Askari polisi : Yanayosemwa juu yenu ni kweli????

munisijo

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2012
Posts
1,126
Reaction score
942
Ni kweli, umuhimu wenu tunaujua lakini mbona faida yenu hatuifaidi katika ukamilifu? Toka nimekuwa na kumbukumbu, what I remember ni 'Kula, usipokula tunakuitia polisi' ... ni kweli nilikula lakini hadi leo nimekuwa mtu mzima na mwenye akili timamu, mtazamo wangu juu yenu umezidi kuwa hasi zaidi! Sina uhakika kama amani na utulivu tulio nao ni kwa sababu ya uwepo wenu ama utashi tu wa kibinadamu, sina uhakika pia uwepo wenu unaadhiri vipi kupungua/kuongezeka kwa uhalifu ... mara nyingine najiuliza, hivi mkipumzika kwa siku 3, ni kibaya kitatokea?!Yawezekana kisitokee chochote ...

Umaarufu mkubwa niusikiao juu yenu ni kuua, ndio kuua i.e Mwangosi, Mabwe-pande, Majambazi (Ingawa nasikia hairuhusiwi), rushwa , yeah, hapa sio siri mpo vizuri kwa kweli, uonevu, ubabe na matumizi ya nguvu yaliyopitiliza! Sifa nyingine kubwa mliyoipata ni kuthibiti maandamano ya vyama vya upinzani na kukitumikia chama tawala, ndio, kuelekea 2015 nitaendelea kutafiti nione kama tuhuma hizi ni za kweli...

Binafsi, nimekua na imani kubwa kwa 'Traffic Police', ukiacha wale wanaojificha kwenye vichaka na kushtukiza magari, wengi wa hapa mjini ni wachapakazi sana...hebu wafikirie wale wa pale Ubungo, Morocco, Magomeni ama Fire ... yeah, heshima kwenu, ni wabinadamu, wapole, mnaelimisha na kwa pollution ya Dar, MUNGU awalinde, kwa nyie wengine wa kitu kidogo naamini mtajirekebisha! Kundi jingine kubwa, bado jamii hatuja waamini vyakutosha hivyo ni vema mkaanza kujisafisha mapema before its too late .....

Hope anyone would want to prove me wrong, ni kweli, nimeshindwa kabisa kuwasifia askari polisi wengi only because hamtaki kutii viapo vyenu na kufuata sheria ... kama kuna yeyote mwenye ushuhuda mzuri ama mbaya wa askari polisi, karibia jamvini na utupe mtazamo wako kuhusu mada hii ......
 
Unajisumbua kusubili faida ya hao mburura. Hao sio wanataaluma, ni wana mafunzo. Hakunaga Diploma, Degree, Masters au PhD ya U-Polisi. You can train even a dog 2 do a police work.:glasses-nerdy:
 
Sio kweli mkuu,...umuhimu wa polisi kama wakiondoa wote utashkwa hata ---- wewe
 
Unajisumbua kusubili faida ya hao mburura. Hao sio wanataaluma, ni wana mafunzo. Hakunaga Diploma, Degree, Masters au PhD ya U-Polisi. You can train even a dog 2 do a police work.:glasses-nerdy:

Asante kwa kufungua mtazamo wangu zaidi, ni kweli, proffessionalism ni ndogo sana katika jeshi letu la polisi, coz kufyetua bunduki na kupiga mtu virungu hata mtu mwenye mtandao wa ubongo anaweza! Nilitemebelea kituo kimoja, hiyo record keeping yao ni balaa .... roho iliniuma!
 
Umeona eeeh?
 
je kuna taasisi gani ya serikali hapa TANZANIA ukiondoa polisi inafanya kazi vizuri?
 
Unajisumbua kusubili
faida ya hao mburura. Hao sio wanataaluma, ni wana mafunzo. Hakunaga
Diploma, Degree, Masters au PhD ya U-Polisi. You can train even a dog 2
do a police work.:glasses-nerdy:

ipo diploma ya police science na upelelezi wamehitimu jana DPA, kama huoni umuhimu ipo siku utaona kaka tuulize siye tuliokolewa gari lilitekwa! na sijui ni idara gani mnayodhani ni watakatifu
 
Wale mliofika vyuo vikuu, na wadiploma bila kukosea wanaijua sana ethics. Hawa polisi wetu ni wale viazi waliokuwa wamechoka na maisha na hawana option nyingine ya maisha na ndo waliopata zero kwenye mitihani yao!!!
Serekali iachane na suala la kuchukua watu waliofeli na kuwafanya polisi!! Hawafaiiiii!! Wahitimu wa vyuo vikuu ndio wanatakiwa wawe mapolisi na mishahara yao iwe ya maana!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…