Askofu Gwajima: Waafrika tumepitia taabu nyingi kuanzia Utumwa, ukoloni, magonjwa na umaskini tukashinda hata Corona haitatuweza

Ngoja nikujibu:
1. Mungu ni mwenye neema na rehema kwa wampendao. Yeye huwapatiliza wana maovu ya baba zao hata kizazi cha nne cha wale wamchukiao but He shows loves for those who love Him (Exodus 20:4-6)
2. The root of every man’s problem is sin and the solution to every man’s problem is remission of sin through Jesus Christ
3. Njaa, magonjwa, vita, na mabaya mengine ni matokeo ya dhambi
4. Ikiwa mtu atamtumainia Mungu na kumtumikia kwa moyo wake wote na kwa nguvu zake zote na kwa akili zako zote hakika mabaya hayatakaribia kwake
5. Taifa ambalo watu wa Mungu wamejinyenyekesha na kumwomba Mungu na kuziacha njia zao mbaya, Mungu huliponya taifa hilo (2 Nyakati 7:14)
5. Huwezi ukamwacha Mungu ukategemea akili zako na ukafuata njia zako halafu ukabaki salama
 
Well said!
 
Ngoja kidogo...

Hapo kwenye Mungu ni zaidi ya sabuni na vitakasa mikono. Yaweza kuwa sawa ki-imani lakini ukweli halisi ni kwamba sabuni na sanitizer zina kemikali zinazoshambulia koti la hawa virusi na hivyo kuwaharibu kabisa.

Huyu mtu asilete kejeli kwenye mambo ambayo hana ufahamu nayo.
 
ujue hapa bongo mungu atuepushe tu, naona kama tunaleta ujuaji sana.ukikaa ukatizama mataifa makubwa watu wanavyo potea.
 

Ahsante kwa angalau kujaribu kujibu, sasa ngoja nikuonyeshe tatizo lilipo kwenye point zako.

1. Umesema mungu ni mwenye neema na rehema kwa wanaompenda. Waafrika mnavyompenda huyo mungu leo hii mko wapi? mbona waovu wengi ndiyo wanatanua dunia hii wanaishi maisha mazuri kuliko wanaokaa kusali kila siku? Hiyo neema yake naona kashindwa kuionyesha, au ana neema ila hana nguvu?
2. Remission of sin kupitia yesu mhh, ndugu unasahau kuna dini zaidi ya 3,000 na ukristo peke yake ndiyo unaamini mambo ya yesu, nyingine zote hata hawana muda na huyo yesu, sasa unataka uniambie wanaoishi vizuri wote wanamuamini yesu? wasiomuamini je? look at the data.
3. Njaa magonjwa vita nii matokeo ya dhambi, hapa naweza ungana na wewe, njaa na vita tunaweza vitokomeza kabisa kama watu tungependana na kusaidiana, magonjwa hapana, hayo yapo tu biologically ipo siku yataibuka kutoka kwa wanyama au viumbe wengine yatatupata tutapambana nayo tu, hata tuwe wema kiasi gani magonjwa yatakuwepo tu, watu mnasali kila siku ila bado mnaugua.
4. Fix tu, wapo wanaomtumikia mungu 100% wanapigwa njaa wanakufa hawana furaha, wengi mno tusiende mbali we tazama watu wanaokuzunguka tu, ila wasiomtumikia huyo mungu wenu wanakula bata tu duniani mnawaona kwenye tv kila siku
5. Waafrika wanaongoza kwa kusali duniani kwa huyo mungu wenu, niambie nchi ya afrika ambayo imeponywa na huyo mungu hata moja.
6. Nilimuacha zamani sana, maisha yangu yameenda vizuri tokea kipindi hicho. Yaani ni mafanikio baada ya mafanikio, angalia tv wavuta bangi, watukana matusi ndiyo wanatawala dunia hii, wapo wenye tabia nzuri pia ila hawana muda na huyo mungu wala nini na wana maisha mazuri mno, turudi sasa kwa nyie mnaosema mnamshikilia, kila siku mnawaza kesho mtakula nini.

Mkuu unajua tatizo ni moja, ukiwa ndani ya kifungo cha dini yote haya huyaoni, nilikua huko mimi, nilikua nasali kila siku, kanisani sikosi, nimekuzwa kikristo toka utotoni na nilikua nina imani sana, ila the moment nilivyokua nikaanza kuquestion nikagundua yote ni upuuzi tu. Wanaomtegemea huyo mungu wengi madoro, vilaza (huoni waumini wa gwajiima walivyo?). Shida tupu
 


Hivi bado kuna maboya hapa Tanzania wanamsikiliza huyu kinyago/msanii? Mi nilifikiri alikuwa anawachezea misukule yake tu, kumbe hata watanzania wenye akili timamu nao wamo? Hapa anacheza na akili za wabongo wasiojitambua kwa kuwaambia upuuzi, akitoka hapa anakwenda chapa mke wa mtu Guest na bado tu watu/waumini wake misukule watabisha na kusema mtumishi wa Mungu hatombi. Mnakwama wapi watanzania, mnatia haibu jamani.
 
ujue hapa bongo mungu atuepushe tu, naona kama tunaleta ujuaji sana.ukikaa ukatizama mataifa makubwa watu wanavyo potea.


Na Magufuli bado anawaambi wananchi wake wazidi kurundikana makanisani na misikitini eti Mungu atatuepusha. Mungu huyo huyo katupa akili ya kujaji uhalisia wa vitu na upuuzi kwa kutumia common sense. Hizi dini za kuletewa kwa kweli zinatulostisha sana waafrika, tunashindwa hata kujitafakari jamani?
 
Umekaririshwa Biblia wewe! Hivi unafikiri wanaokufa kufa kwa Korona wanadhambi kulko sisi ...! kWA HIYO UKIFA KWA MAGONJWA WEWE HUMTEGEMEI MUNGU....mBONA MAGONJWA NDIO VYANZO VYA VIFO VINGI DUNIANI!
 

Kwa muktadha wa imani( ya kikiristo) uko sawa kabisa.

Lakini ki- sayansi hapana.

Kwenye sayansi ambako pia ndio kwenye uhalisia tunaongozwa na ushahidi wa kimaumbile unaotambulika na milango yetu ya fahamu ikisaidiwa na vifaa maalum vinavyotuwezesha kutambua vile ambavyo viko nje ya uwezo wa viungo vyetu vya fahamu.

Na kwa kuwa Covid-19 sio tatizo la ki-imani, ni vizuri zaidi kuzingatia masuluhisho ya kitaalamu(sayansi) kuliko yale ya ki-imani.

Yote kwa yote naheshimu sana imani yako mkuu na pia nani ajuae? Pengine hayo masuhulisho ya kisayansi ni uvuvio kutoka kwa huyo “aliye juu”!
 
Unasemaje ...Mtumishi wa Mungu hafanyi nini...........! Mkuu kuna watoto humu ,...polepole!😀😀😀😀
 
1. Sio kila anayeenda kanisani anampenda Mungu. Wampendao Mungu wanatabia zao zinazowatofautisha na wasiompenda Mungu.
2. I’m a Christian, I believe in the Living Jesus and not historic Jesus. Msingi wa imani yangu na mahusiano yangu kwa Mungu ni Yesu. I’m confident to say the founders of other religions are dead and buried in tombs but in Christianity our Jesus is alive
3. Asante kwa kukubaliana na mimi
4. Hao watu wana mungu wao sio huyu Mungu ninaye muhubiri. Kwa mtu anayemtumikia Mungu akipigika huwa ajua tatizo liko wapi na mara zote tatizo huwa liko kwa mtu mwenyewe na wala sio Mungu
5. Ni kweli lakini kuwa mfuasi wa ukristo au dhehebu flani si lazima kumaanisha una Mungu. Bila udhihirisho wa nguvu za Mungu katika maisha binafsi ya mkiristo basi ukristo wake hauna maana, anabaki na dini tu.
Christianity is not merely a religion but a relationship with God through Christ Jesus
6. Watawala dunia hii na wale wanaamini kuwa kuna supernatural being. Wafanya biashara, politicians na wenye mamlaka believe in God or gods, they either worship God or gods
 
Asante sana kwa comment yako nzuri. Bahati nzuri mimi pia nimesoma sayansi na hata Bachelor’s degree yangu ni ya sayansi lakini kwa neema ya Mungu nimepata kujua there is God’s supper natural power a natural and carnal man cannot comprehend.
Kusoma sayansi hakujanilimit kumjua Mungu. Sayansi inashughulika katika kutatua matatizo ya mazingira ya nje yanayomzunguka mwanadamu(physical world) lakini Mungu anakwenda beyond this physical world.
In Christ Jesus we comprehend the incomprehensible, we know the unkowable and we fathom the unfathomable
 
Kuna watu kiyama watakuwa kuni za kuwachoma wengine! Huyu mtu sio nabii wala mtume ni zaidi ya utapeli! wanacheza na akili za wajinga na kuwatapeli!
 
Nani kamsamehe mwenzake??
Afu lile sakata la video yake ya ngono liliishaje? Maana alisema ataanika kila mtu aliyehusika...
Acheneni na matapeli, hawana lolote hawa ni utapeli na ulaghai tu!
 
Nimekuelewa bwashee!
 
Unahoja nzuri japo kuwa hukuwa unamaanisha Mungu/MUNGU, ulikuwa unamaanisha mungu, waabudu sanamu utawajua tu hata waspojitambulisha,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…