BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
HAKI na UHURU VIMEUMANA!
Maneno "haki" na "uhuru" yameanza kusikika kwa kasi toka midomoni mwa watawala na Viongozi wetu. NAWAPONGEZA.
Hakuna aliyepiga marufuku matumizi ya maneno haya lakini si kila marufuku inatolewa hadharani. Taifa lilishtuka pale tulipoona haya:
1. Watawala waliposisitiza zaidi "uhuru wenye mipaka" badala ya uhuru wenyewe.
2. Walisisitiza "amani" kuliko haki.
3. Wakasisitiza "wajibu" kuliko haki.
4. Kazi ya bunge ikawa ya "kuishauri" serikali na SI "kuisimamia".
Matokeo yake tukapata haya:
i. Utulivu usio na amani
ii. Utumwa mstaarabu
III. Nidhamu ya woga
iv. Matumizi ya nguvu kuliko akili
v. Matumizi ya Vikosi Kazi badala ya mfumo-kazi.
vi. Wakuu wa mikoa na Wilaya wakawapa wabunge masaa 24 warudi bungeni vingine watatiwa pingu
vii. Spika akawa na nguvu kuliko bunge, Rais akawa na nguvu kuliko nchi na wananchi wakawa chini ya vyote.
Sasa hivi wakuu wa mikoa wanatamka neno HAKI. Spika anazungumzia "watu wajimwage wasikie wana nafasi". IGP anawaambia maaskari watende haki na kuelimisha badala ya "notification".
Naamini hata Msajili wa vyama ataanza kutafuta neno HAKI lilienda wapi. Vyama vya siasa vitaachana na kunyonya titi la vyombo vya dola. Wabunge wataiacha serikali ijitetee ili wao waisimamie.
Rais wetu asiingizwe wala yeye mwenyewe kuingia jikoni kwa vitu vidogo (micromanagement). Tulifika mbali, hata wanaume kuchelewa kurudi nyumbani anaambiwa Rais!!
Maneno "haki" na "uhuru" yameanza kusikika kwa kasi toka midomoni mwa watawala na Viongozi wetu. NAWAPONGEZA.
Hakuna aliyepiga marufuku matumizi ya maneno haya lakini si kila marufuku inatolewa hadharani. Taifa lilishtuka pale tulipoona haya:
1. Watawala waliposisitiza zaidi "uhuru wenye mipaka" badala ya uhuru wenyewe.
2. Walisisitiza "amani" kuliko haki.
3. Wakasisitiza "wajibu" kuliko haki.
4. Kazi ya bunge ikawa ya "kuishauri" serikali na SI "kuisimamia".
Matokeo yake tukapata haya:
i. Utulivu usio na amani
ii. Utumwa mstaarabu
III. Nidhamu ya woga
iv. Matumizi ya nguvu kuliko akili
v. Matumizi ya Vikosi Kazi badala ya mfumo-kazi.
vi. Wakuu wa mikoa na Wilaya wakawapa wabunge masaa 24 warudi bungeni vingine watatiwa pingu
vii. Spika akawa na nguvu kuliko bunge, Rais akawa na nguvu kuliko nchi na wananchi wakawa chini ya vyote.
Sasa hivi wakuu wa mikoa wanatamka neno HAKI. Spika anazungumzia "watu wajimwage wasikie wana nafasi". IGP anawaambia maaskari watende haki na kuelimisha badala ya "notification".
Naamini hata Msajili wa vyama ataanza kutafuta neno HAKI lilienda wapi. Vyama vya siasa vitaachana na kunyonya titi la vyombo vya dola. Wabunge wataiacha serikali ijitetee ili wao waisimamie.
Rais wetu asiingizwe wala yeye mwenyewe kuingia jikoni kwa vitu vidogo (micromanagement). Tulifika mbali, hata wanaume kuchelewa kurudi nyumbani anaambiwa Rais!!
"Kwa mtu mmoja dhambi iliingia na hatimaye MAUTI... na kwa mtu mmoja wokovu ulirejea" (Warumi 5: 12-21).