MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,675
- 33,583
Wakuu,
Kama tunavyojua amri jeshi mkuu akitoa maelekezo huku chini ni utii tu. Mama Samia alioneshwa kukerwa na clip ya askari akifafanua mchanganyiko unaofanya gongo na kutetea mfumo/ process za utengenezwaji wake. Huku kukerwa ingawa sijadhibitisha inawezekana yule kijana hana kazi tena.
Nimeona majuzi tena mama yetu akikazia tukio lile. Kiukweli naona mama amelibeba kama tukio la ajabu sana na pengine hata huyo kijana kupoteza kibarua. Lakini nashauri busara zitumike kumpunguzia adhabu au kumsamehe huyo kijana ili atumikie taifa lake.
Tunayo mifano ya wazi ikiwemo wabunge tena wa CCM wakitetea bangi bungeni na hawakuonywa popote, tumeona gongo ikitetewa bungeni tena mara nyingi lakini halikutoka onyo lolote. Lakini huyu kijana mdogo clip ndogo imezima ndoto zake!
Nakuomba mama yetu Samia, msamehe kijana wetu! Pia tukio lile lisahau kidogo maana ulishatoa maelekezo. Kuendelea kulirudia ukiwa amri jeshi mkuu na kauli yako ni amri ni kuzidi kumuweka kwenye mazingira magumu.
Mama tafadhali fuatilia huyo kijana apewe nafasi nyingine! Rungu lako kwake ni zito sana, bora wenyewe maafande wapeane adhabu zao wanazozijua ikiwemo lock up ila maelekezo yako yanaweza kumshukia kama kupiga mende kwa nyundo.
Tumuombe Mh. Rais wetu amsamehe huyo kijana.
Kama tunavyojua amri jeshi mkuu akitoa maelekezo huku chini ni utii tu. Mama Samia alioneshwa kukerwa na clip ya askari akifafanua mchanganyiko unaofanya gongo na kutetea mfumo/ process za utengenezwaji wake. Huku kukerwa ingawa sijadhibitisha inawezekana yule kijana hana kazi tena.
Nimeona majuzi tena mama yetu akikazia tukio lile. Kiukweli naona mama amelibeba kama tukio la ajabu sana na pengine hata huyo kijana kupoteza kibarua. Lakini nashauri busara zitumike kumpunguzia adhabu au kumsamehe huyo kijana ili atumikie taifa lake.
Tunayo mifano ya wazi ikiwemo wabunge tena wa CCM wakitetea bangi bungeni na hawakuonywa popote, tumeona gongo ikitetewa bungeni tena mara nyingi lakini halikutoka onyo lolote. Lakini huyu kijana mdogo clip ndogo imezima ndoto zake!
Nakuomba mama yetu Samia, msamehe kijana wetu! Pia tukio lile lisahau kidogo maana ulishatoa maelekezo. Kuendelea kulirudia ukiwa amri jeshi mkuu na kauli yako ni amri ni kuzidi kumuweka kwenye mazingira magumu.
Mama tafadhali fuatilia huyo kijana apewe nafasi nyingine! Rungu lako kwake ni zito sana, bora wenyewe maafande wapeane adhabu zao wanazozijua ikiwemo lock up ila maelekezo yako yanaweza kumshukia kama kupiga mende kwa nyundo.
Tumuombe Mh. Rais wetu amsamehe huyo kijana.