Asilimia 48.3 ya wanaume tanzania wamebambikiwa watoto na wake zao

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
[h=3]ASILIMIA 48.3 YA WANAUME TANZANIA WAMEBAMBIKIWA WATOTO NA WAKE ZAO[/h]


Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali nchini imesema karibu nusu ya watu waliojitokeza kupima

vinasaba (DNA) ili kubaini uhalali wa watoto wao, vipimo vimeonesha si wazazi halisi wa watoto

waliopimwa.


Takwimu hizo ni kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2010, ikionesha kuwa, asilimia


48.32 ya wazazi 'wanalea' watoto wasio wa kwao wakati asilimia 51.68 ndio wazazi halali.

Hayo yameelezwa jana na Mkuu wa Kitengo cha Makosa ya Jinai, Vinasaba na Baiolojia wa ofisi

hiyo, Gloria Machuve katika mkutano na wanahabari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari

(MAELEZO), Dar es Salaam.

Ingawa hakutaja idadi kamili ya waliojitokeza kupima DNA, alisema idadi hutofautiana mwaka hadi

mwaka. Ili kufanya vipimo vya DNA, wazazi hulazimika kulipia Sh 100,000.


Machuve alisema kazi ya DNA si kutambua watoto halali na wasio halali pekee, bali vipimo hivyo

vina umuhimu mkubwa kwa jamii.


Alitoa mfano kuwa, matumizi ya Teknolojia ya vinasaba vya binadamu yamewezesha kesi mbili za

mauaji ya vikongwe na albino kutolewa hukumu katika mikoa ya Shinyanga, Kagera na

Sumbawanga baada ya kufanyika kwa uchunguzi katika matukio manane.


Aidha, alisema katika majanga mbalimbali yaliyokumba nchi ikiwa pamoja na milipuko ya

mabomu yaliyotokea Mbagala, Dar es Salaam mwaka 2010 walitambua mabaki ya askari sita

ambao baadaye walichukuliwa na ndugu zao na kuzikwa.


Alitolea pia mfano wa tukio la moto katika Shule ya wasichana ya Idodi mkoani Iringa ambako licha

ya kuungua vibaya, miili ya wanafunzi 12 ilitambuliwa hivyo makaburi yao kutambuliwa. Katika

Jengo la ghorofa lililoporomoka mtaa wa Kisutu mwaka huu, marehemu 23 walitambulika.


Aidha, katika ajali ya Ndege ya Comoro mwaka 2010 mabaki ya miili ya marehemu 25 ilitambuliwa

huku katika masuala ya uhamiaji teknolojia hiyo ilitumika kudhihirisha hawana uhusiano na

wananchi wa Tanzania.


Machuve alisema katika masuala ya ubakaji na mimba za utotoni teknolojia hiyo imesaidia kuwa

fikisha wahusika mahakamani pamoja na katika wizi wa kutumia silaha.



ASILIMIA 48.3 YA WANAUME TANZANIA WAMEBAMBIKIWA WATOTO NA WAKE ZAO - MPEKUZI HURU
 
Hapa sina tena na wasiwasi kwani nilishapima DNA watoto wangu wote watatu bila ya mke wangu kujuwa. Kwa sasa naishi kwa amani na furaha tele moyoni.
Mkuu Mkereketwa_Huyu Kati ya hao watoto wako 3 ungeligunduwa mmoja wapo sio Mwanao ungelifanyaje? Wakati kitanda cha ndoa hakizai mtoto wa nje ya ndoa?
 
Mkuu Mkereketwa_Huyu Kati ya hao watoto wako 3 ungeligunduwa mmoja wapo sio Mwanao ungelifanyaje? Wakati kitanda cha ndoa hakizai mtoto wa nje ya ndoa?

Nitamuuliza mke wangu maswali ya kumbana juu ya uhalali wa huyo mtoto kuwa wangu na kwa vyovyote vile atajigonga tu ama kuwa na wasiwasi. Kama sitopata jibu sahihu juu ya uhalali wa huyo mtoto then nitamwambia ukweli. Kinachofuata ni talaka na nabaki na watoto wangu hao wawili. Kwa mwanamke mpaka kuhamua kuzaa na njemba wa nje huku akiwa kwenye ndoa ya uhalali na mumewe, basi ujuwe huyo alishakuona mjinga kwa sababu kama ni suala la kufanya ngono tu na mwanamme wa nje (kitu ambacho ni kawaida sana) angejikinga, ila kuhamua kuzaa naye? Weweeeee, unacheza nini? Naelewa kwanini watu wengine wanahamua kabisa kuua.
 
Mkuu Mkereketwa_Huyu wewe ni Mkereketwa_Huyu Je ulisha wahi kupima DNA na baba yako Mzazi? Uamuzi Mzuri kumuacha au unaweza pia usimuache na uka muhudumia huyo mtoto ingawa sio wako Mke wako anaweza kujiuwa ukichukuwa huo uamuzi.
 
Last edited by a moderator:
Mimi ndo maana nimeahidi kutokuoa lakini kuwachapa na kuwazalisha nitatekeleza!!-sasa itokee litoto lina miaka 20 halafu kumbe umechakachuliwa (hata ukimbuki ilikuaje) ukijua si utalaani ulimwengu wote!!The world is unfair kwa kweli hatuna tofauti na wanyama binadamu hasa hasa tatizo kama hili mama wa mtoto anahusika 100%hivi anajiteteaje?ikitokea hv?huko kwa Mungu inatakiwa kuwepo moto mkali hata ukikaribia tu unayeyeka ndo staili yao!!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Haina ukweli kusema 48.3% ya wanaume wa 'Tanzania'..
Mtu anaepeleka mtoto kupima DNA anayo mazingira yanayomshawishi kua mtoto aweza kua si wake, na hivyo nategemea sampuli ya wapimaji wa aina hii lazima itoe asimilia kubwa. Wachague sampuli sahihi na sio kutisha wananchi

tragedy of the commons
 
Asilimia 48.3 ya wanaume tanzania wamebambikiwa watoto na wake zao
Kuna makosa makubwa kwenye utoaji wa taarifa hii. Watu wanaokwenda kupima DNA ni wachache sana ukilinganisha na idadi ya wanandoa waliopo Tanzania, na hiyo haitoshi kuwa 'sample' ya utafiti. Mimi nadhani ofisi ya Mkemia Mkuu ingesema"Asilimia 48.3 ya wanaume Tanzania walioenda kupima DNA wamebambikiwa watoto na wake zao"
 
Mimi mke wangu hata wakiomba Fukushimayake huko mtaani akirudi tu najua mtu kazengea.
Akija toa Fukushima kwa mtu mwingine hata aoge matra saba,ile tukitazamana macho tu siri itakua nje.

Uongo mtupu.

Ukweli wenyewe ni kwamba jamaa hata wakiikung'uta vipi akirudi mwenyewewe hata hisia za kuibiwa sina.
 
Mkuu Mkereketwa_Huyu wewe ni Mkereketwa_Huyu Je ulisha wahi kupima DNA na baba yako Mzazi? Uamuzi Mzuri kumuacha au unaweza pia usimuache na uka muhudumia huyo mtoto ingawa sio wako Mke wako anaweza kujiuwa ukichukuwa huo uamuzi.


Haisee kwetu tuko sita na sina shaka kabisa na mama yangu kucheza rafu kwani kati yetu sie sita wote kasoro mmoja tunafanana na baba, urefu, tabasamu, rangi, na haswa mimi na kaka yangu wa pili, tuna tabia ya baba na ndio tunaofanana naye zaidi. Sitaki kulea mtoto wa mtu mwingine, nasema sitaki.
 
As a scientist, I am inclined to question the authenticity of the analytical techniques/methods involved- be it PCR, sequencing, etc used..................................before coming to such a figure of 48%! A lot of technicalities are involved particularly in resource constrained countries like ours when it comes to integrity of basic laboratory science techniques! Hiyo figure in kubwa mno. Kitu cha kwanza nitahoji utaalamu, wataalamu, equipments, quality controls in all aspects of the lab etc, etc, etc, etc, etc waliofanya analysis hiyo. Hata preservation of DNA particularly kwetu kunako katikakatika umeme mara kwa mara, nasita kukubali figure kama hiyo!
Pili, wanakwenda wanaume ambao tayari wana mashaka na wake zao! Hakuna random sampling yoyote hapo, ni targeted sampling and therefore targeted analysis which is very much likely to give such results!.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…