Daniel Mwinula
JF-Expert Member
- Jul 15, 2012
- 302
- 328
Ni jambo la kheri na la kutia moyo kuona nchi zetu za Afrika Mashariki zimechaguliwa ku-host mashindano ya AFCON. Hapo tunatakiwa kujiandaa kwa vitu vikubwa viwili, VIWANJA BORA na TIMU BORA….!!!
Binafsi ningetamani sana atafutwe kocha MAPEMA mwenye uwezo wa kubadilisha kabisa mpira wetu tuliouzoea, na kujenga timu bora itakayoweza kuleta changamoto CHANYA katika mashindano hayo…!!!
Naamini kocha mgeni mwenye kariba ya kocha Nabi (kwa mfano), anaweza kusaidia kujenga timu vizuri sana endapo atafanikiwa kukaa na timu kuanzia mapema. Nimesema Nabi kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba Nabi alijitahidi kuleta changamoto fulani TOFAUTI na tulivyokuwa tumezoea.
Au combination ya mgeni na mzawa kama Mgunda, binafsi naamini kwa muda uliobaki wanaweza wakatengeneza timu INAYOELEWEKA, huku tukiamini kwamba wachezaji waliopo kwa sasa UMRI UNAELEKEA KUWATUPA MKONO….!!!
Wapewe kazi ya kufanya scouting ya kutosha kutafuta vipaji vipya na kupika timu mpya nzuri kwa muda wa miaka mi3 iliyobaki INATOSHA KABISA….!!
Yangu ni hayo tu….!!!
Binafsi ningetamani sana atafutwe kocha MAPEMA mwenye uwezo wa kubadilisha kabisa mpira wetu tuliouzoea, na kujenga timu bora itakayoweza kuleta changamoto CHANYA katika mashindano hayo…!!!
Naamini kocha mgeni mwenye kariba ya kocha Nabi (kwa mfano), anaweza kusaidia kujenga timu vizuri sana endapo atafanikiwa kukaa na timu kuanzia mapema. Nimesema Nabi kwa sababu ni ukweli usiopingika kwamba Nabi alijitahidi kuleta changamoto fulani TOFAUTI na tulivyokuwa tumezoea.
Au combination ya mgeni na mzawa kama Mgunda, binafsi naamini kwa muda uliobaki wanaweza wakatengeneza timu INAYOELEWEKA, huku tukiamini kwamba wachezaji waliopo kwa sasa UMRI UNAELEKEA KUWATUPA MKONO….!!!
Wapewe kazi ya kufanya scouting ya kutosha kutafuta vipaji vipya na kupika timu mpya nzuri kwa muda wa miaka mi3 iliyobaki INATOSHA KABISA….!!
Yangu ni hayo tu….!!!