5th December 2009
Baada ya Mbuge wa sasa wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia (CCM), Ephraim Madeje, kutangaza kuwa hatagombea tena ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani, Askofu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Peter Mwamasika, ametangaza nia yake ya kugombea kiti hicho.
Dk. Mwamasika, alisema jana kuwa alikuwa anatafuta jimbo ambalo angeweza kugombea nafasi ya ubunge na kwa kuwa Mbunge wa Dodoma Mjini ametangaza kutokugombea ni wazi sasa ana haki ya kuchukua nafasi hiyo.
Alieleza kuwa pamoja na kuwa ni mstaafu katika nafasi ya uaskofu lakini bado ana uwezo wa kuwa mwanasiasa kwani hata kabla ya kushika nafasi ya uaskofu, alishawahi kuwa mbunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Iringa Vijijini.
Askofu Mwamasika alisema kuwa ana kila sasabu ya kugombea Jimbo la Dodoma Mjini kutokana na wabunge wengi ambao wametangulia kutoleta maendeleo ya kweli katika jimbo hilo wakati lina rasilimali nyingi ambazo kama zikitumiwa vizuri, zinaweza kuwaondolea wananchi umasikini unaowakabili.
Aliongeza kuwa pamoja na serikali kuanzisha mkakati wa Kilimo Kwanza, lakini mkakati huo unaonekana kuwa itakuwa vigumu kuutekeleza kwani wananchi bado hawajaweza kupatiwa elimu ya kilimo na kupewa pembejeo za kutosha.
Askofu huyo mstaafu alisema kuwa inashangaza kuona wakazi wengi wa Dodoma wanaendelea kuwa ombaomba wakati wana utajiri mkubwa ambao unaweza kuwafanya kuishi maisha mazuri lakini kila mbunge ambaye ameshika nafasi hiyo amekuwa akijisahau na kuingia bungeni kama sehemu ya kujipatia maslahi yake binafsi.
Askofu Mwamasika alifafanua kuwa ili wakazi wa Dodoma waweze kuishi maisha mazuri na wakubaliane na sera ya serikali ni lazima wawezeshwe katika kufufua kilimo cha zabibu na wapatiwe soko la uhakikika la zao hilo.
Aidha, alisema kuwa Mkoa wa Dodoma una fursa nyingi na kiongozi ambaye anaongoza mji wa Dodoma anatakiwa kuwa mbunifu na mwenye uwezo wa kutafuta wafadhili ambao wanaweza kupeleka maendeleo katika jimbo hilo.
Alisema katika uongozi wake wa miaka 20 ambayo ameitumikia Dayosisi ya Dodoma, ameweza kubadilisha maisha ya waumini wa kanisa hilo na sasa hakuna muumini ambaye hana maendeleo.
Alibainisha kuwa kutokana na jitihada zake za kutafuta maendeleo ya watu wake, alifanya juhudi ya kujenga hospitali yenye hadhi ya rufaa na kuanzisha kiwanda cha maji ya A-Sante ambayo yanapatikana katika kijiji cha Ntyuka na kwamba wafanyakazi wa kiwanda hicho ni wenyeji wa kijiji hicho.
Alisema kuwa mgombea wa nafasi ya ubunge anatakiwa kujitambua na kuelewa kuwa ni mtumishi wa watu badala ya kuwa mtawala na kuhakikisha anatetea maslahi ya wananchi.
Ni lazima kusimama kidete kuhakikisha nchi inafanikisha kuwawajibisha wale wote ambao wanaitwa mafisadi ambao mimi huwa nawaita wahujumu uchumi, alisema Askofu Mwamasika, ambaye mara nyingi hukemea maovu katika jamii.
Hata hivyo, alisema CCM inatakiwa kuonyesha ujasiri katika kuwawajibisha wale wote wenye tuhuma za kweli za vitendo vya ufisadi ili wananchi waweze kuwa na imani na serikali iliyoko madarakani.
CHANZO: NIPASHE:
Mheshimiwa Askofu anamalengo mazuri na inaonekana amejitahidi kufanya maendeleo kipindi cha uaskofu wake...
swali la msingi mbona hajazunguzia alifanya nini alipokuwa mbunge wa Iringa Mjini maana ndo post inafanana na anayoitaka sasahivi...
Asije akapata ubunge akapoteza malengo yake akatumbukia kwenye ufisadi..
kila la heri askofu
Baada ya Mbuge wa sasa wa Jimbo la Dodoma Mjini kupitia (CCM), Ephraim Madeje, kutangaza kuwa hatagombea tena ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani, Askofu mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Peter Mwamasika, ametangaza nia yake ya kugombea kiti hicho.
Dk. Mwamasika, alisema jana kuwa alikuwa anatafuta jimbo ambalo angeweza kugombea nafasi ya ubunge na kwa kuwa Mbunge wa Dodoma Mjini ametangaza kutokugombea ni wazi sasa ana haki ya kuchukua nafasi hiyo.
Alieleza kuwa pamoja na kuwa ni mstaafu katika nafasi ya uaskofu lakini bado ana uwezo wa kuwa mwanasiasa kwani hata kabla ya kushika nafasi ya uaskofu, alishawahi kuwa mbunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Iringa Vijijini.
Askofu Mwamasika alisema kuwa ana kila sasabu ya kugombea Jimbo la Dodoma Mjini kutokana na wabunge wengi ambao wametangulia kutoleta maendeleo ya kweli katika jimbo hilo wakati lina rasilimali nyingi ambazo kama zikitumiwa vizuri, zinaweza kuwaondolea wananchi umasikini unaowakabili.
Aliongeza kuwa pamoja na serikali kuanzisha mkakati wa Kilimo Kwanza, lakini mkakati huo unaonekana kuwa itakuwa vigumu kuutekeleza kwani wananchi bado hawajaweza kupatiwa elimu ya kilimo na kupewa pembejeo za kutosha.
Askofu huyo mstaafu alisema kuwa inashangaza kuona wakazi wengi wa Dodoma wanaendelea kuwa ombaomba wakati wana utajiri mkubwa ambao unaweza kuwafanya kuishi maisha mazuri lakini kila mbunge ambaye ameshika nafasi hiyo amekuwa akijisahau na kuingia bungeni kama sehemu ya kujipatia maslahi yake binafsi.
Askofu Mwamasika alifafanua kuwa ili wakazi wa Dodoma waweze kuishi maisha mazuri na wakubaliane na sera ya serikali ni lazima wawezeshwe katika kufufua kilimo cha zabibu na wapatiwe soko la uhakikika la zao hilo.
Aidha, alisema kuwa Mkoa wa Dodoma una fursa nyingi na kiongozi ambaye anaongoza mji wa Dodoma anatakiwa kuwa mbunifu na mwenye uwezo wa kutafuta wafadhili ambao wanaweza kupeleka maendeleo katika jimbo hilo.
Alisema katika uongozi wake wa miaka 20 ambayo ameitumikia Dayosisi ya Dodoma, ameweza kubadilisha maisha ya waumini wa kanisa hilo na sasa hakuna muumini ambaye hana maendeleo.
Alibainisha kuwa kutokana na jitihada zake za kutafuta maendeleo ya watu wake, alifanya juhudi ya kujenga hospitali yenye hadhi ya rufaa na kuanzisha kiwanda cha maji ya A-Sante ambayo yanapatikana katika kijiji cha Ntyuka na kwamba wafanyakazi wa kiwanda hicho ni wenyeji wa kijiji hicho.
Alisema kuwa mgombea wa nafasi ya ubunge anatakiwa kujitambua na kuelewa kuwa ni mtumishi wa watu badala ya kuwa mtawala na kuhakikisha anatetea maslahi ya wananchi.
Ni lazima kusimama kidete kuhakikisha nchi inafanikisha kuwawajibisha wale wote ambao wanaitwa mafisadi ambao mimi huwa nawaita wahujumu uchumi, alisema Askofu Mwamasika, ambaye mara nyingi hukemea maovu katika jamii.
Hata hivyo, alisema CCM inatakiwa kuonyesha ujasiri katika kuwawajibisha wale wote wenye tuhuma za kweli za vitendo vya ufisadi ili wananchi waweze kuwa na imani na serikali iliyoko madarakani.
CHANZO: NIPASHE:
Mheshimiwa Askofu anamalengo mazuri na inaonekana amejitahidi kufanya maendeleo kipindi cha uaskofu wake...
swali la msingi mbona hajazunguzia alifanya nini alipokuwa mbunge wa Iringa Mjini maana ndo post inafanana na anayoitaka sasahivi...
Asije akapata ubunge akapoteza malengo yake akatumbukia kwenye ufisadi..
kila la heri askofu