Askofu Mwamakula: Hatuwezi kunyamaza

Askofu Mwamakula: Hatuwezi kunyamaza

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
843639DC-A1C0-4549-9E74-7B17B2B3989F.jpeg


Baadhi ya watu wanashangaa Askofu Mwamakula kuwatetea CHADEMA! Wapo wanaoshauri Askofu awe anafanya mara moja moja lakini sio kila mara. Wakati wa janga la UKIMWI, tulizika ndugu zetu wengi. Lakini hatukuchoka kulia kila ndugu alipokufa eti kwa sababu tulilia misiba ya jana na juzi. CHADEMA wapo katika msiba mzito. Kila siku viongozi na wanachama wao wanakamatwa, wanavunjiwa Ofisi zao, wanapigwa, wanabambikiwa kesi, wanaswekwa ndani, wanaporwa chaguzi, nk. Tunaweza kuchoka kulia nao lakini tusichoke kuwatetea wanapopigwa bila sababu. Kijijini, adui alipofiwa hatukumsusia kuzika.

Jana, Askofu aliongea na Catherine Ruge, Katibu Mkuu wa BAWACHA. Alimshauri kuongoza kwa umakini wakati wenzake wako kizuizini. Leo tumeambiwa kuwa Catherine amekamatwa na Polisi alipokwenda Kisutu kusikiliza Kesi ya Mbowe. Amekamatwa pamoja na viongozi wengine wa BAWACHA akiwemo Makamu Mwenyekiti wao Shariffa na Suzana Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Kukamata viongozi wengi namna hii pasipo sababu za msingi kunaweka ombwe la uongozi. Wafuasi wao wakiamua 'kucheza mdundiko' uraiani, hakuna atakayewatuliza.

Katika mazingira haya, sisi Askofu hatuwezi kunyamaza. Hatuwezi kuacha kupaza sauti eti kwa sababu tulifanya vile jana! Ni nani anayeweza kufurahia mapumziko wakati jirani anaomboleza? Tunalitaka Jeshi la Polisi kumuachia Catherine Ruge na wenzake pasipo masharti ye yote. Tutunze utulivu uliopo, tusiweke mianya ya kuuondoa.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
 
Mfumo wa sasa wa uendeshaji wa Jeshi la Polisi Tanzania unapaswa kufumuliwa wote na kusukwa upya, ili lipatikane kuwepo jeshi jipya ambalo linajiendesha kwa waledi na kuzingatia hali halisi kutokana na matakwa ya wakati. Hili la sasa ni sawa tu na lile kundi la "green guard" ambalo limefichwa kwa kile kionekanacho kama jeshi la polisi.

Ni aibu na fedheha kubwa sana kuwa na jeshi kama hili
Ni gani ambalo linashindwa kuwajibika kwa mujibu wa sheria za nchi isipokuwa tu kupitia maelezeko ya makada wenye mawazo finyu wa chama tawala.

IGP Zero..Oh! No...Ziro..Oh! Yes Zero..Oh! No... I mean Siro. You must do something to stop this nonsense and nuisance.
 
Kitengo cha maccm hao. Huwa wanaitiwa ubwabwa Ikulu, kilo 10 za mchele na vibahasha vya kaki vyenye 20,000 ndani basi hujiona watu wa maana sana hivyo kuunga mkono juhudi.
Natamani kusikia neno kutoka Bakwata
 
Kitengo cha maccm hao. Huwa wanaitiwa ubwabwa Ikulu, kilo 10 za mchele na vibahasha vya kaki vyenye 20,000 ndani basi hujiona watu wa maana sana hivyo kuunga mkono juhudi.

mkuu naona unataka kuchafua hari ya hewa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji2223][emoji2223][emoji2223]
 
Kwani wananchi wanasemaje juu ya kuwapigania viongozi wao pendwa wa chadema[emoji1][emoji1].

Au hawana muda!!!
 
View attachment 1884050

Baadhi ya watu wanashangaa Askofu Mwamakula kuwatetea CHADEMA! Wapo wanaoshauri Askofu awe anafanya mara moja moja lakini sio kila mara. Wakati wa janga la UKIMWI, tulizika ndugu zetu wengi. Lakini hatukuchoka kulia kila ndugu alipokufa eti kwa sababu tulilia misiba ya jana na juzi. CHADEMA wapo katika msiba mzito. Kila siku viongozi na wanachama wao wanakamatwa, wanavunjiwa Ofisi zao, wanapigwa, wanabambikiwa kesi, wanaswekwa ndani, wanaporwa chaguzi, nk. Tunaweza kuchoka kulia nao lakini tusichoke kuwatetea wanapopigwa bila sababu. Kijijini, adui alipofiwa hatukumsusia kuzika.

Jana, Askofu aliongea na Catherine Ruge, Katibu Mkuu wa BAWACHA. Alimshauri kuongoza kwa umakini wakati wenzake wako kizuizini. Leo tumeambiwa kuwa Catherine amekamatwa na Polisi alipokwenda Kisutu kusikiliza Kesi ya Mbowe. Amekamatwa pamoja na viongozi wengine wa BAWACHA akiwemo Makamu Mwenyekiti wao Shariffa na Suzana Kiwanga, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA. Kukamata viongozi wengi namna hii pasipo sababu za msingi kunaweka ombwe la uongozi. Wafuasi wao wakiamua 'kucheza mdundiko' uraiani, hakuna atakayewatuliza.

Katika mazingira haya, sisi Askofu hatuwezi kunyamaza. Hatuwezi kuacha kupaza sauti eti kwa sababu tulifanya vile jana! Ni nani anayeweza kufurahia mapumziko wakati jirani anaomboleza? Tunalitaka Jeshi la Polisi kumuachia Catherine Ruge na wenzake pasipo masharti ye yote. Tutunze utulivu uliopo, tusiweke mianya ya kuuondoa.

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Mwanakondoo ameshinda
 
Back
Top Bottom