BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
AMEGUSA KILA KITU BILA KUKISUMBUA..
Hotuba imeisha. Tumeisikia. Penye wengi kuna mengi. Nimetoka na haya:
1. Hotuba nzuri lakini ya kawaida. Wakuu wa nchi wa kawaida huongea kwa uungwana mbele ya mabunge. Yaliyo mengi tumeyashika tangu utoto. Yalienda likizo awamu ya tano.
2. Kawa jasiri kugusa demokrasia na Haki za Binadamu. Vigelegele vilipungua. Sababu ipo. Awamu iliyopita haikuwa rafiki wa demokrasia na Haki za Binadamu. Wapiga vigelegele wasingeweza kunyea mbeleko. Nampongeza hata kwa kusema. Kutenda tunasubiri.
3. Mgongano upo. Mama na yeye kitu kimoja. Mmoja adui wa demokrasia na Haki za Binadamu, mwingine rafiki. Any way, Roma haikujengwa siku moja. Tungoje hata kama matumbo yanauma.
4. Kavitaka vyombo vya haki vitoe haki kwa mujibu wa sheria. Awamu iliyopita zilipitishwa sheria nyingi mbaya na kwa haraka. Haki ipi mbele ya sheria mbaya? Sheria mbaya huzaa haki mbaya.
5. Kaahidi kukutana na vyama vya siasa. Bila shaka alimaanisha vya upinzani kwa sababu cha kwake si cha siasa ni cha dola. Ahadi inasubiriwa. Ahadi imekosa vigelegele. Walipita bila kupingwa na demokrasia ikafa bila kupingwa.
6. Mwisho wa mwezi, Mama anakalia kiti cha chama dola chetu. Baada ya hapo akutane na vyama vya siasa. Akiwa nao atasahau kuwa yeye ni Mwenyekiti wa chama dola? Mashaka ni makubwa kuliko matumaini. Nia anayo, moyo wake u radhi, lakini mwili ni dhaifu. Hata hivyo anaonekana kuwa na ngozi ngumu. Kasema ruksa kukosoa. Tumuombee.
7. Hotuba imegusa vitu vingi. Mama ahsante. Kuna vitu nimevikosa na ni haki nivikose kwa sababu hotuba sikuandaa mimi. Nilitamani:
- Katiba mpya aliyoiongoza
- Maridhiano na wahanga wa awamu
Iliyopita
- Matamko yaliyokiuka katiba na
yanaendelea kutekelezwa
- Uhuru wa vyombo vya habari.
Nina mengine, nitamtafuta mama.
Namuombea mama. Ameshikilia mustakabali wetu. Kudemka kwa bunge hakujaisha.
Kazi Iendelee
Hotuba imeisha. Tumeisikia. Penye wengi kuna mengi. Nimetoka na haya:
1. Hotuba nzuri lakini ya kawaida. Wakuu wa nchi wa kawaida huongea kwa uungwana mbele ya mabunge. Yaliyo mengi tumeyashika tangu utoto. Yalienda likizo awamu ya tano.
2. Kawa jasiri kugusa demokrasia na Haki za Binadamu. Vigelegele vilipungua. Sababu ipo. Awamu iliyopita haikuwa rafiki wa demokrasia na Haki za Binadamu. Wapiga vigelegele wasingeweza kunyea mbeleko. Nampongeza hata kwa kusema. Kutenda tunasubiri.
3. Mgongano upo. Mama na yeye kitu kimoja. Mmoja adui wa demokrasia na Haki za Binadamu, mwingine rafiki. Any way, Roma haikujengwa siku moja. Tungoje hata kama matumbo yanauma.
4. Kavitaka vyombo vya haki vitoe haki kwa mujibu wa sheria. Awamu iliyopita zilipitishwa sheria nyingi mbaya na kwa haraka. Haki ipi mbele ya sheria mbaya? Sheria mbaya huzaa haki mbaya.
5. Kaahidi kukutana na vyama vya siasa. Bila shaka alimaanisha vya upinzani kwa sababu cha kwake si cha siasa ni cha dola. Ahadi inasubiriwa. Ahadi imekosa vigelegele. Walipita bila kupingwa na demokrasia ikafa bila kupingwa.
6. Mwisho wa mwezi, Mama anakalia kiti cha chama dola chetu. Baada ya hapo akutane na vyama vya siasa. Akiwa nao atasahau kuwa yeye ni Mwenyekiti wa chama dola? Mashaka ni makubwa kuliko matumaini. Nia anayo, moyo wake u radhi, lakini mwili ni dhaifu. Hata hivyo anaonekana kuwa na ngozi ngumu. Kasema ruksa kukosoa. Tumuombee.
7. Hotuba imegusa vitu vingi. Mama ahsante. Kuna vitu nimevikosa na ni haki nivikose kwa sababu hotuba sikuandaa mimi. Nilitamani:
- Katiba mpya aliyoiongoza
- Maridhiano na wahanga wa awamu
Iliyopita
- Matamko yaliyokiuka katiba na
yanaendelea kutekelezwa
- Uhuru wa vyombo vya habari.
Nina mengine, nitamtafuta mama.
Namuombea mama. Ameshikilia mustakabali wetu. Kudemka kwa bunge hakujaisha.
Kazi Iendelee