Askari trafiki uliyekuwa eneo la Mchicha leo tumia akili au urudi ofisini uwe GD

Askari trafiki uliyekuwa eneo la Mchicha leo tumia akili au urudi ofisini uwe GD

Good Father

JF-Expert Member
Joined
Feb 28, 2014
Posts
10,321
Reaction score
18,574
Wakuu leo asubuhi hii waliopita barabara ya Airport (Pugu road) ni mashahidi kuwa pana foleni ndefu kwa sababu ya misafara ya viongozi, awali alipita Makamu wa Rais, baadae kidogo kukawa na foleni kubwa na askari wengi sana barabarani bila shaka itakuwa IGP naye anatoka kwake Chanika kwenda Mjini.

Sasa kuna kisa kimetokea maeneo ya Mchicha pale kwenye njia panda ya kuingia barabara kubwa (Pugu road), mimi nilipanda bolt niwahi jambo langu, bolt alikosea njia tulikuwa tunatoka uelekeo wa airport kwenda Mchicha, ghafla trafiki huyu hapa ni mmama mtu mzima kama nimeona vizuri ni Staff sergeant wa polisi alikuwa na fimbo yake ya madaraka, yeye baada ya kuona boda amekunja pale alikasirika akarusha ile fimbo yake ili ampige dereva wa bolt.

Sasa nawaza kwa mfano ile fimbo ingempata dereva, pikipiki ikayumba tukapata ajali pale yule trafiki anahisi angekuwa salama?

Au ndio mafundisho mapya kwamba dereva akikosea bahati mbaya unapaswa kumpiga?
Nawaza tena, yule mama leo angekuwa na silaha ya moto angefyatua risasi kwa sababu dereva kakunja sehemu ambayo hairuhusiwi?

Polisi, Polisi, Polisi nawaita tena nawaambia tumieni akili, tumieni akili zenu.

We mama yangu trafiki uliyekuwa Mchicha leo kama tungepata ajali na nikasalimika nisife, ningefatilia vizuri nijue kama Serikali imekuchukulia hatua au la, kama ungeachwa mimi binafsi ningeshughulika nawewe nina hakika nakuweza vizuri tu.

Nawajua vizuri Polisi nje ya hiyo uniform hauna mtetezi, tumia akili zako vizuri maana wakati mwingine hata ukiwa na uniform ukishaharibu kazi wakubwa wako watakukataa.

Kwa muonekano ule wewe hauko mbali na kustaafu, linda hata hicho kipensheni chako.

Ni hayo tu..
 
Iko hivi aliyeanza kuharibu ni nani? Dereva wako wa bodaboda si ndiyo?

Acha kumtamkia mama wa watu maneno ya hovyo.

Tulia achana na kazi za watu, hiyo fimbo alorusha ndo inakutoa povu refu namna hii!
 
Ulitakiwa uzi wa kwanza umuanzishie huyo bodaboda wako. Na kwa vile ni bolt ungeweka na utambulisho wake hapa ili tuwe tunacancel request zetu pindi likitokea jina lake...

Umeshahukumu kuwa boda boda kakosea njia bahati mbaya (very biased) halafu unamuhukumu trafiki kuwa kakosea makusudi na angewaua kwa ajali kisa amewarushia fimbo... KWA KUWA ULITAKA KUWAHI JAMBO LAKO HUKUTAKA KUIRUHUSU AKILI KUJUA KUWA SWALA LA KUPITA NJIA ISIYO SAHIHI NI SABABU TOSHA YA KUWAUA AU KUWAJERUHI KWA AJALI NA KUMKARIPIA HUYO BODABODA WAKO LILITAKIWA LIWE JAMBO LA KWANZA..

Hopeless kabisa
 
Iko hivi aliyeanza kuharibu ni nani? Dereva wako wa bodaboda si ndiyo?

Acha kumtamkia mama wa watu maneno ya hovyo.

Tulia achana na kazi za watu, hiyo fimbo alorusha ndo inakutoa povu refu namna hii!

Amerusha kwa boda boda lakini ajali ingetupata wote namimi ambaye sikuvunja sheria mi ni abiria tu.
Hakuna sehemu nimemtetea bodaboda.

Polisi tumieni akili zenu vizuri
 
Pole pia punguza vitusho huna lolote we ni boya I'm huyo traffic

Boya utakuwa wewe Polisi kilaza

Mimi abiria sina kosa, angesababisha ajali ingenihusu mimi pia wakati mimi sina kosa lolote. Angekamata pikipiki.
Boda boda kukosea kakosea wala simtetei na angekamatwa nisingemtetea maana kakosea alisatahili adhabu lakini sio kurusha fimbo ambayo ingepelekea ajali na pengine kupoteza maisha.
Nyie teteeni ujinga tu lakini kosa la bodaboda halingekuwa na impact ukilinganisha na kosa la trafiki.

Tumieni akili Polisi
 
Ulitakiwa uzi wa kwanza umuanzishie huyo bodaboda wako. Na kwa vile ni bolt ungeweka na utambulisho wake hapa ili tuwe tunacancel request zetu pindi likitokea jina lake...

Umeshahukumu kuwa boda boda kakosea njia bahati mbaya (very biased) halafu unamuhukumu trafiki kuwa kakosea makusudi na agewaua kwa ajali kisa amewarushia fimbo... KWA KUWA ULITAKA KUWAHI JAMBO LAKO HUKUTAKA KUIRUHUSU AKILI KUJUA KUWA SWALA LA KUOITA NJIA ISIYO SAHIHI NI SABABU TOSHA YA KUWAUA AU KUWAJERUHI KWA AJALI NA KUMKARIPIA HUYO BODABODA WAKO LILITAKIWA LIWE JAMBO LA KWANZA..

Hopeless kabisa

Hopeless ni wewe Polisi wa mchongo.
Katika uzi wangu sijamtetea Bodaboda soma upya.

Tukio la trafiki lingeweza kusababisha kifo au majeruhi kwa mimi ambaye sijavunja sheria yoyote mi abiria tu na helmet nilivaa kwahyo ukija hapa usitoe povu bila kuelewa mada
 
Mateso yote hayo usingeyapata kama ungekuwa na gari, pole sana.

Ishu sio gari mkuu, labda kwa kukupa uelewa ni kwamba nilishuka kwenye gari la ofisi nikapanda bolt ili niwahi kibaruani nilikuwa nahitajika. Kwa foleni ile ya misafara hapakuwa na dalili ya kutoka mapema
 
Mngetakiwa mfe wote ili iwe fundisho kwa wengine.
Hakunakukosea sheria kwa bahari mbaya. Unataka kutuaminishia huyo boda ni mgeni wa njia hapa mjink hasaa sehemu ulotaja. Acha kukumbatia uhalifu kwa kulinda maslahi yako ama kujiangalia wewe tu.
Kitendo chakupita sehemu isiyo sahihi ilikuwa chanzo cha ajali pia. Anza kustaarabika then ndo uwastaarabishe wengine. Ungemkemea boda asipite sehemunisiyo sahihi wala usingekwazika leo
 
Again mazuzu ni rahisi kukimbilia majibu rahisi kuliko kuangalia tatizo lipo wapi, alama za barabarani ni zero kabisa hasa hapa Dar, madereva hawajui kabisa jinsi ya kutafsiri sheria hizi angalia kwenye round about ni vurugu tupu, elewa mwenye right of way ni yule aliye ndani ya mzunguko na aliyekulia kwako, wewe wa kushoto you must yield, and why nchi hii kila kiongozi ana blue lights why?,blue lights ni kwa no 1,2 na PM basi, wengine lazima wawahi kutoka kama wanataka kuwahi, it's craze nchi hii
 
Hopeless ni wewe Polisi wa mchongo.
Katika uzi wangu sijamtetea Bodaboda soma upya.

Tukio la trafiki lingeweza kusababisha kifo au majeruhi kwa mimi ambaye sijavunja sheria yoyote mi abiria tu na helmet nilivaa kwahyo ukija hapa usitoe povu bila kuelewa mada
TENDO LA KWANZA... Ulitakiwa uanze kumkaripia kwanza huyo bodaboda wako kwa kupita njia isiyo sahihi, kwa vile ATHARI YA KWANZA KABISA YA HICHO KITENDO INGEKUWA NI KUSABABISHA AJALI NA KUWATIA ULEMAVU AU KUWAUA WOTE NA WEWE ABIRIA UNAYEJIONA HUNA MAKOSA UKIWEMO...

Na uzuri unampini wa kumshikia huyo bodaboda wako UNGEMWAMBIA NAKUREPORT UENDESHIAJI WAKO USIOFUATA SHERIA BOLT pia ulivyomuona huyo traffic police ulitakiwa umsemee..

Unakimbilia kupiga kelele tukio la pili ambalo ni matokeo ya tukio la hovyo la kwanza ambalo kwa vile uliona linakufavour kwenye kuwahi kwako ukalifumbia macho na kukaza mishipa ya shingo kutetea upuuzi..

SIO KILA ANAYETUMIA COMMON SENSE KUKOSOA UPUUZI WAKO NA HUYO BODABODA WAKO NI ASKARI.. hujiulizi kwanini wachangiaji wengi wanakuona wewe ndio wa hovyo! .."Eti mimi sina makosa kwa vile ni abiria tu.... bure kabisa"
 
We na bodaboda wako wote ni wapumbavu ....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Mngetakiwa mfe wote ili iwe fundisho kwa wengine.
Hakunakukosea sheria kwa bahari mbaya. Unataka kutuaminishia huyo boda ni mgeni wa njia hapa mjink hasaa sehemu ulotaja. Acha kukumbatia uhalifu kwa kulinda maslahi yako ama kujiangalia wewe tu.
Kitendo chakupita sehemu isiyo sahihi ilikuwa chanzo cha ajali pia. Anza kustaarabika then ndo uwastaarabishe wengine. Ungemkemea boda asipite sehemunisiyo sahihi wala usingekwazika leo

Nakukumbusha mi nilikuwa abiria wala sikujua kama jamaa angekunja pale.
Kwa nafasi yangu napenda kufuata sheria sana maana nami ni msimamizi wa sheria kwenye taasisi yangu.

Nakuja kushtuka trafiki amerusha fimbo jamaa anaikwepa, unaweza kuona uhusika wangu hapo sasa alafu nikapata ajali nalaumiwa au yanakuwa malipo kwangu kwa kosa lipi nililotenda?
Watu wanakuja hapa kutoa povu ila uhalisia hawajaujua, mimi sikushinikiza bolt akunje pale wala ni ile ghafla jamaa kakunja trafiki huyu hapa anarusha fimbo, imekuwa ni bahati tu halijatokea jambo baya.

Kwa namna yoyote, kama tungepata ajali ningemlaumu trafiki kwa kutomkamata bolt maana angekamatwa sheria ingefuata mkondo wake wala nisingekuja hapa kuanzisha uzi.
 
TENDO LA KWANZA... Ulitakiwa uanze kumkaripia kwanza huyo bodaboda wako kwa kupita njia isiyo sahihi, kwa vile ATHARI YA KWANZA KABISA YA HICHO KITENDO INGEKUWA NI KUSABABISHA AJALI NA KUWATIA ULEMAVU AU KUWAUA WOTE NA WEWE ABIRIA UNAYEJIONA HUNA MAKOSA UKIWEMO...

Na uzuri unampini wa kumshikia huyo bodaboda wako UNGEMWAMBIA NAKUREPORT UENDESHIAJI WAKO USIOFUATA SHERIA BOLT pia ulivyomuona huyo traffic police ulitakiwa umsemee..

Unakimbilia kupiga kelele tukio la pili ambalo ni matokeo ya tukio la hovyo la kwanza ambalo kwa vile uliona linakufavour kwenye kuwahi kwako ukalifumbia macho na kukaza mishipa ya shingo kutetea upuuzi..

SIO KILA ANAYETUMIA COMMON SENSE KUKOSOA UPUUZI WAKO NA HUYO BODABODA WAKO NI ASKARI.. hujiulizi kwanini wachangiaji wengi wanakuona wewe ndio wa hovyo! .."Eti mimi sina makosa kwa vile ni abiria tu.... bure kabisa"

Soma uzi wangu kwanza alafu utafakari, bolt kukunja pale haikuwa discussion kwamba nikamwambia kunja hapo. Mi ni kuhamaki anakwepa fimbo la askari, hapo kosa langu nini labda??

Watu wana mihemuko humu, mimi na kuendesha boda boda wapi na wapi? Mimi nilikuwa abiria, bodaboda mnawajua nyie au mko nje ya nchi??

Ile fimbo ilimlenga bodaboda sio mimi, lakini bodaboda angepoteza concetration sote tungekufa pale, na hata kukata pale kama ingetokea ajali sote tungekufa, sasa kosa la bodaboda halifutwi na tuhuma juu ya Polisi, uhalisia ni kwamba pamoja na kosa la bodaboda bado Polisi anakosa la kurusha fimbo na kusema ukweli kama ningeumia yule Polisi ningemtafuta tu maana kumpata inawezekana.
 
Soma uzi wangu kwanza alafu utafakari, bolt kukunja pale haikuwa discussion kwamba nikamwambia kunja hapo. Mi ni kuhamaki anakwepa fimbo la askari, hapo kosa langu nini labda??

Watu wana mihemuko humu, mimi na kuendesha boda boda wapi na wapi? Mimi nilikuwa abiria, bodaboda mnawajua nyie au mko nje ya nchi??

Ile fimbo ilimlenga bodaboda sio mimi, lakini bodaboda angepoteza concetration sote tungekufa pale, na hata kukata pale kama ingetokea ajali sote tungekufa, sasa kosa la bodaboda halifutwi na tuhuma juu ya Polisi, uhalisia ni kwamba pamoja na kosa la bodaboda bado Polisi anakosa la kurusha fimbo na kusema ukweli kama ningeumia yule Polisi ningemtafuta tu maana kumpata inawezekana.
Bodaboda tunawajua ndio maana hapa tunakusisitiza lawama zako zingeenda kwa bodaboda wako, na unatakiwa umripoti BOLT ili wamfungie... je, wewe unaweza kuikimbiza bodaboda ukiwa kwa miguu!? .... Ila ulitaka huyo askari mwanamama amkimbize na amkamate akiwa kwa miguu [emoji3][emoji3].
Hakuna anayekutolea povu instead tunakupa ukweli mweupe.

Don't take things personal ndugu.
 
Wakuu leo asubuhi hii waliopita barabara ya Airport (Pugu road) ni mashahidi kuwa pana foleni ndefu kwa sababu ya misafara ya viongozi, awali alipita Makamu wa Rais, baadae kidogo kukawa na foleni kubwa na askari wengi sana barabarani bila shaka itakuwa IGP naye anatoka kwake Chanika kwenda Mjini.

Sasa kuna kisa kimetokea maeneo ya Mchicha pale kwenye njia panda ya kuingia barabara kubwa (Pugu road), mimi nilipanda bolt niwahi jambo langu, bolt alikosea njia tulikuwa tunatoka uelekeo wa airport kwenda Mchicha, ghafla trafiki huyu hapa ni mmama mtu mzima kama nimeona vizuri ni Staff sergeant wa polisi alikuwa na fimbo yake ya madaraka, yeye baada ya kuona boda amekunja pale alikasirika akarusha ile fimbo yake ili ampige dereva wa bolt.

Sasa nawaza kwa mfano ile fimbo ingempata dereva, pikipiki ikayumba tukapata ajali pale yule trafiki anahisi angekuwa salama?

Au ndio mafundisho mapya kwamba dereva akikosea bahati mbaya unapaswa kumpiga?
Nawaza tena, yule mama leo angekuwa na silaha ya moto angefyatua risasi kwa sababu dereva kakunja sehemu ambayo hairuhusiwi?

Polisi, Polisi, Polisi nawaita tena nawaambia tumieni akili, tumieni akili zenu.

We mama yangu trafiki uliyekuwa Mchicha leo kama tungepata ajali na nikasalimika nisife, ningefatilia vizuri nijue kama Serikali imekuchukulia hatua au la, kama ungeachwa mimi binafsi ningeshughulika nawewe nina hakika nakuweza vizuri tu.

Nawajua vizuri Polisi nje ya hiyo uniform hauna mtetezi, tumia akili zako vizuri maana wakati mwingine hata ukiwa na uniform ukishaharibu kazi wakubwa wako watakukataa.

Kwa muonekano ule wewe hauko mbali na kustaafu, linda hata hicho kipensheni chako.

Ni hayo tu..
Hakunaga kukosea njia bahati mbaya bro, assume kingetokea chombo kikingine ambacho kipo sawa mkapata ajali? Hao bodaboda usipowaongoza wana michezo ya kipuuzi sana barabarani!!

Halafu, bodaboda anaharibu makusudi abiria ndiyo anakuwa mkali kuhalalisha kosa la Dereva wa bodaboda!!
 
Hakunaga kukosea njia bahati mbaya bro, assume kingetokea chombo kikingine ambacho kipo sawa mkapata ajali? Hao bodaboda usipowaongoza wana michezo ya kipuuzi sana barabarani!!

Halafu, bodaboda anaharibu makusudi abiria ndiyo anakuwa mkali kuhalalisha kosa la Dereva wa bodaboda!!

Reaction ya polisi sijaipenda ingeweza kuleta madhara zaidi kwa sababu ni kufumba na kufumbua jamaa kakunja kona mara naona ana struggle kukwepa fimbo ya polisi
 
Back
Top Bottom