Askofu Mwamakula: Viongozi wa dini ndani ya TBC

Askofu Mwamakula: Viongozi wa dini ndani ya TBC

BAK

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2007
Posts
124,790
Reaction score
288,165
VIONGOZI WA DINI WATUMIA TBC KUTOA MAONI YAO KUMSIFIA RAIS MAGUFULI.

Tarehe 9 Desemba 2020 majira ya Saa 9 asubuhi. Nipo katika runinga nikitazama na kuangalia kipindi maalum katika TBC. Kuna viongozi wawili wa dini, Askofu Sylivester Gamanywa wa WAPO Mission International na Sheikh Swed Twaib wa BAKWATA wanatoa maoni yao kuhusu Utendaji wa Rais Magufuli hususan Uteuzi wa Baraza la Mawaziri uliofanywa hivi karibuni. Wamesifia weredi, na umakini wa Rais katika kuunda Baraza lake la Mawaziri na kwamba amefuata viwango, vigezo na Katiba.

Hayo ni maoni ya viongozi hao wa dini. Wao wameamua kusifia na hicho walichokiona. Hatuwezi kusema wanafanya siasa au wanachanganya dini na siasa. Ni haki yao kikatiba lakini pia ni haki ya wananchi kusikia maoni ya viongozi wa dini wanaosifia utendaji wa Serikali.

Vilevile, ni vizuri tukaelewa kuwa wapo viongozi wa dini wanaotoa maoni yao kwa njia ya kukosoa, kuonya au kukemea pale wanapoona kuwa hapaendi sawa. Nao ni mtazamo wao na hatuwezi kusema kuwa wanafanya siasa au wanachanganya dini na siasa. Ni haki yao kikatiba na ni haki ya wananchi kusikia maoni ya viongozi wa dini wanaokuwa na maoni tofauti kwa kukosoa, kuonya na kukemea mambo yasiyokwenda sawa!

Tanzania tuwe tayari kusikia maoni ya viongozi wa dini yawe ya kusifia, kuonya, kukemea au kukosoa. Tunawatia moyo kuanzia Januari 2021 kujitokeza kwa wingi kusikiliza maoni ya Askofu Mwamakula kupitia "Matembezi ya Hiyari" kuhusu umuhimu wa Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Uandikwaji wa Katiba Mpya!

Mwana Kondooo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
 
Mkuu,

Kwa hiyo wewe ndiye huyu kiongozi wa kiroho-Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki?

Kama ndio wewe basi ni wazi umepwaya kuitwa kiongozi wa kiroho. Kiongozi wa kiroho anakemea na kuonya kwa HEKIMA kisha kutoa mwongozo wa nini kifanyike kwa BUSARA, lakini maandiko yako mengi yanakosa vitu hivyo. Kiongozi hana chuki na mtu wala hasira zisizo na maana lakini wewe unajionesha bayana ulivyo. Naonaujitahidi kupigania nafsi na mwili kuliko roho kama utume wa kazi ya Mungu ulivyo.

Siasa haiponeshi roho ila huburudisha hisia za kufikirika. Neno la Mungu huponesha roho, mwili na nafsi kwa kuacha matendo maovu. Duniani hakuna serikali zilizookoka ndio maana Yesu alisema ya Kaisari mpeni Kaisari na ya Mungu mpeni Mungu lakini wewe ni lukewarm katika mtazamo huo.

Mawazo yangu pia yaheshimiwe kwa kuwa ni sehemu ya kukurekebisha na wewe na usijione ni Malaika kwamba unachokisema kinawezekana umetumwa na Mungu kumbe ni hisia zako za kufikirika kwa mgongo wa haki ya itikadi kinzani.
 
Muulize kwanza wakati wanasafiri kwenye kampeni na katimba walikuwa wanalala chumba kimoja au tofauti? Na kama ni kimoja kilikuwa na vitanda vingapi?

Je mpaka sasa wanawasiliana na katimba au hapana?

Je maombi yao yalisikilizwa au mungu aliyatupilia mbali?

Je bado wanamuamini mungu kwa kila jambo au kwabaadhi ya mambo?
 
Lengo na dhumuni kuu la dini yoyote ni kuhakikisha katika jamii kuna misingi ya HAKI, tofauti na viongozi wengine wa dini Ask. Mwamakula & Ask. Niwemugizi wamekuwa taswira bora katika kipindi hiki kigumu kwa wapenda haki.
 
Ndiyo zao hao WANAFIKI.
Tatizo la Askofu nikua anatoa maonyo na kuelimisha...ila siku akisujudu na kushangilia Serikali iliyopo madarakani ...Utakua nae kwa pamoja
 
Askofu hewa huyu, ni kajinga kama wajinga wengine tu
Mmh? Jamani naona mnawashambulia maaskofu tu vp huyu nduguyngu wa bakwata ?hanaga shida et
IMG_20200924_141427_8.jpg
 
Unafiki wa hali ya juu! Kwa hiyo kwako wewe viongozi wa dini ambao wanasifia unaona wanafanya jambo jema lakini wale wanaokosoa udhalimu wa kutisha unaozidi kushamiri nchini hawastahili kufanya hivyo. Wapuuzi kama wewe ni matatizo makubwa sana Nchini na ndiyo mnaovimbisha kichwa huyo anayejiita mwendawazimu na mporaji uchaguzi.
 
Nchini na ndiyo mnaovimbisha kichwa huyo anayejiita mwendawazimu na mporaji uchaguzi.
Wote ni wavimbisha vichwa! Wewe umechagua kumvimbisha kichwa makengeza wengine wanamvimbisha kichwa jiwe, kama ni upuuzi basi wote ni wapuuzi...
 
Nimesoma makala zake huyu mchungaji atakuwa anaumwa ugonjwa wa akili na bangi za mbeya zimemjaa kwenye damu
 
Kwa UFINYU wa akili zako. Hata POPE Francis kule Vatican anakemea na kukosoa maovu mbali mbali duniani lakini akifanya hivyo Askofu Mwamakula KOSA! Kule South Africa kuna Askofu TUTU naye alikemea na anaendelea kukemea maovo mbali mbali ndani ya Afrika Kusini na kwingineko duniani ambao umemjengea umaarufu mkubwa sana katika Nchi nyingi duniani.

Nimesoma makala zake huyu mchungaji atakuwa anaumwa ugonjwa wa akili na bangi za mbeya zimemjaa kwenye damu
 
VIONGOZI WA DINI WATUMIA TBC KUTOA MAONI YAO KUMSIFIA RAIS MAGUFULI.

Tarehe 9 Desemba 2020 majira ya Saa 9 asubuhi. Nipo katika runinga nikitazama na kuangalia kipindi maalum katika TBC. Kuna viongozi wawili wa dini, Askofu Sylivester Gamanywa wa WAPO Mission International na Sheikh Swed Twaib wa BAKWATA wanatoa maoni yao kuhusu Utendaji wa Rais Magufuli hususan Uteuzi wa Baraza la Mawaziri uliofanywa hivi karibuni. Wamesifia weredi, na umakini wa Rais katika kuunda Baraza lake la Mawaziri na kwamba amefuata viwango, vigezo na Katiba.

Hayo ni maoni ya viongozi hao wa dini. Wao wameamua kusifia na hicho walichokiona. Hatuwezi kusema wanafanya siasa au wanachanganya dini na siasa. Ni haki yao kikatiba lakini pia ni haki ya wananchi kusikia maoni ya viongozi wa dini wanaosifia utendaji wa Serikali.

Vilevile, ni vizuri tukaelewa kuwa wapo viongozi wa dini wanaotoa maoni yao kwa njia ya kukosoa, kuonya au kukemea pale wanapoona kuwa hapaendi sawa. Nao ni mtazamo wao na hatuwezi kusema kuwa wanafanya siasa au wanachanganya dini na siasa. Ni haki yao kikatiba na ni haki ya wananchi kusikia maoni ya viongozi wa dini wanaokuwa na maoni tofauti kwa kukosoa, kuonya na kukemea mambo yasiyokwenda sawa!

Tanzania tuwe tayari kusikia maoni ya viongozi wa dini yawe ya kusifia, kuonya, kukemea au kukosoa. Tunawatia moyo kuanzia Januari 2021 kujitokeza kwa wingi kusikiliza maoni ya Askofu Mwamakula kupitia "Matembezi ya Hiyari" kuhusu umuhimu wa Kuunda Tume Huru ya Uchaguzi na Uandikwaji wa Katiba Mpya!

Mwana Kondooo Ameshinda! Tumfuate!

Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
We askofu una..rwa
 
Back
Top Bottom