Askari wa cheo gani anatakiwa kunikamata mim?

Askari wa cheo gani anatakiwa kunikamata mim?

Hebel Mlagala

Senior Member
Joined
Aug 4, 2012
Posts
134
Reaction score
49
Hivi karibuni nilimshuhudia Mchungaji Christopher Mtikila akimwambia askari aliye kuwa akitaka kumkamata kuwa hawezi kukamatwa na askari huyo kwakuwa cheo chake (huyo askari) ni kidogo na askari akatii.

Swali langu ni je askari anatakiwa kwenda kumkamata mtuhumiwa kwa kuzingatia cheo chake na hadhi ya mtuhumiwa. Na je mtuhumiwa ana haki ya kukataa kukamatwa na askari wa cheo cha chini?

Sasa mtu mwenye shahada mbili kwa mfano anatakiwa kukamatwa na askari wa cheo gani? Maana asije siku moja akatokea koplo kutaka kunikamata kumbe mimi nastahili kukamatwa na sajenti au meja au IGP mwenyewe!

Na je ni lazima askari ajitambulishe cheo chake wakati wa kumkamata mtuhumiwa au ni juu ya mtuhumiwa kujua cheo cha askri kwa kuangalia alama za vyeo au kumwuliza endapo atakuwa hajavaa sare?
 
mmm!hii nayo kali,kwa hiyo maprofesery watakamatwa na nani?ngoja waje wenyewe watakujibu.
 
Polisi Yoyote anaweza kumkamata Mtu yoyote ikiwa ana kibali cha kukamata Arrest Warrant.
 
hhahhahhaha!hilo ni biti tu la mzee wa mujini bana,hata polisi jamii tu anaweza kumkamata kama anakibali cha kufanya hilo.....
Policcm kaenda kienyeji katulizwa,,,,chezea muzee ya makesi mingi,,lol!

 
Ndo Raha ya kuzaliwa mujini. Askari kapigwa biti kaduwaa, mtikila akasepa. Chezeya pastor weye!?
 
Actually, sio lazima awe polisi. Kuna kitu kinaitwa "citizen arrest". Mbuda (sio polisi) kama mimi na wenzangu tunaweza kumkamata mtu bila ya arrest warrant ili mradi tu mara moja tumfikishe kwenye kituo cha usalama. Tukimtia korona (kamba) na kumfunga kwenye mwembe kwa muda bila ya kutaarifu vyombo vya dola basi anaweza kutushitaki (na akashinda) kwa false imprisonment.

Raia wote wana uwezo wa, na mamlaka ya kumkamata mtu anaedhaniwa ni mhalifu na kumfikisha polisi.

Mfano: Kibaka mitaani aliye dhaniwa amefanya kosa (wizi) anaweza kukamatwa na mtu (watu) yeyote (si lazima awe polosi) na kupelekwa kituo cha polisi.

Upekuzi au Search:
Now, kupekuliwa (search) kwa mtu (nyumbani kwake au yeye binafsi) lazima kufanywe na (m)afisa usalama (w)akiwa na kibali cha korti (search warrant). Vinginevyo ushahidi utakaopatikana kutokana na upekuzi huu unaweza kuwa batili.

Haya, my learnered sisters & brothers (Esqs), nikosoeni hapa.
 
Mtikila alijua hao askari hawajielewi akachimba mkwara jamaa wakaogopa. Hii ndio mambo ya town.
 
Actually, sio lazima awe polisi. Kuna kitu kinaitwa "citizen arrest". Mbuda (sio polisi) kama mimi na wenzangu tunaweza kumkamata mtu bila ya arrest warrant ili mradi tu mara moja tumfikishe kwenye kituo cha usalama. Tukimtia korona (kamba) na kumfunga kwenye mwembe kwa muda bila ya kutaarifu vyombo vya dola basi anaweza kutushitaki (na akashinda) kwa false imprisonment.

Raia wote wana uwezo wa, na mamlaka ya kumkamata mtu anaedhaniwa ni mhalifu na kumfikisha polisi.

Mfano: Kibaka mitaani aliye dhaniwa amefanya kosa (wizi) anaweza kukamatwa na mtu (watu) yeyote (si lazima awe polosi) na kupelekwa kituo cha polisi.

Upekuzi au Search:
Now, kupekuliwa (search) kwa mtu (nyumbani kwake au yeye binafsi) lazima kufanywe na (m)afisa usalama (w)akiwa na kibali cha korti (search warrant). Vinginevyo ushahidi utakaopatikana kutokana na upekuzi huu unaweza kuwa batili.

Haya, my learnered sisters & brothers (Esqs), nikosoeni hapa.

No comment Upo Sawa kabisa
 
Duh Mtikila jamani kafanya nn tena na biti zake?
 
Hivi karibuni nilimshuhudia Mchungaji Christopher Mtikila akimwambia askari aliye kuwa akitaka kumkamata kuwa hawezi kukamatwa na askari huyo kwakuwa cheo chake (huyo askari) ni kidogo na askari akatii.

Swali langu ni je askari anatakiwa kwenda kumkamata mtuhumiwa kwa kuzingatia cheo chake na hadhi ya mtuhumiwa. Na je mtuhumiwa ana haki ya kukataa kukamatwa na askari wa cheo cha chini?

Sasa mtu mwenye shahada mbili kwa mfano anatakiwa kukamatwa na askari wa cheo gani? Maana asije siku moja akatokea koplo kutaka kunikamata kumbe mimi nastahili kukamatwa na sajenti au meja au IGP mwenyewe!

Na je ni lazima askari ajitambulishe cheo chake wakati wa kumkamata mtuhumiwa au ni juu ya mtuhumiwa kujua cheo cha askri kwa kuangalia alama za vyeo au kumwuliza endapo atakuwa hajavaa sare?
awali ya yote uelewe askari yoyote mwenye kuanzia cheo cha chini yaani police constable ana haki ya kukukamata akiwa na report book (RB) hapo ni haki yake kukukamata sema huyo askari hajui haki zake huo ni mkwala tu wa raia na akikataa kukamatwa anatakiwa afunguliwe kesi ya kukataa amri halali ya polisi na wewe unayekamatwa una haki ya kumuomba RB na kama hajavaa sare unatakiwa umuombe kitambulisho cha kazi ili akupe ujue ni askari na hapo ukubali kwenda kituoni kwa hatua zaidi
 
Hahaha. Mtikila bwana! I wish we were friends!

You can create the friendship for that purpose as long as you know what you want.

Ila kwa hizo gwanda kwenye avatar yako sijui askari wa cheo gani atakukamata...LoL
 
Back
Top Bottom