Askofu amekuja na Gwajima Rede Cup

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamis Mwinjuma Septemba 3, 2023 Jijini Dar Es Salaam amefungua mashindano ya mchezo wa rede (Gwajima Rede cup) katika jimbo la Kawe.

Akizungumza wakati wa kufungua mashindano hayo, Mwinjuma amesema Serikali inathamini michezo ya aina zote, ambapo ameeleza kuwa, mchezo wa Rede ni miongoni mwa michezo ya jadi ambayo inapewa kipaumbele na itaendelea kuwekewa mazingira bora ili jamii iifurahie mchezo huo.


Mashindano hayo yaliyoandaliwa na Mbunge wa jimbo hilo Mhe. Askofu Josephat Gwajima yanahusisha timu nane kutoka katika kata za jimbo hilo.

 
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma Septemba 3, 2023 Jijini Dar Es Salaam amefungua mashindano ya mchezo wa rede (Gwajima Rede cup) katika jimbo la Kawe...
2025 is loading...........😂😂
 
Huyu jamaa yangu Gwaji Boy kila ninapoikumbuka ile clip yake aliyojirekodi na ile pisi nyeupe, na namna alivyokuja kuikana hadharani eti hakuwa yeye!! Enzi hizo vita yake na DAB ndiyo imepamba moto kweli kweli!! Huwa nabakia tu kucheeka.
 
Bila shaka atatafuta kati yao aliyenona ili aendeleze nae Utamaduni wake wa Kurekodi Movie ya Kibaiolojia kama ile ya 2020 iliyobamba Tanzania nzima.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…