BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,165
MOYO WA ASKOFU MWAMAKULA KWA TAIFA
Unatafuta kuongoza Kitongoji, Kijiji, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na hata Taifa. Lakini unapanda miiba njiani ili kuwazuia washindani wako. Unatafuta uteuzi au hata ushindani wa kibiashara au unatafuta kushinda tenda Serikalini, lakini unatega mabomu ili kutaka kuwalipua washindani wako! Unataka nafasi ya kisiasa katika Chama chako, lakini unatembea na ndoo ya maji taka ili kummwagia mtu ye yote utakayekutana naye njiani. Unataka anuke ili asichaguliwe!
Ukishindwa kufanikisha hayo yote, miiba yako ikioza, mabomu yako yakishindwa kulipuka, maji taka yasipowapata walengwa; unabuni mbinu nyingine! Unaharibu biashara za washindani wako au hata unahakikisha wamefukuzwa kazi! Unamrushia jini mshindani wako. Likimkosa, unamuandalia sumu, ili aangamie kabisa. Vyote hivyo vikishindikana, unatafuta watu wasiojulikana unawalipa pesa ili wammalize kwa risasi!
Unafanya yote haya ili upande juu, ili upate uongozi, ili ushinde ushindani wa kibiashara! Ukifanikiwa katika adhma yako, unasahau kurudi nyuma kuja kuondoa miiba uliyoipanda njiani na unasahau hata kuja kutegua mabomu uliyotega. Hata kukumbuka kuja kuwanunulia sabuni wale uliowamwagia maji taka ili angalau waoge unashindwa! Si ukimbuke basi hata kuwatunza wale yatima, wajane na wagane wa wale uliowaua?
Jamii ikiwa na viongozi wa namna hii haiwezi kupata ustawi. Viongozi ambao wamejenga maadui kila mahali walikopita watatumia nafasi zao ili kujilinda na kudhibiti wengine. Uadui, chuki na visasi hutawala katika jamii. Kila kiongozi anapokuja atafichua uovu wa aliyetangulia kwa kuwa aliyetangulia alijikita zaidi katika kudhibiti wengine na kujilinda yeye.
Askofu Mwamakula ni ishara kwenu katika zamani hizi! Huu ujumbe unawahusu wengi usije ukafikiri unakwenda kwa Mayasa au Ndunguru! Ingawa ujumbe huu unawagusa sana wanasiasa, wafanyakazi na wafanyabiashara; viongozi wa Dini hawawezi kujitenga nao! Kwa sababu nao kwao yamesikika hayo hasa wale ambao nafasi za uongozi wa juu hupatikana kwa njia ya Uchaguzi.
Msihangaike na maumbile ya Askofu Mwamakula! Hangaikeni na ujumbe anaouwasilisha kwenu! Na ninyi CCM, ambao keshokutwa mna vikao nyeti! Dondosheni hizo ndoo zenu za maji taka! Mnabeba miiba ya nini enyi Vijana wa BAVICHA wakati wa kumtafuta Katibu Mkuu? Wanawake wanajulikana kwa huruma na ni walezi wazuri, hivyo hatutegemei watu wa BAWACHA kubeba mabomu wakati mnakwenda kumtafuta kiongozi wenu!
Naitamani siku ambapo nchi hii itatabasamu! Siku ambapo washauri wa Rais Samia watamtia moyo Mheshimiwa Rais kuwaongoza viongozi wa vyama vyote vya siasa nchini katika kuzika tofauti za kisiasa kwa njia ya maridhiano! Siku ambayo milango ya Magereza itakapotema mahabusu wote waliopelekwa kule kama njia ya kuwakomoa na kuwadhibiti! Machozi yanalowesha karatasi yangu! Nalazimika kunyamala! Nanyamaza! Ngubatama! Ngibile (Ezekieli 33:1-20).
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki
Unatafuta kuongoza Kitongoji, Kijiji, Kata, Jimbo, Wilaya, Mkoa na hata Taifa. Lakini unapanda miiba njiani ili kuwazuia washindani wako. Unatafuta uteuzi au hata ushindani wa kibiashara au unatafuta kushinda tenda Serikalini, lakini unatega mabomu ili kutaka kuwalipua washindani wako! Unataka nafasi ya kisiasa katika Chama chako, lakini unatembea na ndoo ya maji taka ili kummwagia mtu ye yote utakayekutana naye njiani. Unataka anuke ili asichaguliwe!
Ukishindwa kufanikisha hayo yote, miiba yako ikioza, mabomu yako yakishindwa kulipuka, maji taka yasipowapata walengwa; unabuni mbinu nyingine! Unaharibu biashara za washindani wako au hata unahakikisha wamefukuzwa kazi! Unamrushia jini mshindani wako. Likimkosa, unamuandalia sumu, ili aangamie kabisa. Vyote hivyo vikishindikana, unatafuta watu wasiojulikana unawalipa pesa ili wammalize kwa risasi!
Unafanya yote haya ili upande juu, ili upate uongozi, ili ushinde ushindani wa kibiashara! Ukifanikiwa katika adhma yako, unasahau kurudi nyuma kuja kuondoa miiba uliyoipanda njiani na unasahau hata kuja kutegua mabomu uliyotega. Hata kukumbuka kuja kuwanunulia sabuni wale uliowamwagia maji taka ili angalau waoge unashindwa! Si ukimbuke basi hata kuwatunza wale yatima, wajane na wagane wa wale uliowaua?
Jamii ikiwa na viongozi wa namna hii haiwezi kupata ustawi. Viongozi ambao wamejenga maadui kila mahali walikopita watatumia nafasi zao ili kujilinda na kudhibiti wengine. Uadui, chuki na visasi hutawala katika jamii. Kila kiongozi anapokuja atafichua uovu wa aliyetangulia kwa kuwa aliyetangulia alijikita zaidi katika kudhibiti wengine na kujilinda yeye.
Askofu Mwamakula ni ishara kwenu katika zamani hizi! Huu ujumbe unawahusu wengi usije ukafikiri unakwenda kwa Mayasa au Ndunguru! Ingawa ujumbe huu unawagusa sana wanasiasa, wafanyakazi na wafanyabiashara; viongozi wa Dini hawawezi kujitenga nao! Kwa sababu nao kwao yamesikika hayo hasa wale ambao nafasi za uongozi wa juu hupatikana kwa njia ya Uchaguzi.
Msihangaike na maumbile ya Askofu Mwamakula! Hangaikeni na ujumbe anaouwasilisha kwenu! Na ninyi CCM, ambao keshokutwa mna vikao nyeti! Dondosheni hizo ndoo zenu za maji taka! Mnabeba miiba ya nini enyi Vijana wa BAVICHA wakati wa kumtafuta Katibu Mkuu? Wanawake wanajulikana kwa huruma na ni walezi wazuri, hivyo hatutegemei watu wa BAWACHA kubeba mabomu wakati mnakwenda kumtafuta kiongozi wenu!
Naitamani siku ambapo nchi hii itatabasamu! Siku ambapo washauri wa Rais Samia watamtia moyo Mheshimiwa Rais kuwaongoza viongozi wa vyama vyote vya siasa nchini katika kuzika tofauti za kisiasa kwa njia ya maridhiano! Siku ambayo milango ya Magereza itakapotema mahabusu wote waliopelekwa kule kama njia ya kuwakomoa na kuwadhibiti! Machozi yanalowesha karatasi yangu! Nalazimika kunyamala! Nanyamaza! Ngubatama! Ngibile (Ezekieli 33:1-20).
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki