Askofu Mwingira avunja nyumba za wananchi Handeni. Mkuu wa wilaya aamuru Askofu akamatwe

Askofu Mwingira avunja nyumba za wananchi Handeni. Mkuu wa wilaya aamuru Askofu akamatwe

MKATA KIU

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2010
Posts
3,410
Reaction score
8,184
Watumishi wa Mungu wanagombania pesa na mali, mchungaji anagombania ardhi ya wananchi. Mwingira wa Efatha anatia aibu watumishi.

Hapo unakuta kuna wamama wanaamini Mwingira ndio mlezi wao wa kiroho wa kuwafikisha mbinguni, huku mchungaji mwenyewe anavunja nyumba za wananchi ili apate ardhi.


 
Hapo sidhani kama kuna kesi ila ukute wananchi ndiyo dizaini ya wale wanaouza ardhi na kutakiwa kuhama ila wanajibu, ngoja tunajenga huko makazi mapya.

Mfanyabiashara muwekezaji ndg mchungaji anakuja kutaka kuwekeza kwenye eneo lake, anaonekana mbaya.

Note this na subiri jibu siku si nyingi.
 
Mkuu mbona unatoa taarifa huku unaonekana Una chuki na upande mmoja.....hayo makanisa si yanajengwa juu ya ardhi..... kwanini wasiwe au wasimiliki ardhi........

Hata yeye ana haki ya kumiliki ardhi kulingana na sheria na utaratibu wa nchi.......

Jitahidi unapotoa habari ujitenge na mihemko unaweza ukaonekana unapiga majungu badala ya kuleta habari........
 
Watumishi wa Mungu wanagombania pesa na mali, mchungaji anagombania ardhi ya wananchi. Mwingira wa efatha anatia aibu watumishi

Hapo unakuta kuna wamama wanaamini mwingira ndio mlezi wao wa kiroho wa kuwafikisha mbinguni, huku mchungaji mwenyewe anavunja nyumba za wananchi ili apate ardhi


View attachment 3010162
Je, hawo wananchi wenye akili ma vi kama za CCM ikiwa wao ndio wamevamia viwanja vya Mwingira wakajenga kwa nguvu ulitaka awachekee?
 
Mkuu mbona unatoa taarifa huku unaonekana Una chuki na upande mmoja.....hayo makanisa si yanajengwa juu ya ardhi..... kwanini wasiwe au wasimiliki ardhi........

Hata yeye ana haki ya kumiliki ardhi kulingana na sheria na utaratibu wa nchi.......

Jitahidi unapotoa habari ujitenge na mihemko unaweza ukaonekana unapiga majungu badala ya kuleta habari........
Mkuu umeongea ukweli tupu. Sasa kama wananchi wamevamia maeneo yake alitaka awachekee ili iweje?
 
Mkuu umeongea ukweli tupu. Sasa kama wananchi wamevamia maeneo yake alitaka awachekee ili iweje?
Hakika ndugu......

Hawa wanaojiita wanyonge wanapenda sana kulalamika ili waonewe huruma hata kama haki si yao..........

Hata mtoa mada anaonekana ndio wale wale wanaojiita wanyonge........

Kupitia kichwa chake ameshaendesha kesi na ameshatoa hukumu..........
 
Sipendi kuchangia thread kama hizi lakini kwa hili la Mwingira itabidi. Hii si mara ya kwanza Mwingira anaingia kwenye migogoro na waumini wake juu ya viwanja. Huyu ni tapeli anatumia imani za watu vibaya kuwatapeli ardhi, na anapaswa ashitakiwe kwa wizi wa kuaminiwa.

Wale walio tasnia ya sheria watakumbuka Mwingira alifanikiwa kumuingiza Advocate Hubert Mbuya (alishakufa) kwenye kanisa lake na akawa rafiki wa kanisa. Alipojua Mbuya ana kiwanja kikubwa pale Kawe akamshawishi akitoe "kwa ajili ya Mungu". Mbuya akakubali kutoa kiwanja chake bure na kumkabidhi Mwingira kitumike kwa ajili ya kazi za Mungu.

Sasa baadae ilikuja kujulikana kuwa Mwingira alikuwa anajifanya yuko karibu na Mbuya kumbe alikuwa anatembea na mke wa Mbuya. Mbuya alipopata taarifa alidai Mwingira amrudishie kiwanja chake kwa sababu yeye sio mtumishi wa kweli wa Mungu, ni tapeli. Mwingira aligoma kurudisha kiwanja.

Mbuya alimshitaki Mwingira mahakamani lakini alishindwa ile kesi, kwa sababu alipomkabidhi kiwanja hakuna mahali makabidhiano yalisema nikitembea na mke wako itabidi nirudishe kiwanja. Mahakama iliona kuwa suala la Mwingira kutembea na mke wa Mbuya halikuhusiana na mkataba wa Mbuya kutoa kiwanja chake.

Mwingira alikuwa mjanja wa kukabidhiana kiwanja kwa maandishi, naona ndilo alilowafanyia hawa watu huko. Ni tapeli huyu anapaswa kukamatwa na kuwekwa ndani
 
Hapo sidhani kama kuna kesi ila ukute wananchi ndiyo dizaini ya wale wanaouza ardhi na kutakiwa kuhama ila wanajibu, ngoja tunajenga huko makazi mapya.

Mfanyabiashara muwekezaji ndg mchungaji anakuja kutaka kuwekeza kwenye eneo lake, anaonekana mbaya.

Note this na subiri jibu siku si nyingi.

Mbona kesi za ardhi zinamuandama sana huyu Mchungaji? Kulikoni?
 
Sipendi kuchangia thread kama hizi lakini kwa hili la Mwingira itabidi. Hii si mara ya kwanza Mwingira anaingia kwenye migogoro na waumini wake juu ya viwanja. Huyu ni tapeli anatumia imani za watu vibaya kuwatapeli ardhi, na anapaswa ashitakiwe kwa wizi wa kuaminiwa.

Wale walio tasnia ya sheria watakumbuka Mwingira alifanikiwa kumuingiza Advocate Hubert Mbuya (alishakufa) kwenye kanisa lake na akawa rafiki wa kanisa. Alipojua Mbuya ana kiwanja kikubwa pale Kawe akamshawishi akitoe "kwa ajili ya Mungu". Mbuya akakubali kutoa kiwanja chake bure na kumkabidhi Mwingira kitumike kwa ajili ya kazi za Mungu.

Sasa baadae ilikuja kujulikana kuwa Mwingira alikuwa anajifanya yuko karibu na Mbuya kumbe alikuwa anatembea na mke wa Mbuya. Mbuya alipopata taarifa alidai Mwingira amrudishie kiwanja chake kwa sababu yeye sio mtumishi wa kweli wa Mungu, ni tapeli. Mwingira aligoma kurudisha kiwanja.

Mbuya alimshitaki Mwingira mahakamani lakini alishindwa ile kesi, kwa sababu alipomkabidhi kiwanja hakuna mahali makabidhiano yalisema nikitembea na mke wako itabidi nirudishe kiwanja. Mahakama iliona kuwa suala la Mwingira kutembea na mke wa Mbuya halikuhusiana na mkataba wa Mbuya kutoa kiwanja chake.

Mwingira alikuwa mjanja wa kukabidhiana kiwanja kwa maandishi, naona ndili alilowafanyi ahawa watu huko. Ni tapeli huyu anapaswa kukamatwa na kuwekwa ndani

Ile bank ya Efatha aliwapiga sana wajinga wajinga wanaopenda maajabu. Waliwekeza bank ikafa kifo cha mende
 
Mkuu mbona unatoa taarifa huku unaonekana Una chuki na upande mmoja.....hayo makanisa si yanajengwa juu ya ardhi..... kwanini wasiwe au wasimiliki ardhi........

Hata yeye ana haki ya kumiliki ardhi kulingana na sheria na utaratibu wa nchi.......

Jitahidi unapotoa habari ujitenge na mihemko unaweza ukaonekana unapiga majungu badala ya kuleta habari........
Nakazia hoja.
Najaribu kupata picha ya Askofu akiwa active ameshika nyundo au mtalimbo akivunja nyumba za Wananchi.
 
Nilisoma mahali Huko Rukwa nako amefunguliwa kesi ya kupora ardhi ya watu.
Sidhani kama iko hivyo kama inavyoripotiwa. Isije kuwa watu wanamwuzia ardhi halafu baadaye wanarudi kinyume-nyume kutaka kuitumia hiyo ardhi ilhali walishalamba asali.
 
Sidhani kama iko hivyo kama inavyoripotiwa. Isije kuwa watu wanamwuzia ardhi halafu baadaye wanarudi kinyume-nyume kutaka kuitumia hiyo ardhi ilhali walishalamba asali.
Fuatilia vizuri kuna maeneo mengi ana migogoro ya ardhi, nadhani anaipata kwa ujanja ujanja.
 
Kuna wananchi huwa wanauza maeneo yao halafu hawami haraka kumpisha waliomuuzia, kinachofuata ni kubomolewa magofu kwa nguvu
 
Back
Top Bottom