Askofu Mwamakula: Matokeo ya mkataba wa milele kati ya Essau na Yakobo kwa vizazi vyao vyote!

Askofu Mwamakula: Matokeo ya mkataba wa milele kati ya Essau na Yakobo kwa vizazi vyao vyote!

Mtanzania2020

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2020
Posts
817
Reaction score
1,752
MATOKEO YA MKATABA WA MILELE KATI YA ESSAU NA YAKOBO KWA VIZAZI VYAO VYOTE!

Madhara ya mkataba kati ya Essau na Yakobo yalikuja kuonekana baadaye baada ya Essau kupoteza kabisa haki zake zote za kiutawala, kiuongozi, kiuchumi, kidiplomasia na kisiasa. Chanzo cha mkataba ule ilikuwa ni tamaa ya Essau ya kupata pesa ya kufanyia shopping, kula nyama choma na kunywa supu ya pweza.

Baada ya Yakobo kugundua kuwa Essau alitaka sana apate hela ya matanuzi na supu ya pweza, aliweka sharti la kuandikiana mkataba. Lakini kwa kuwa akili ya Essau ilikuwa katika kupata vile vitu na jinsi atakavyowalingishia wenzake wa Mesopotamia, hakuweza hata kuwa makini kuangalia vipengere vya mkataba na wala yeye hakuona shida mkataba kuandikwa na Yakobo.

Baadaye alipokuja kushtuka akakuta mkataba ulikuwa hauna ukomo - ulikuwa ni wa milele na kuwa Yakobo alikuwa amejimilikisha kila kitu. Lakini Essau alipotaka kubadili vile vipengere vibaya ndani ya mkataba, Yakobo alikataa lakini hata Mahakama ya rufani chini ya Mzee Isaka ilisema kuwa mkataba ule hauvunjiki. Mkataba ule ulipora haki zote hata za vizazi vya Essau katika nyanja zote - kidiplomasia, kiuchumi, kiutawala, kisiasa, nk (Mwanzo 25).

Wataalamu wengi wa Biblia wanakubaliana pia kuwa uzao wa Yakobo ndilo taifa la Israeli na uzao wa Essau ndilo taifa la Jordan. Je, kama hiyo ni kweli kuhusu historia ya mataifa hayo mawili yaliyo jirani, unayaonaje mahusiano ya nchi hizo mbili na hasa ushawishi wa kila nchi katika jumuiya ya kimataifa kisiasa, kiuchumi, kijeshi na kidiplomasia?

Uliwahi kusoma kisa cha Essau na Yakobo kwa jicho la mkataba? Unafahamu kuwa mikataba yote inayohusu rasilimali inahitaji umakini sana kwa kuwa mtu akikabidhiwa rasilimali haziachii kirahisi? Unafikiri ni kwa nini Yakobo aliandika mkataba mwenyewe bila kumshikirisha Essau?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 22 Julai 2023; 07:08 am
 
Askofu anababatiza visa na kuvihusianisha na analotaka watu waamini. Kiufupi kisa cha Essau na Yakobo kilikuwa ni kuonesha nguvu ya mdomo katika kujinenea maneno ambayo hugeuka balaa.

Kisa cha Yakobo na nduguye Essau hakifit kwenye jambo hili kama ambavyo askofu anataka tuamini maana hata wakati mama yake Yakobo anapanga mpango wa kumpokonya Essau haki yake kama mzaliwa wa kwanza, Yakobo alimhoji akiihofia hiyo dhambi endapo Baba yake akiigundua na Mama akamjibu lolote katika mpango ule ni juu yake.

Pengine angetuambia kisa cha Yakobo na mjomba wake Labani, ambapo walikubaliana Yakobo afanya kazi kwa miaka 7 ili apewe mke ambaye alikuwa ni moja wa binti wa Labani aitwae Rachel lakini baada ya miaka 7 Labani akampa Yakobo Leah kinyume cha makubaliano hivyo kupelekea Yakobo kufanya makubaliano mengine ile apewe Rachel. (Biblia inamuelezea Rachel alikuwa mzuri wa sura na umbo.)

Sasa hapakuwa na mkataba hapo kama anavyojaribu kutuelezea Askofu.
 
Yaani hadi wao hawaelewi ilikuaje huu mkataba ukavuja kiasi hiki. Mwarabu naye haelewi fukuto limekua kubwa hivi.

Ashukuriwe aliyevujisha hii maneno
 
Mnataka viongozi wa DINI wakae kimya hata kwenye UHARIBUFU Kama huu.Kwani kuwa Kiongozi wa DINI ni kunyamazia maovu?

Je! Kuwa Kiongozi wa dini kuwa mjinga mjinga hapa ndio ccm mnakosea kabisa.

Hivi wewe na unasoma vitabu gani hivyo wenye kuzuia Viongozi wa Dini wafunge midomo kwenye Nchi yao wakati Wana Siasa wanakula Nchi Kama mchwa anakuka nyasi?

Rudi nyuma shetani were maana huiwazii mema Nchi yetu TANGANYIKA/ TANZANIA.
 
Mama SSH na ccm yake sijui kwanini amekubali hii kitu iliyoharibu CV yake kwa kiwango kikubwa sana!
 
Una mapepo wewe mnataka viongozi wa DINI wakae kimya hata kwenye UHARIBUFU Kama huu.Kwani kuwa Kiongozi wa DINI ni kunyamazia maovu?
Je! Kuwa Kiongozi wa dini kuwa mjinga mjinga hapa ndio ccm mnakosea kabisa.

Hivi wewe na unasoma vitabu gani hivyo wenye kuzuia Viongozi wa Dini wafunge midomo kwenye Nchi yao wakati Wana Siasa wanakula Nchi Kama mchwa anakuka nyasi?

Rudi nyuma shetani were maana huiwazii mema Nchi yetu TANGANYIKA/ TANZANIA.
Tanganyika ilizikwa mwaka Aprili 1964.
 
Tanganyika ilizikwa mwaka Aprili 1964.
Hujui unachokiongea na kukitetea.
Hawa unaowachekea siku moja
Tanganyika ilizikwaje mbona bado Zanzibar Ina:-
1).Rais wake,
2).Wimbo wake
3).BUNGE lake
4).Serikali yake
5).Askari wake
Kwani ili tuipate TANZANIA formula gani ilitumika?
Usitulishe matango mwitu,TANGANYIKA bado iko hai mpaka na wajinga ndio WANAIITA TANZANIA BARA.
 
Hujui unachokiongea na kukitetea.
Hawa unaowachekea siku moja
Tanganyika ilizikwaje mbona bado Zanzibar Ina:-
1).Rais wake,
2).Wimbo wake
3).BUNGE lake
4).Serikali yake
5).Askari wake
Kwani ili tuipate TANZANIA formula gani ilitumika?
Usitulishe matango mwitu,TANGANYIKA bado iko hai mpaka na wajinga ndio WANAIITA TANZANIA BARA.
Yaani mzee baba agenda ilikuwa ni kuimeza Zanzibar moja kwa moja lakni ilipofika kooni mwa Tanganyika ikakwama chini haiendi juu hairudi nda maana unaona Muungano huu umekaa kimchongo na hauelezeki kimantiki.
Nchi mbili zikiungana huunda serikali moja au tatu. Huu Muungano wetu ulisababishwa na uroho wa Nyerere kutaka kuipora Zanzibar kitu ambacho kilimshinda hadi alipokuwa akizikwa kule bitiama hakuwa amefanikiwa.
 
Back
Top Bottom