Uchaguzi 2020 Askofu Bagonza aleta tafakuri nzito akihusisha Uchaguzi Mkuu 2020 na maajabu ya Corona na kupigwa risasi kwa Tundu Lissu

share

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2008
Posts
6,064
Reaction score
10,468
Mheshimiwa Mhashamu Askofu Bagonza leo wakati akitoa nasaha zake kwenye mkutano wa kampeni za Uchaguzi Mkuu 2020 huko mkoani Kagera amesikika akitaja mambo matatu.

Moja kati ya hayo ni kuwa Uchaguzi Mkuu huu una wakutanisha watu wawili wanaojinasibu moja kwa moja na maajabu ya Mungu. Mmoja anajiuza binafsi kuwa ameufukuza Corona virus kwa maombi na mwingine anamshukuru Mungu kwa maajabu ya kulinywa baada ya kupigwa risasi zaidi ya 30 huku 16 zikiingia mwilini.

Askofu Bagonza anawaambia Wana Kagera ni yupi anastahili kupigiwa kura. Mfukuza korona (kama kweli ni muujiza) na anayeishi baada ya kupigwa risasi 16 mwilini. Watoe uamuzi tarehe 28 Oktoba 2020.

Sisi tusiokuwepo Kagera hili pia ni JAMBO LETU. Lipi kati ya hayo mawili ni ajabu la Mungu? Kufukuza korona au kupona kipigo cha risasi 16 mwilini? JAMBO LETU tarehe 28 Oktoba 2020 liwe kwa nani?
 
Huyu Baba Askofu huwa namfananisha na yule aliyeuawa na Nduli Iddi Amin, kwa kumweleza ukweli.

Watumishi wa aina hii huwa ni nadra sana kuwapata. Nabii Yohana Mbatizaji aliuawa kwa kukatwa kichwa.na Herode kisa alimkemea kwa kuoa na mke wa ndugu yake aliyemuua.

Tuwaombee sana Watumishi wa Mungu wasiojua kuchanganya rangi. Usishangae akaja kuitwa sio Mtanzania.
 
Kwahiyo Bagonza pamoja na PhD yake kaona hiyo ndio sera ya kuwaambia wana Kagera?

Huyu corana ili mvuruga kumbe? Maana akijishaua kufunga makanisa kwenye dayosisi yake wakati wenzie wameungana na watz kumuomba Mungu!

Naona bado anaona aibu kwa kumtukuza shetani badala ya Mungu.

Haka kajamaa lazima hata hirizi kanayo
 
Bagonza hachanganyi rangi?

Hivi huyo ana tofauti gani na Gwajima?
 
Mnafiki Hugo Askofu
 
 

Attachments

Mheshimiwa Mhashamu? Ndio kitu gani hicho? By the way sidhani kama KKKT wana Mhashamu.
 
Bagonza ni mnafiki tu bado anaona aibu ya kufunga makanisa kisa corona huku wenzie wameamua wasali!

Yeye alimtukuza shetani badala ya Mungu
Gwajima alivyomtukana Askofu Pengo na hilo unalionaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…