. Huogopi hata anaweza kukuwekea sumu. Huyu alipumbazwa na nini au alijiaminia nini? Tena anamtukania nyumbani kwake mama wa watu (kama ni kweli), pamoja sishabikii kifo, lakini hiki kifo alikikaribisha mwenyewe.
 
Ahsante mwalimu,

Nimekoma kusikiliza hadithi za mitaani.... Khaa! Mwinyi alikuwa hataki masihara eh? Miaka 10 watu 72? Na shujaa wangu naye alikuwa muuaji kumbe?... Kazi ya urais ni ngumu sana aisee....!
Pima thamani ya maisha na imani! wewe unaweza kujilipua! Je, unaamini kuua kafir ni sawa? Baadaye, njoo na majibu!
 
mkuu huyo uliyemgusa sasa ni kipenzi cha watu hapa jf, hata akitoa ushuzi kwenye kikao wafuasi wake hao watasema hakujamba, bali mwili wake automatically unatoa 'natural perfume' jiandae na mashambulizi dhidi yako mkuu kwani watakuja punde tu.
Ile ya Josephine na Slaa, mme wa Josephine aliishadharau na kuendelea na maisha yake. Ila, CCM kwa sababu za kisiasa ndiyo wakaianzisha. Lakini hata hivyo hawakufika mbali. Sisi wanaume, mwanamke akishatembea nje, kinachofuata ni kumuacha siyo kumng'ang'ania. Mwanaume utamng'ang'ania mwanamke ili iweje, hasa akishatamka hakutaki. Pia, kumbuka katika ndoa nyingi za kwetu, mara nyingi ndoa ikivunjika mwanamke ndiyo anapoteza, na mara chache mwanamke anaenda pazuri zaidi kuliko alipotoka, hii ndiyo maana wanaume hudharau na kutafuta mwingie! Lakini mwanamke, kwa mfano, tayari kakongoroka, atampata wapi wa kumliwaza! NDIYO MAANA HUCHUKUWA MAAMUZI MAGUMU!
 
.......Hii story ndio kwanza nasikia leo, ila Asha alifanya kosa kubwa la kumuua Happyness.
Angeamua kudeal na mumewe na sio kumfupishia maisha mwezie. Ukisikia mwanamke ana roho mbaya/mkatili ndio kama huyo Asha.
Kwa macho yako wewe kama mwanamke. Lakini kwa macho yake, yeye alioona amshughulikie mwanamke. Faida ya kumshughulikia mwanamke, bado mme wake angebaki na alibaki akiwatunza watoto. Lakini angeemua baba watoto, hasara ingekuwa kubwa maana kipato cha baba kilikuwa kinategemewa mno.
 
Mkuu naomba uweke na case ya mwalimu Peter muhozi vs AG na ya hamisi and six other vs AG ipo kwenye kitabu cha administrative law by chipet na kama unacho naomba unipe
Huo sasa uvivu. Mnapenda saana vya kupewa/bure. Wewe unajuwa unachokitaka kinapatikana wapi, lakini unataka mwingine ahangaike kukutafutia. Kwa njia hii kweli tutaendelea!
 
Gudume Happyness ndio alimpeleka mke halali wa Dr Hauli polisi hapo ndio ujue alikuwa hazimtoshi
Sifa kubwa ya Mpare ni kesi. Ndiyo maana unaambiwa Mpare akiibiwa kuku, atauza ng'ombe apate pesa ya kuendeshea kesi ya kuibiwa kuku. UPOOOOO! Hilo kabila liko "addicted" na mashitaka au kushitaki!
 
JF ilipokuwa JF
 
Kumbe hata miaka hio ya 80 kulikua na mambo hayo!
Alimwambia kwa kipare cheimie ni kuthotholwa vigingi he mdhuti
Maana yake kilichobaki ni wewe kuingizwa vijiti mku????****ni
Hii ni dharau kubwa mno unachukua mume wa mtu na bado ukamfuata mwenye mali hadi nyumbani
na huko nyumbani unakwena kumtukana
Ningekuwa judge nisingemhukumu kunyongwa
Marehemu alijitengenezea mazingira mwenyewe ya kuuawa
Si ungi mno mauaji lakini kuna mazingira mtu anayaleta mwenyewe
nikupe mfano mzuri sana aje jamaa wa kiume nyumbani kwako mbele ya watoto wako amvue mkeo nguo kwa nguvu ambake kisha achukue binti yako afanye hivyo na wewe una silaha huyu mtu anastahili nini????
Hakiamungu tutaugombea mlango mimi wa magereza wewe mortuary halafu nikinyongwa mungu mwenyewe atapima mwenye haki.
Aliyempa msamaha nina uhakika alizama sana ndani na kufikiria mazingira mungu ambariki
Marehemu naye mwana kulitafuta mwana kulipata.Mungu amgeuze kuni za kuchomea wenzake.Na huyu muuaji MUNGU ampe shifwaa njema ampunguzie makosa yake ikiwezekana aingie peponi dawa ya jino ni jino
 
Kwa kiasi kikubwa wa kulaumiwa ni marehemu, ingawa hata mtuhumiwa hakosi lawama lakini kwa hatua ile mtu yoyote angeweza kufanya chochote hata huyo hakimu .
 
Imenibidi nije kusoma hii kesi baada ya Beatrice kumuua Msele.
 
Rip mtambuzi
 
Haya mambo kumbe yalishaanza kutokea miaka ya zamani. Kabla ya hii mitandao kwa hiyo kufuatilia hii kesi miaka hiyo ilikuwa ni mpaka redio au magazeti
Hakuna jipya chini ya jua.Kuna kesi nyingine humu Mke wa jaji Liundi.Ambae ni mama wa Taji Liundi aliwapa wanae sumu na yeye akanywa kisa manyanyaso kutoka kwa Mmewe. Watoto walikufa na Taji pekee ndo alipona na huyo mama alipona pia.Nadhani aliitwa Doris Agnes Liundi.
 
Sawa kabisa mhenga alikuwa anaitwa Doris Agnes Liundi mimi na Taj wakati huo tulikuwa primary school.Huyu mama alikuwa anasoma chuo cha ualimu Kigurunyembe sasa alivyokuwa chuo kuna mwanafunzi mwenzake alimbaka bahati mbaya akamuambukiza ugonjwa wa zinaa akaja kumuambukiza mumewe.
Manyanyaso yalianzia hapo.Akaanza kukumbuka yeye ni yatima akaona watoto wake wakibaki watanyanyasika akaona aondoke nao.
Nyerere hii ilimgusa sana alivyoletewa a sign kunyongwa akatamka siwezi ku m frustrate mtumishi wange Christopher Liundi yule mama alikaa jela ila hadi sasa sina uhakika yuko wapi mjuzi atuambie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…