Askofu Bagonza, barua ya kumkaribisha Rais Magufuli Mkoani Kagera na tahakiki ya mjadala tunduizi


Kuna tofauti kubwa kati ya Yesu aliyezaliwa kijiweni na askofu mwenye kanisa lililoezekwa kwa mabati yanayoshilikiwa kwa kuta za mabati huku akikusanya sadaka na kujenga orofa nyumbani kwake kwa ajili ya mke, watoto na ukoo wake.

Yesu wa kijiweni ni bora kuliko askofu tapeli anayeishi orofani.


Homeless Jesus was born in KICHEFUCHEFU LABOR WARD at Bethlehem
 
Hivi kila mkoa kuwa na chuo ni sera ya taifa ama?! Naomba kueleweshwa.
 
Alichofanya mleta bandiko ndivyo CRITICAL DISCOURSE ANALYSIS inafanyika.
Unashauriwa kuanza kuizoea.
Kama hutaki kuona CRITICAL DISCOURSE ANALYSIS usisome bandiko hili.
Mhadhiri mkuda! Mara useme bandiko linasomeka hata kwa darasa la saba mara nione critical discourse analysis. Lipi ni lipi? Superiority complex at play!
 
Hivi kila mkoa kuwa na chuo ni sera ya taifa ama?! Naomba kueleweshwa.
Sio sera ya Taifa.

Lakini, pointi ya mwandika waraka ni kuwa mchujo wa p/schoool unajaza s/school, mchuzo wa s/school unajaza college/vyuo.

Kwa kuwa kuna wanafunzi wengi kutoka kila shule ya Kata, it is logical kufikiria juu ya vyuo vya mikoa na Taifa.

However, that needs to be argued carefully, kwani sio lazima wanafunzi wa mkoa X wasomee chuo kilichoko mkoa X.
 
Mhadhiri mkuda! Mara useme bandiko linasomeka hata kwa darasa la saba mara nione critical discourse analysis. Lipi ni lipi? Superiority complex at play!
Critical discourse analysis ndivyo ilivyo. Izoee. Huwa tunafanya matatu makubwa:

- kwanza ni kubainisha hoja kwa kuangalia sehemu zake nane: claim, ground, warrant, backing, objection, rebuttals, qualifiers and concessions.

- pili ni kuhakiki hoja kwa kuangalia muundo na maudhui yake kama yanakidhi vigezo vya ukweli uliomo katika jamii.

- tatu, ni kuchunguza kama ukweli uliomo katika jamii ni ukweli wa kudumu au ukweli wa mpito wenye kutengenezwa na kikundi cha watu kwa ajili ya maslahi binafsi.
 
Mhadhiri mkuda! Mara useme bandiko linasomeka hata kwa darasa la saba mara nione critical discourse analysis. Lipi ni lipi? Superiority complex at play!

Kipi bora:

Superiority complex?

Inferiority complex?

Au unyenyekevu complex?
 
Mhadhiri mkuda! Mara useme bandiko linasomeka hata kwa darasa la saba mara nione critical discourse analysis. Lipi ni lipi? Superiority complex at play!

Kipi bora: mhadhiri mkuda au askofu waruwaru?
 
Kipi bora:

Superiority complex?

Inferiority complex?

Au unyenyekevu complex?
Ms Critical Discourse Analysis, hapo hakuna kilicho bora. Nimekuelewa kuwa unadhani superiority complex ni bora! The complex you're practicing. Hata nayo haifai hata kidogo. Kwa kuwa humaanisha arrogance iliyopitiliza.

Wakati inferiority complex ni unyenyekevu wa kuelekea kwenye ujinga! Hakuna complex nzuri. Kila kitu kiwe kwa kiasi. Hata upendo na uzuri wake wote nao pia uwe kwa kiasi. TOO much of ANYthing(complex) is HARMful!
 
Kipi bora: mhadhiri mkuda au askofu waruwaru?
Najua chaguo lako hapo. Na hivyo ndivyo ulivyo,unfortunately! Kama kuna jambo lolote baya kwako academically, chanzo chake ni ujivuni pachae ukuda! Muhongo complex. Na hili ndilo sababu ya bandiko lako. Askofu waruwaru? Hivyo ulterior motive ya bandiko lako ni yote mawili disinformation na malinformation.

Wataka nini au walenga nini ni usiku wa giza kwangu. Bado nasoma mabandiko yako with reservations kwa sababu sikufahamu. Kukufahamu ni muhimu kuongeza uelewa maridhawa wa mabandiko yako! Moral Rearmament wanasema: you can't live crooked and think straight nor think crooked and live straight. Nakubaliana!
 
Pole Askofu. Kanisa ni wito. Karibu uraiani.toa kanzu shika bakora
 

Sasa, hiyo ni theomania kama sio kupiga ramli.

Unajuaje chaguo langu kabla sijakwambia?.

Kwani wewe ni Mungu anayejua kila kitu?

Naina, unadondisha maneno kama maembe yadondokavyo toka mtini. Live croooked, think straight, ujivuni pachae ukuda, etc Jesus lived a crooked life, yet thought straight to convince you become his follower!

Jielekeze katika hoja, achana na mleta hoja. Lakini nasisitiza: ni vigumu kwa Dr. Bagonza kupata audience ya serikali kama hajajitenga na haya matatu: disinformation, misinformation, malinformation about the government. Anajua vizuri makosa yake, lini yamefanyika, kwa vipi, na kwa sababu gani.

Nimeifanyia kazi barua yake kwa umakini Kwa vile naona inapigania maslahi ya umma mpana.

Anaweza kupata fursa ya ushirikiano na serikali kwa kiwango hicho, lakini sio kabla ya kujirekebisha.
 

Sawa. Too much of anything complex is harmful.

Lakini, mbona huchukui hatua ya kubomoa mifumo inayopinga slogan yako hii?

Sheria za Kanisa lako zinasema kuwa deliberative power is exclusively reserved for the clergy (institutionalised superiority complex).

Sheria hizo zinaongeza kusema kuwa the power of the laity is exclusively restricted to consultative power (institutionalized inferiority complex)

These are two extremes contradicting your slogan.

Any plan of transforming this institutionised sin of social inequality contrary to divine will about the equality of human dignity as specified by rational, intellectual and volitional powers equally possessed by the clergy and laity alike?
 
Kuna wakati baba askofu alibaini kuna watu waliotaka kumdhuru. Akasema wamefika Karagwe. Nadhani wale wanaojulikana sana wasiojulikama. Nahisi ni wakati ule unaabiri kuelekea Rwanda. Ilikuwa lazima upite Karagwe na kuulizia nafasi kwa ajili ya nduguyo ya kujiunga na chuo kikuu.
Chuo kikuu ambacho hakijasajiliwa kwa sababu ya mwanzilishi kuwa na mdomo. Yote unayajua. Suluhisho ni kuunga mkono juhudi. Vinginevyo asahau kama Rugemalira kuhukumiwa na mahakama. Alishahukumiwa na DPP. Yeye si mahabusu bali mfungwa.
Wasiojulikana wakajulikana. Wamerudisha visu kwenye ala. Wamechomoa kalamu. Aliyemshindia wa jambia bado yu hai. Kumtetea atamtetea tu. Si lazima kuokota makopo. Hata kumuita mtumishi wa Mungu waruwaru, tapeli sio jambo dogo. Hili ni kujitoa mhanga.
Mwanzo nilifikiri watu hawachangii hili bandiko kwa sababu ya urefu wake. Hawana muda wa kulisoma. Mafuta ya kula yamepanda bei sana. Wanaikimbiza shilingi. Imeota mbawa. Sasa ni bayana hawachangii kwa kuwa hawataki kukaribiana na mlaaniwa. Nami sasa nanawa mikono. Kazi nimemaliza. Endelea!
 

Naona unamjadili mtu unayemwita askofu na kumtaja kama mtu wa mungu bila kubainisha ushahidi wa matamko hayo na badala ya kujadili hoja ya bandiko. That is a tangential response. It warrants no further comment. Kuhusu takwimu za wasomaji, wachangiaji na watazamaji ulizoulizia, hizi hapa:



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…