Ataka kujiua kwa kujikata koromea

Ataka kujiua kwa kujikata koromea

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
1660720069106.png

James Msengi Mkazi wa Tabora anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40 amenusurika kifo baada ya kujaribu kujiua kwa kujikata na kisu shingoni akiwa kwenye kituo cha Mabasi cha Msamvu mkoani Morogoro.

Majeruhi huyo ambaye amesema alikuwa anasafairi kutoka Dar es salaam kuelekea kwao Tabora lakini alipofika katika kituo hicho cha mabasi aliamua kujikata kwa makusudi shingoni kwa lengo la kujiua kutokana na ugumu wa maisha ambao ulisababishwa na kukosa ajira.

Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro Scholastika Ndunga amethibitisha kumpokea Majeruhi akiwa katika hali mbaya na kutokwa na damu nyingi shingoni ambaye alianza kupatiwa matibabu na sasa anaendelea vizuri.

Shuhuda wa tukio hilo Mzee Ibrahim Omary ambaye Majeruhi alitumia kisu chake cha kuuzia miwa kujikata koromeo amesema kuwa Mtu huyo alifika katika eneo analofanyia biashara na kutaka auziwe muwa ambao haujamenywa lakini walishangaa baada ya kupewa kisu akaanza kujichinja.
 
hayupo sawa! sirikali imsaidie...

ingawa mental health ni kitu ambacho nchi za kiafrica haziwekei maanani sana!

ni balaa la bara katika miaka ijayo!
 
[Morogoro] Msomi ajikata koromeo katika kituo Cha mabasi kutokana na kukosa ajira na ugumu wa maisha
ANGALIA VIDEO
 
James Msengi Mkazi wa Tabora anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 40 amenusurika kifo baada ya kujaribu kujiua kwa kujikata na kisu shingoni akiwa kwenye kituo cha Mabasi cha Msamvu mkoani Morogoro.
At 40 mtu anapaswa kuwa ametulia kimaisha. Lkn jamaa ndiyo kwanza anatafuta ajira. Hivi hii kauli ya " life begins at 40" inafanya kazi Afrika??
 
Familia yake itafutwe,tujue shida zaidi alizonazo.
Kama ni ajira, serikali iangalie namna ya kumsaidia.
Hapa ndipo namlaumu Magufuli.
Alivuruga mfumo wa ajira kwa ujinga wake tu.
 
Back
Top Bottom