Asilimia 82% ya mizigo ya Uganda huwa inapita kwenye bandari ya Mombasa

Asilimia 82% ya mizigo ya Uganda huwa inapita kwenye bandari ya Mombasa

pingli-nywee

JF-Expert Member
Joined
Sep 16, 2015
Posts
11,923
Reaction score
13,350
Nimeshangazwa sana na hizi habari kuhusu mizigo ya Uganda ambayo huwa inapita kwenye bandari ya Mombasa. Baada ya kelele zote ambazo huwa nazisikia humu, kutoka kwa majirani zetu nilidhani kwenye biashara ya kupokea na kusafirisha mizigo ya Uganda, Kenya na Tz tungekuwa tunagawana angalau 50-50. Kumbe ushindani wa bandari ya Dar kwenye biashara ya nchi moja tu ambayo inapakana na nchi zote mbili za Kenya na Tz ni longolongo na porojo tu. Hawa jirani zetu nasikia ni mandugu wa kufa na kupona. Eti na mmoja wao aliikomboa nchi ya mwenzake kutoka kwenye minyororo ya udikteta. Kumbe miaka yote hii ikifika kwenye biashara Kenya na bandari yake ndio imekuwa ikifanya vitu vinavoeleweka? https://www.trademarkea.com/news/kenya-news/82-of-ugandas-cargo-passes-through-mombasa/
 
Kama hata ya Rwanda inapitia Mombasa nashangaa hii sgr yao inaenda wapi?
 
Kwa nchi ambazo zina njia mbadala ni ngumu kupitisha mzigo dar kwa sababu kadhaa. Kubwa ni kutozwa VAT wakati mizigo hiyo haitumiki nchini.
Kwa kawaida biashara ambayo inaingizia nchi fedha za kigeni haitakiwi kutozwa kodi kama vat. Ndio maana bidhaa zinazoenda migodini hazitozwi vat kwa kuwa mwisho wa siku dhahabu inaingiza fedha za kigeni.
Ushindani hautokani na kina kirefu cha maji cha bandari. Bali ni matokeo ya huduma bora, gharama nafuu na wepesi kutoa mzigo wenyewe.
Pia kubadilika badilika kwa taratibu kunawakwaza wapitishaji wengi tu wa mizigo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa nchi ambazo zina njia mbadala ni ngumu kupitisha mzigo dar kwa sababu kadhaa. Kubwa ni kutozwa VAT wakati mizigo hiyo haitumiki nchini.
Kwa kawaida biashara ambayo inaingizia nchi fedha za kigeni haitakiwi kutozwa kodi kama vat. Ndio maana bidhaa zinazoenda migodini hazitozwi vat kwa kuwa mwisho wa siku dhahabu inaingiza fedha za kigeni.
Ushindani hautokani na kina kirefu cha maji cha bandari. Bali ni matokeo ya huduma bora, gharama nafuu na wepesi kutoa mzigo wenyewe.
Pia kubadilika badilika kwa taratibu kunawakwaza wapitishaji wengi tu wa mizigo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Sijataja kuhusu kina kirefu cha maji bandarani. Ila hujakosea, mlilala darasani zamani sana.
 
Nimeshangazwa sana na hizi habari kuhusu mizigo ya Uganda ambayo huwa inapita kwenye bandari ya Mombasa. Baada ya kelele zote ambazo huwa nazisikia humu, kutoka kwa majirani zetu nilidhani kwenye biashara ya kupokea na kusafirisha mizigo ya Uganda, Kenya na Tz tungekuwa tunagawana angalau 50-50. Kumbe ushindani wa bandari ya Dar kwenye biashara ya nchi moja tu ambayo inapakana na nchi zote mbili za Kenya na Tz ni longolongo na porojo tu. Hawa jirani zetu nasikia ni mandugu wa kufa na kupona. Eti na mmoja wao aliikomboa nchi ya mwenzake kutoka kwenye minyororo ya udikteta. Kumbe miaka yote hii ikifika kwenye biashara Kenya na bandari yake ndio imekuwa ikifanya vitu vinavoeleweka? https://www.trademarkea.com/news/kenya-news/82-of-ugandas-cargo-passes-through-mombasa/
Ferry at mwanza is slow and risky..But dont to worry..SGR will branch off to kampala on its way to kigali
 
Back
Top Bottom